Rais Samia ingilia kati, TRA watatukwamisha

Rais Samia ingilia kati, TRA watatukwamisha

Rais wangu, ukipata nafasi mwite ofsini Kamishna wa TRA nchini, Bwana Alphayo Kidata. Muulize katika mwezi April/May ambao yeye amekua ofisini amekusanya mapato kiasi gani. Akikupa hesabu linganisha na mwezi wowote katika mwaka wowote unaoutaka wewe. Achana na miaka ya JPM ambayo inasemwa kodi zilikusanywa kwa nguvu. Tumia mwezi wowote katika kipindi cha awamu ya nne kwa makadilio. Ukipata majibu, mpe nafasi ya mwisho Alphayo Kidata, aache kukuchezea!!

Rais wangu, TRA ya Tanzania haikusanyi kodi tena. Wanafika ofsini kwa muda, wanakaa kidogo katika meza zao zilizopangwa shaghalabaghala, wengine wanawasha kompyuta wengine hawawashi. Baada ya muda mfupi, wanakusanyana nusu yao wanaondoka. Wao wanasema wanakwenda kufanya kazi za nje. Ndugu Rais, TRA ya Tanzania inafanya kazi za nje kwa ajili ya kazi za ndani zisizokuwepo.

Rais wangu, wakati wote huu wote waliobaki ofsini, hawana cha kufanya. Waranda-randa ofsini na kupiga miayo na soga. Wengine wanasimulia habari za msiba wa JPM. Hakuna lolote linalofanyika kwa sababu hakuna mtandao. TRA hawakusanyi pesa kwa sababu ya mtandao, nchi haikusanyi mapato kwa sababu ya mtandao. Tatizo la mtandao wa TRA limekua sugu katika nchi yetu, linajirudia leo, kesho na keshokutwa. No one cares!! Mtu mmoja ameniambia kuwa jana (May, 26) TRA nchi nzima haikufanya kazi. Yaani kwamba, kwa siku nzima nchi yote haikukusanya mapato kupitia chombo chake kikuu cha makusanyo. Kama taarifa hii ni ya kweli basi tatizo ni kubwa. Nchi hii siku hizi haikusanyi pesa, halafu inatumia pesa zilizokusanywa na wengine. Wenye hofu wanasema zikiisha zilizokusanywa nchi inaweza kuanguka.

Rais wangu, nenda leo TRA Mwenge, TRA Tegeta na TRA Kimara (zote za Da'slama), kwa kuzitaja chache. Ukikuta zote zinafanya kazi na inaonesha zimefanya kazi yake ipasavyo kwa siku tatu nyuma au na zaidi, niwajibishe mimi kwa namna utakayoona inafaa. Tuna tatizo kubwa, katika nchi kubwa namna hii kushindwa kukudanya mapato kwa sababu ya mtandao ni aibu. Huu utaratibu usipoangaliwa, nchi itatufia mikononi. Nchi isiyokuwa na mapato yake haiwezi kulipa mishahara kwa wakati, haiwezi kununua dawa za hospitali, hakwezi kugharamia elimu bila malipo na haitoweza kukamilisha miradi ya maendeleo ya gharama kubwa. Tukiruhusu nchi ifike hapo, ndio tumekwenda na maji tayari.

Rais wangu, juzi mtandao wa Tanesco ulisumbua kidogo katika kununua LUKU. Licha ya taarifa iliyotolewa mapema na Tanesco ya kuomba radhi lakini nchi nzima ilisimama. Waziri wa Nishati akahamaki, akafukuza watu hovyo, Waziri Mkuu akasimama kutoa maelekezo. Baada ya muda mfupi, umeme ukarudi. Tanesco haikusanyi mapato kama TRA lakini tuliwekeza nguvu kubwa usiku na mchana. Mtandao wa TRA hauna uhakika kwa zaidi ya mwezi, unasumbua kila siku lakini hakuna anayejali, Waziri wa fedha hajulikani alipo wala hajali.

