Interesting. Point ya maana sana hii. UKWELI ni kwamba hakuna haja ya uchaguzi mkuu 2025. Hakuna asiyejua yatakayokuwa matokeo tukiendelea na status quo. More of the same, beyond half a century of existence of the nation, is utter MADNESS.
Heri Samia apewe hadi 2030 kwa maelewano ya kitaifa kwamba kipindi chote hicho kitatumika kurekebisha katiba, sheria na mfumo mzima wa utawala wa nchi (Rais kuwa chini ya utawala wa sheria, Bunge huru, Mahakama huru, Tume ya uchaguzi huru, Taasisi huru za umma (autonomous), na namna ya usimamizi makini wa vyombo vya dola chini ya utawala wa kiraia.
Tukishindwa hilo ni bora tuendelee na maisha yetu kama yalivyo bila kupoteza muda na nguvu kwenye porojo za kisiasa.