Rais Samia hawezi kushinda urais 2025 kirahisi kama Wakurugenzi na Tume ya Uchaguzi watadhibitiwa

Pole kwako Sukuma gang member, kaa zako kwa kutulia kwani sidhani kama kushinda/kushindwa kwake kunakuhusu.
 
Sasa mbona mtu kama Jiwe alikuwa Rais?
 
Kwani wajua jinsia yake mpaka wamwita mama? Au hoja zimekuishia? Wasukuma bhana [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Stress hizo anatakiwa apewe dawa ya Mkuyati ili atibiwe.
 
BONGO LAND hakunaga uchaguzi wa fair ila atakaye pitishwa na kamati kuu ya chama flani ndiye atakaye kuwa rais ,na labda ni kuambie tu SSH akiamua kuwa rais 2025 -2035 hakuna wa wa kumzuia hata punje ,labda aamue yeye mwenyewe kuachia kwa busara zake.Ili tuweze kuwa na fair election jambo la msingi kuwe na tume huru ya uchaguzi,vyombo vya usalama viwe vina practice fairness,media zote ziwe zinatoa air time kwa vyama vyote in unbiased manner hasa tbc bila kufanyika haya tunadanganyana kabisa
 
Hizi ni stori za Sukuma gang na Chadomo kujifariji..

Hao wananchi wasiomkubali unawajua wewe peke yako?

Samia atashinda mchana kweupeee
 
We are going to write "The end of an era" Let us wait and see. Lowest income concerners are not well satisfied with the current situation.

CC. Joyce Banda
 
Nchi yangu TANZANIA imepitia wakati mgumu sana ktk siasa zake, Chama Dola pia kimegawanyika makundi makundi,bt yenye nguvu ni makubwa mawili.

KATIBA mpya ndio njia pekee ya kuondoa mpasuko huo ndani ya CHAMA. In other way naeza Sema CCM wanahitaji Katiba mpya kuliko hata vyama vya upinzani na makundi mengine.

Mwl Nyerere alikuwa na uwezo mkubwa wa kuona ya MBELENI kuliko viongozi wengi waliopo sasa.

Kuingia ktk Uchaguzi mamlaka ya Rais yakiwa pale pale Kwa mlango wa tume kuwa huru, wakati huo huo matokeo ya urais hayahojiwi mahakamani, na Rais hashtakiwi Kwa makosa yoyote aliyofanya akiwa madarakani ni tunajidanganya, yaani tuendelee kuitumbukiza Nchi SHIMONI bila kujali vizazi vijavyo.

Nawasihi Kwa la MUNGU Alie hai, msiwaze vyeo vya kisiasa pekee, Amani muionayo ilitengenezwa, zamani viongozi walichukia RUSHWA Kutoka moyoni, Msisubiri mabaya yatokee ndo mrekebishe, fanyeni sasa NCHI ISIANGAMIE. Amen
 
Kwa KATIBA iliyopo, Hata stiv Nyerere akisimamishwa na chama Dola, Mkt wa tume akishamtangaza, hayupo wa kupinga.

Msijidanganye, KATIBA mpya ni muhimu ipatikane kabla ya uchaguzi, ni kheri UCHAGUZI usogezwe mbele tupate Katiba mpya. Amen
 
Mawazo na uhalisia ni vitu viwili tofauti
 
Wananchi wa kawaida labda umaanishe hawa wanaoshinda JF wakiandika maoni yao, lakini hao wa huko chini watampigia kura tena nyingi sana.

Bajeti ya wizara ya kilimo imeongezwa zaidi ya asilimia sabini, kilimo kimeguswa moja kwa moja kwa maana ya pembejeo na ufufuaji wa mazao yaliyokuwa yakipuuzwa miaka ya nyuma. Hao wote ni wapiga kura na ni wengi sana kulinganisha na wapambe wanaoshinda humu jukwaani.
 
Dunia nzima hakuna nchi ambayo pesa inagawiwa mitaani. Huyu anapiga kelele akifurahisha nafsi yake.
 
Nipe mwaka ambao ccm imeshinda uchaguzi wa urais..kwa haki na usawa..

Ccm ilishakataliwa kitambo..walichobakiza ni ubabe mabavu..wizi wa kura na uchakachuaji kupitia tume ya hovyo..katiba ya hovyo..wakilindwa na policcm.

Hii nchi ccm imeitia unajisi kupitia viongozi wake wenye uchu wa madaraka.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio Samia tu hata jiwe asingeshinda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…