Rais wangu, ni kama wote tumeridhika na hali hii. Pesa hazikusanywi kwa wakati kwa sababu ya mtandao, watu wanakwenda TRA na kurudi kila siku halafu muda wa kulipa ukipita mfanyabiashara anatozwa faini (penalty) kwa kuchelewa kulipa kodi. Hivi ndivyo tunavyohuisha bishara na kuvutia wawekezaji katika nchi yetu. Mtu kwenda TRA kulipa kodi moja kila siku ni kero, tunaharibu ratiba za watu bila sabbau. Wanaomkumbuka Magufuli wanamkumbuka kwa mengi, sisi tuendelee kufanya kazi za nje tukirudi ndani nchi itakua hoi bin taaban. Rais wangu, TRA watakukwamisha ukiweza chukua hatua sasa

MenukaJr,
Da'slama-Tanzania.
Maybe ni strategy ya kuleta hela mtaani, si watu wanalilia mzunguko wa pesa mtaani? Ngoja raia wafuje ili zije mtaani.
 
Waliambiwa wakajadiliane na walipa kodi.

Ninadhani ndio hizo kazi za nje.

Wanawabembeleza walipa kodi..mambo yatakaa vizuri muda sii mrefu. Usihofu.
Lack of professionalism. Tumieni nguvu basi kama mtapata kodi...kwa mantiki hii, TRA inahitaji kusukwa upya. Iwe na watu wanaojitambua na wanatambua wajibu wao. TRA sio jeshi. Ni taasisi yenye waajibu wa kukusanya kodi na kuwalinda walipa kodi ili kodi iwe endelevu. TRA ya sasa inataka kukusanya kodi bila kujua wana wajibu wa kuwalinda walipa kodi kwa kudai kodi halali.
 
Hakuna Urafiki wa watoza kodi na wafanyabiashara dunia nzima (nature of Tax incidence)
Mkuu naomba usiweke mawazo ya jumla. Wanaofanya kuwe na uadui kati ya watoza kodi na wafanyabiashara ni watoza kodi wenyewe. Yaani kuanzia kwenye kukadiriwa utahojiwa kama uko kwenye Kituo cha Polisi. Ukiwaomba mfike kwenye eneo la biashara yako hawataki ni full kukadiria wapendavyo. Njoo sasa wakati wa kulipa makadirio waliyofanya, utakuta hata mtoa controll number anakuuliza "mbona umekadiriwa kidogo hivyo, kwanini". Halafu hiyo controll number kuipata unaisotea ni balaa. Sasa hapo unategemea nini?
 
Rais wangu, ukipata nafasi mwite ofsini Kamishna wa TRA nchini, Bwana Alphayo Kidata. Muulize katika mwezi April/May ambao yeye amekua ofisini amekusanya mapato kiasi gani. Akikupa hesabu linganisha na mwezi wowote katika mwaka wowote unaoutaka wewe. Achana na miaka ya JPM ambayo inasemwa kodi zilikusanywa kwa nguvu. Tumia mwezi wowote katika kipindi cha awamu ya nne kwa makadilio. Ukipata majibu, mpe nafasi ya mwisho Alphayo Kidata, aache kukuchezea!!

Rais wangu, TRA ya Tanzania haikusanyi kodi tena. Wanafika ofsini kwa muda, wanakaa kidogo katika meza zao zilizopangwa shaghalabaghala, wengine wanawasha kompyuta wengine hawawashi. Baada ya muda mfupi, wanakusanyana nusu yao wanaondoka. Wao wanasema wanakwenda kufanya kazi za nje. Ndugu Rais, TRA ya Tanzania inafanya kazi za nje kwa ajili ya kazi za ndani zisizokuwepo.

Rais wangu, wakati wote huu wote waliobaki ofsini, hawana cha kufanya. Waranda-randa ofsini na kupiga miayo na soga. Wengine wanasimulia habari za msiba wa JPM. Hakuna lolote linalofanyika kwa sababu hakuna mtandao. TRA hawakusanyi pesa kwa sababu ya mtandao, nchi haikusanyi mapato kwa sababu ya mtandao. Tatizo la mtandao wa TRA limekua sugu katika nchi yetu, linajirudia leo, kesho na keshokutwa. No one cares!! Mtu mmoja ameniambia kuwa jana (May, 26) TRA nchi nzima haikufanya kazi. Yaani kwamba, kwa siku nzima nchi yote haikukusanya mapato kupitia chombo chake kikuu cha makusanyo. Kama taarifa hii ni ya kweli basi tatizo ni kubwa. Nchi hii siku hizi haikusanyi pesa, halafu inatumia pesa zilizokusanywa na wengine. Wenye hofu wanasema zikiisha zilizokusanywa nchi inaweza kuanguka.

