Eric Cartman
JF-Expert Member
- May 21, 2009
- 11,966
- 11,218
Nafikiri kama taifa tumefika sehemu ambayo Mahakama haziheshimiwi Tena na viongozi wetu...Rais kasema '' Kama asingevunja sheria tungekuwa naye hapa''
Kauli hii inafanana na ile ya BBC kwa mantiki
Kwamba Rais anaongelea suala lililopo mahakamani. Pili Rais anamtuhumu Mbowe .
Akiwa mkuu wa nchi tayari ana influence maamuzi ya mahakama kwamba,Mbowe ana makosa . Ni Jaji gani Tanzania atakayekwenda kinyume na Rais?
Waliambiwa '' hukumu zenu zizingatie hali ya nchi''
Rais anasema ' kuna kusameheana''.
Kusamehe kunatokea penye kosa, tayari keshamtia Mbowe hatiani na anataka kumsamehe.
Nadhani anapoongea kwa hasira anasahau ni Rais na hivyo kueleza hisia zake na kusahau nafasi yake. Kauli zake za leo hazikumtendea haki Mbowe , zimeingilia mahakama.
Hivi kwanini Wasadizi wa Rais hawamshauri kuhusu masuala ya mahakamani?
Hivi CJ ana maoni gani kuhusu hili na kwamba ameshindwa hata kumnong'oneza
Alinda JokaKuu
Hii inanikumbusha CHADEMA NA MH. EDO bila shaka sio Mh. RAIS tu ndio hulka za wanasiasa wetu.Kwa Tanganyika hii tunabahati mbaya sana kuwa na rais ambae anasahau Jana alisema nini na leo atasema nini ?
Sheria inasema . mtu anabaki bila hatia hadi pale mahakama itakapothibitisha.Sawa mkuu......
Tujikite kwenye mzizi wa mada hii.....
Kuratibu au kuendesha vitendo vya kigaidi ni kosa kisheria na anayefanya anakuwa amevunja sheria.......kauli ya raisi kuwa kama hangevunja sheria angekuwa hapa nadhani ameakisi na kesi inayoendelea mahakamani dhidi ya tuhuma za Mbowe.......
Mahakama gani imethibitisha uvunjaji wa sheria na nani alihusikaKuheshimu sheria ni pamoja na kujipusha na vitendo au matukio yanayopelekea uvunjifu wa sheria......
Well, Rais alsema wenzake wa,eshafungwa, alimhukumu nje ya mahakama. Jana kasema asingevunja sheria, kamuhukumu nje ya mahakama!Kwa mujibu wa utaratibu wa nchi yetu mahakama pekee ndio chombo Cha kutoa haki.....
Rais anamsamehe vipi mtu ambaye hajathibitika ana makosa? Hivi wewe kuna mtu anaweza kukusamehe hapo ulipo! Mbowe hajapatikana na hatia hivi anasamehewa kwa kosa gani na kutoka mahakama gani?Kuhusu kusameheana bila shaka amelenga mamlaka aliyokuwa nayo kama mkuu wa nchi kuhusu misamaha dhidi ya wafungwa na sio kesi zinazoendelea mahakamani.......
Kesi ya Mbowe imefunua Mahakama na jinsi inavyotumika na vyombo vya UmmaNafikiri kama taifa tumefika sehemu ambayo Mahakama haziheshimiwi Tena na viongozi wetu...
Kesi hii Rais ameiingilia sana, hukumu yoyote itahusishwa na kauli za RaisKipindi cha nyuma tulizoea kusikia kesi iko Mahakamani hivyo siwezi iongelea... Tofauti na Sasa Viongozi wetu ndo wamekuwa wapanda majukwaa na kutoka maelezo ni nini kifanyike na nini kisifanyike Mahakamani, na hapo hapo wanatuhimizi Sisi wananchi tusio na vyeo Tena kwa msisitizo kuheshimu sheria...
Tunasababu za kumlaani mkoloniBado nawaza Tanzania miaka 60 ya uhuru....
Mimi ningependa Mbowe afungwe jela na kifungo chake ndicho kitapelekea Watanzania kwa wingi kukiondoa chama changu cha CCM madarakani kwenye uchaguzi ujao wa mwaka 2025.
Huu ni mtizamo wangun
Hiyo ni trick tu ya kujikosha ,na Zito anafanya kazi maalumu ya mamlaka,maana wanaotafuta namna ya kuifuta hiyo kesi kidizainiBi mkubwa kashaanza kulegea