Rais Samia fanya mpango utupunguzie wakulima huu mzigo

Rais Samia fanya mpango utupunguzie wakulima huu mzigo

Ndenji five

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2021
Posts
1,985
Reaction score
3,109
Pole na hongera kwa kutimiza majukumu ya nchi.

Mheshimiwa rais kilio chetu wakulima ni kile kile.

Pembejeo zipo juu sana mama hasa mbolea na inazidi kupanda kila kukicha mpaka kufikia sasa.

Urea imefikia laki na elfu ishirini. Mama hii ni bei kubwa sana kwetu wakulima wadogo.

Mheshimiwa raisi fanya jambo maana hata ile pesa uliotoa kwa NFRA kwaajili ya ununuzi wa maind haijasaidia chochote wamenufaika wachache hasa wakulima wakubwa na wafanyabishara.

Mheshimiwa rais nilisikia tetesi yakuwa serikali yako imewakataza wafanyabishara walio taka kutushushia mbolea bei ila sikutaka kuamini hizi tetesi.

Mheshimiwa kama mbolea huko nchi za wenzetu ni ghali fanya jambo japo kwenye hizi viwanda zetu tia japo kahela ili kusaidia huu ukali wa gharama na mfumuko huu wa mbolea.

Mheshimiwa raisi angalia hili kwa jicho la tatu najua una taarifa za nchi ambazo zime asilika na njaa na ambazo zinapambana hivi sasa na njaa.

Mheshimiwa rais njaa ikiingia hapa nchini hakuna ataejua umejenga shule hakuna ataejali unakopa ili kujenga barabara.

Mheshimiwa rais najua labda serikali yako inajivunia hiyo akiba mliyo ikusanya NFRA ila tumia tu akili je hiyo akiba inaweza kulisha watanzania wote mpaka kukuta msimu mwingine.

Mheshimiwa rais fanya jambo leo hutaona madhara ya wakulima kuto kurudi shamba msimu huu ila hili litakupa doa kubwa kuliko hata mnavyofikiri.

Mheshimiwa rais kula ndio kila kitu huko kwingine tutauvumilia ukiwa na njaa huwezi hata kukaa hapo kwenye kiti kusikiliza wananchi ukiwa na njaa safari za nje hutozitaman hata uraisi utauona mzigo.

Ndio maana hata maandiko na vitabu vya dini vinasema ukiwa na chakula na mavazi shukuru kwa hivyo vingine bwebwe.

Kama mimi muongo basi shinda njaa japo siku mbili.

Njaa ni ugonjwa ulio changamka.

Najua unakumbuka 2016
 
Sasa huyu si kila kitu kimepanda adi kipande cha sabuni we unaongelea mbolea tu😀😀😀😀 atakwambia "haya nimeskia na hilo tunalibeba" atachukua hatua Uviko-19 ikiisha😀😀😀😀
 
Mheshimiwa rais na maind bei ipo chini sana Junia la kilo 100 ni elfu 29

Je, tutanunua hiyo mbolea ya laki na 20
 
Sasa huyu si kila kitu kimepanda adi kipande cha sabuni we unaongelea mbolea tu[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] atakwambia "haya nimeskia na hilo tunalibeba" atachukua hatua uvico19 ikiisha[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Naongelea mbolea kwa kuwa kula ni lazima
 
Mzanzibari na kilimo wapi na wapi..huko ni uvuvi na kudemka tu ndicho wanajua..

#MaendeleoHayanaChama
 
Pole na hongera kwa kutimiza majukumu ya nchi

Mheshimiwa rais kilio chetu wakulima ni kile kile...
Kama mngekuwa na Bunge linalojali maisha ya wananchi hali isingefika hivi ilivyo.
 
Back
Top Bottom