Rais wangu, nenda leo TRA Mwenge, TRA Tegeta na TRA Kimara (zote za Da'slama), kwa kuzitaja chache. Ukikuta zote zinafanya kazi na inaonesha zimefanya kazi yake ipasavyo kwa siku tatu nyuma au na zaidi, niwajibishe mimi kwa namna utakayoona inafaa. Tuna tatizo kubwa, katika nchi kubwa namna hii kushindwa kukudanya mapato kwa sababu ya mtandao ni aibu. Huu utaratibu usipoangaliwa, nchi itatufia mikononi. Nchi isiyokuwa na mapato yake haiwezi kulipa mishahara kwa wakati, haiwezi kununua dawa za hospitali, hakwezi kugharamia elimu bila malipo na haitoweza kukamilisha miradi ya maendeleo ya gharama kubwa. Tukiruhusu nchi ifike hapo, ndio tumekwenda na maji tayari.

Rais wangu, juzi mtandao wa Tanesco ulisumbua kidogo katika kununua LUKU. Licha ya taarifa iliyotolewa mapema na Tanesco ya kuomba radhi lakini nchi nzima ilisimama. Waziri wa Nishati akahamaki, akafukuza watu hovyo, Waziri Mkuu akasimama kutoa maelekezo. Baada ya muda mfupi, umeme ukarudi. Tanesco haikusanyi mapato kama TRA lakini tuliwekeza nguvu kubwa usiku na mchana. Mtandao wa TRA hauna uhakika kwa zaidi ya mwezi, unasumbua kila siku lakini hakuna anayejali, Waziri wa fedha hajulikani alipo wala hajali.

Rais wangu, ni kama wote tumeridhika na hali hii. Pesa hazikusanywi kwa wakati kwa sababu ya mtandao, watu wanakwenda TRA na kurudi kila siku halafu muda wa kulipa ukipita mfanyabiashara anatozwa faini (penalty) kwa kuchelewa kulipa kodi. Hivi ndivyo tunavyohuisha bishara na kuvutia wawekezaji katika nchi yetu. Mtu kwenda TRA kulipa kodi moja kila siku ni kero, tunaharibu ratiba za watu bila sabbau. Wanaomkumbuka Magufuli wanamkumbuka kwa mengi, sisi tuendelee kufanya kazi za nje tukirudi ndani nchi itakua hoi bin taaban. Rais wangu, TRA watakukwamisha ukiweza chukua hatua sasa

MenukaJr,
Da'slama-Tanzania.
nitakuunga mkono ukinionesha uthibitisho wa kuwa wewe ni mlipa kodi ya moja kwa moja. Weka payments zako za kodi kwa quarter ya kwanza ya mwaka tuone ulivyocomply kabla ya kuja na kulalamika.
 
Mkuu naomba usiweke mawazo ya jumla. Wanaofanya kuwe na uadui kati ya watoza kodi na wafanyabiashara ni watoza kodi wenyewe. Yaani kuanzia kwenye kukadiriwa utahojiwa kama uko kwenye Kituo cha Polisi. Ukiwaomba mfike kwenye eneo la biashara yako hawataki ni full kukadiria wapendavyo. Njoo sasa wakati wa kulipa makadirio waliyofanya, utakuta hata mtoa controll number anakuuliza "mbona umekadiriwa kidogo hivyo, kwanini". Halafu hiyo controll number kuipata unaisotea ni balaa. Sasa hapo unategemea nini?
Hebu mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, kweli unawezaje kukubali tu ubambikiwe.Mimi wjaribu maana natunza rekodi zangu zote za mauzo ,manunuzi na matumizi ya biashara.Hapa najua ndiyo dawa kutunza kumbukumbu tu maana hata bodi au mahakama ya rufaa ya kodi ntafika.
 
