Rais Samia ili ku-deal kisawasawa na watu hao, unda Tume ya kijaji kuchunguza mauaji ya MKIRU, kina Ben Saanane, Azory, kushambuliwa kwa Lissu

Mama kawa mpole sana mpaka mnamshika sharubu. Ila tatizo la Mama kaja kuwa kama vile yeye hakuwa sehemu ya Dkt Magufuli
 
Ali Hassan Mwinyi alitufanyia madudu akutengenezee gabacholi 90, huyu nae Kaanza kukusanya ndizi barabarani, huu muungano kama ni koti tuuvue tu
 
Akipuuza ushauri huu nitamshangaa sana !
 
Hizo silaha za Nyuklia zina wakati wake.... ila kwa sasa huo ujanja hana. Anahitaji kanda ya ziwa 2025, kina ngosha wakimgeuka atapata tabu sana. JK walimtesa sana 2010.
Siku hizi kura za kwenye box hazina thamani tena na upumbavu huu uliasisiwa na Magufuli,hivyo wingi wa kura zenu za kwenye box hazimtishi aliyepo madarakani. Wanaodai Katiba Mpya wameona mbali,kwa mfumo huu wa wizi wa kura na matumizi ya mabavu ya vyombo vya dola haiwezekani kumuondoa madarakani aliyepo madarakani. Sukuma Gang kubalini Saigon Club imewazidi kete.
 
Nafikiri kilichopo ni Magu gang na Sukuma gang ni kitu tu cha kufikirika.
You are right,hata magu mwenyewe hakuwa Msukuma,bali aliutumia Usukuma ili kupata uungwaji mkono kwa vile Wasukuma ndiyo kabila lenye idadi kubwa sana ya watu. Inafaa kuanzia sasa hili genge lijulikane ka magu gang. Mimi ni Msukuma lakini sijawahi kumkubali mwendazake.
 
Nimekumbushia tu uchaguzi wa 2010. Nguvu ya umma ilikuwa kubwa sana kanda ya ziwa. Masha na Diallo hawakuanguka bure, pressure ya wananchi ilikuwa kubwa sana; wakaona isiwe tabu. You never know.
 
Unadhani mama hajipendi? Anajua fika kuwa baadhi ya matukio yalifanywa na mbabe wake ili kumchafua Kubwa lao Magu.

Eti leo aunde timu ya uchunguzi, acha utani.
 
Hizo silaha za Nyuklia zina wakati wake.... ila kwa sasa huo ujanja hana. Anahitaji kanda ya ziwa 2025, kina ngosha wakimgeuka atapata tabu sana. JK walimtesa sana 2010.
Kwa tume ipi? Ya Mahera?
 
Mbona wakulima na wafugaji wote ni SG au hujui wewe.Unapoteza muda.Piga kazi yote yatakaa sawa.Imba Hapa KAZI TU
Labda wakulima wa dengu, lakini siyo wakulima wa mahindi, korosho, mbaazi, kahawa, wala matunda kama parachichi.
 
Mama kawa mpole sana mpaka mnamshika sharubu. Ila tatizo la Mama kaja kuwa kama vile yeye hakuwa sehemu ya Dkt Magufuli
Wanasema ajali ya kizembe ya basi lawama zote kwa dereva, siyo utingo.
 
Wakwe zangu ni wasukumu, sijawahi kuona mwanafamilia yeyote akimshabikia.

Wapambe wake usukumani ni wa kuhesabu kama mikoa mingine.

Hakuwa msukuma bali mhamiaji toka Kigoma. Baba yake aliweka makazi kule Sengerema, karibu na maeneo ya Nzera; na huko pia wazazi wake walihamia tokea Burundi.

Baada ya kifo cha baba yake, kutokana na kuchukiwa na wenyeji, walihamia Biharamulo. Kule mama akapata baba wa kambo, msubi. Hawa kazi yao kubwa ni uwindaji. Akiwa bado mdogo, akaambatana na mamaye kwenda maeneo ya Chato kwa sababu baba wa kambo alikuwa akifanyia shughuli zake za uwindaji kwenye msitu wa Burigi.
 
Aliyekwambia Rais na Mbunge wa Tanzania anategemea hizo takataka za makaratasi zinazoitwa kura ni nani??

Jidanganye.

Katiba Mpya na Tume huru ndio Uchumi wetu.
Kwahiyo huwa wanapoteza bure pesa za kufanyia kampeni?
 
Wasukuma hii aliyoleta BAMS naona ni kweli na muitumie hii kuelewa kuwa watanzania hawawachukii wasukuma ila tunawaita SUKUMAGANG hao wahamiaji Toka Burundi waliovaa ngozi ya kabila la wasukuma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…