Rais Samia Kiwanda cha Chibuku/ Darbrew LTD kilifungwa tangu mwaka 2018. Muwekezaji yupo lakini Watendaji wa Jiji la Ilala wanakwamisha

Ushahidi upo mkuu tena ni watertight,na taarifa zipo hadi TAKUKURU na uenda huyu mkurugenzi mpya wa TAKUKURU zitamfikia soon
L
Ushahidi upo mkuu tena ni watertight,na taarifa zipo hadi TAKUKURU na uenda huyu mkurugenzi mpya wa TAKUKURU zitamfikia soon
Tatizo ubaridi mkuu.............labda naye ameingiwa na ubaridi
 
Mama Ni ustaadhat .

Pombe Ni haramu kwake .

Subirini atoke .

By the way chibuku Ni pombe tamu Sana[emoji1]
 
Pombe haramu ya kibuku is no more.🤣🤣
 
Umeandika vizuri sana na poleni sana waathirika wa moja kwa moja wa hujuma hizi. Binafsi nimeshaingilia kati hujuma kama hii hivi karibuni na nilifanikiwa kupata suluhu chanya kwa mwekezaji na taifa. Ninachoweza kusema kwa ujumla ni kwamba viongozi wengi watendaji kwenye sekta ni wasomi wa darasani bila uzoefu kwa hiyo ukiwapelekea tatizo wanakuwa ama hawaelewi cha kufanya au wanakuwa waoga kwa kujua hawana uwezo wa kutetea hoja. Kuhusu suala langu, waliniambia wanaacha sheria ifuate mkondo wake lakini sheria yenyewe inawataja kuwa wao ndiyo watekekezaji wa sheria hiyo! Nilipowaambia sikubali ndipo walipokusanya akili na kutoa uamuzi!
 
1. Iacheni pombe ya chibuku ife kifo chema wala msilazimishe wananchi waendelee kunywa pombe ya kienyeji.

2. Chibuku ililenga nchi au jamii maskini tu nadhani Tanzania, Botswana, Zambia, Zimbabwe na Malawi ndiyo kuna kampuni kubwa za kutengeneza pombe ya nafaka

3. Mozambique, Uganda na Tanzania wote wameacha kutengeneza. Soko limepungua kwa sababu watu wenye kipato wanakuwa conscious na afya zao hivyo kunywa kwa plastic inakuwa shida

4. Ukiweka kwenye tetra pack lazima upandishe Bei. Ukipansisha unaanza kupoteza wateja dhidi ya pombe za mnazi, kimpumu, mbege na komoni.

5. Hata CEO wa Chibuku na Salesperson wao ikifika jioni wanakunywa Serengeti na Castle Lite. Hii Chibuku ni alama ya umaskini.

Acheni tu Serikali iangalie namna ya kutumia lile eneo pale Ubungo kuliko kugombea kuendelea kupika pombe ya kienyeji kwenye Karne ya 21 wakati nchi iko uchumi wa lower middle
 
Haya mapombe yanafaa kunywewa na bata tu, nashangaa binadamu bado wanang'ang'ania kunywa uchafu.

Miaka 5 sasa kiwanda kimefungwa , je mumepungukiwa nini bila kuwa na chibuku?
 
Haya mapombe yanafaa kunywewa na bata tu, nashangaa binadamu bado wanang'ang'ania kunywa uchafu.

Miaka 5 sasa kiwanda kimefungwa , je mumepungukiwa nini bila kuwa na chibuku?
Nafaka ni uchafu? Kwahiyo Kvant na visungura ndio pombe za maana?
 
Nafaka ni uchafu? Kwahiyo Kvant na visungura ndio pombe za maana?
nilikuwa namfahamu Marketing Manager na CEO wa Chibuku miaka ya 2006-10, sikuwahi kuwakuta wakinywa hiyo uchafu. Tukikutana weekend wankunywa Safari au Kilimanjaro
 
nilikuwa namfahamu Marketing Manager na CEO wa Chibuku miaka ya 2006-10, sikuwahi kuwakuta wakinywa hiyo uchafu. Tukikutana weekend wankunywa Safari au Kilimanjaro
Kwahiyo mfanyakazi wa TBL akinywa Heineken maana yake bia za TBL ni chafu?
 
Wazalendo bado wapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…