Rais wangu, ukipata nafasi mwite ofsini Kamishna wa TRA nchini, Bwana Alphayo Kidata. Muulize katika mwezi April/May ambao yeye amekua ofisini amekusanya mapato kiasi gani. Akikupa hesabu linganisha na mwezi wowote katika mwaka wowote unaoutaka wewe. Achana na miaka ya JPM ambayo inasemwa kodi zilikusanywa kwa nguvu. Tumia mwezi wowote katika kipindi cha awamu ya nne kwa makadilio. Ukipata majibu, mpe nafasi ya mwisho Alphayo Kidata, aache kukuchezea!!

Rais wangu, TRA ya Tanzania haikusanyi kodi tena. Wanafika ofsini kwa muda, wanakaa kidogo katika meza zao zilizopangwa shaghalabaghala, wengine wanawasha kompyuta wengine hawawashi. Baada ya muda mfupi, wanakusanyana nusu yao wanaondoka. Wao wanasema wanakwenda kufanya kazi za nje. Ndugu Rais, TRA ya Tanzania inafanya kazi za nje kwa ajili ya kazi za ndani zisizokuwepo.

Rais wangu, wakati wote huu wote waliobaki ofsini, hawana cha kufanya. Waranda-randa ofsini na kupiga miayo na soga. Wengine wanasimulia habari za msiba wa JPM. Hakuna lolote linalofanyika kwa sababu hakuna mtandao. TRA hawakusanyi pesa kwa sababu ya mtandao, nchi haikusanyi mapato kwa sababu ya mtandao. Tatizo la mtandao wa TRA limekua sugu katika nchi yetu, linajirudia leo, kesho na keshokutwa. No one cares!! Mtu mmoja ameniambia kuwa jana (May, 26) TRA nchi nzima haikufanya kazi. Yaani kwamba, kwa siku nzima nchi yote haikukusanya mapato kupitia chombo chake kikuu cha makusanyo. Kama taarifa hii ni ya kweli basi tatizo ni kubwa. Nchi hii siku hizi haikusanyi pesa, halafu inatumia pesa zilizokusanywa na wengine. Wenye hofu wanasema zikiisha zilizokusanywa nchi inaweza kuanguka.

Rais wangu, nenda leo TRA Mwenge, TRA Tegeta na TRA Kimara (zote za Da'slama), kwa kuzitaja chache. Ukikuta zote zinafanya kazi na inaonesha zimefanya kazi yake ipasavyo kwa siku tatu nyuma au na zaidi, niwajibishe mimi kwa namna utakayoona inafaa. Tuna tatizo kubwa, katika nchi kubwa namna hii kushindwa kukudanya mapato kwa sababu ya mtandao ni aibu. Huu utaratibu usipoangaliwa, nchi itatufia mikononi. Nchi isiyokuwa na mapato yake haiwezi kulipa mishahara kwa wakati, haiwezi kununua dawa za hospitali, hakwezi kugharamia elimu bila malipo na haitoweza kukamilisha miradi ya maendeleo ya gharama kubwa. Tukiruhusu nchi ifike hapo, ndio tumekwenda na maji tayari.

Rais wangu, juzi mtandao wa Tanesco ulisumbua kidogo katika kununua LUKU. Licha ya taarifa iliyotolewa mapema na Tanesco ya kuomba radhi lakini nchi nzima ilisimama. Waziri wa Nishati akahamaki, akafukuza watu hovyo, Waziri Mkuu akasimama kutoa maelekezo. Baada ya muda mfupi, umeme ukarudi. Tanesco haikusanyi mapato kama TRA lakini tuliwekeza nguvu kubwa usiku na mchana. Mtandao wa TRA hauna uhakika kwa zaidi ya mwezi, unasumbua kila siku lakini hakuna anayejali, Waziri wa fedha hajulikani alipo wala hajali.

Rais wangu, ni kama wote tumeridhika na hali hii. Pesa hazikusanywi kwa wakati kwa sababu ya mtandao, watu wanakwenda TRA na kurudi kila siku halafu muda wa kulipa ukipita mfanyabiashara anatozwa faini (penalty) kwa kuchelewa kulipa kodi. Hivi ndivyo tunavyohuisha bishara na kuvutia wawekezaji katika nchi yetu. Mtu kwenda TRA kulipa kodi moja kila siku ni kero, tunaharibu ratiba za watu bila sabbau. Wanaomkumbuka Magufuli wanamkumbuka kwa mengi, sisi tuendelee kufanya kazi za nje tukirudi ndani nchi itakua hoi bin taaban. Rais wangu, TRA watakukwamisha ukiweza chukua hatua sasa

MenukaJr,
Da'slama-Tanzania.

=====
UPDATES:
=====

TRA Wamekanusha habari za Mtandao kusumbua. Wamesema hii ni taarifa ya Uongo na Uzushi. Kwani imelenga kupotosha na kuleta taharudi miongoni mwa Walipa Kodi pamoja na kuidhalilisha taasisi na Watumishi wake.

Katika kipindi cha mwezi mzima, TRA haikuwa na Hitilafu yoyote.

TRA imewataka Waipa Kodi kuendelea kulipa kodi.
View attachment 1800203
Bora wametoa hii TRA maana walitaka msingizia baba wa watu bure. Yaani kuna vitu vingine unaona ni wivu tu au utakuta huyu mkuu wao tra ni msimamizi mzuri katika makusanyo.
 
Form six mna akili ndogo sana. Kwani hilo tatizo analo zungumzia mtoa mada linamuongelea babu yako, au linazungumzia TRA? Unafahamu maana ya OP wewe?
Umejibu kwa ghalabu. Dalili ya kuonyesha nilichosema kimekuingia panapo stahili na umepata ujumbe sahihi.
 
Samia ana marafiki gani ishu ya kodi na makusanyo yake kazingua sana na itamzingua mwenyewe. Mtake msitake kazingua kodi ndio uhai na heshima ya serikali. Mkisifia sifia ila ukweli kuhusu kodi ni kituko.
Mkuu 'Galileo_Gaucho' ni vizuri wakati mwingine kumsoma mtu na kuelewa kilichoandikwa.

Sikueleza chochote hapo juu kuonyesha kuwa kodi sio muhimu kwa nchi yoyote duniani; na wala sijamsifia lolote juu ya marafiki zake wafanya biashara.
Kama lisemwalo ni kweli, basi sote, mimi nawe tusubiri kuyaona matokeo. Maana haya hayajifichi.
 
Sasa majungu yako wapi hapo! Mimi nimetoa tu maoni yangu na tena nimeshauri! Au umeona nimemtaja mtu, zaidi ya kuitaja hiyo Taasisi? Uwe una akili hata kidogo basi.
Unawalalamikia TRA kwamba wanafanya makadirio unapotaka kuanza biashara bila kufika site. Nimehoji wafike kwenye biashara ipi wakati ndio umewafuata ili wakukadirie? Hayo kama sio majungu ni nini kumbe?
 
Unawalalamikia TRA kwamba wanafanya makadirio unapotaka kuanza biashara bila kufika site. Nimehoji wafike kwenye biashara ipi wakati ndio umewafuata ili wakukadirie? Hayo kama sio majungu ni nini kumbe?
Usikute nabishana na mtu ambaye hajui hata TIN ni kitu gani. Katika hali ya kawaida unawezaje kulipia mapato pasipo na biashara?

Na unapoenda kulipia, ndiyo wanakukadiria kodi pasipo kufika kwenye eneo ilipo biashara! Sasa wewe unaongea kama umekunywa pombe za kienyeji! Unanichosha tu hapa. Eti majungu! Yaani niionee majungu TRA!
 
Umejibu kwa ghalabu. Dalili ya kuonyesha nilichosema kimekuingia panapo stahili na umepata ujumbe sahihi.
Nimekupa jibu lililo endana na ulicho kiandika. Mada ilihusu ina mahusiano na TRA! Hivyo sikuwa OP kama ulivyochulia wewe. Wewe ndiyo umekurupuka.
 
Usikute nabishana na mtu ambaye hajui hata TIN ni kitu gani. Katika hali ya kawaida unawezaje kulipia mapato pasipo na biashara? Unaanzisha biashara, ndiyo unaenda TRA kulipia leseni.

Na unapoenda kulipia, ndiyo wanakukadiria kodi pasipo kufika kwenye eneo ilipo biashara! Sasa wewe unaongea kama umekunywa pombe za kienyeji! Unanichosha tu hapa. Eti majungu! Yaani niionee majungu TRA!

TRA wanatoa leseni za biashara..?
 
Back
Top Bottom