Rais Samia: Kodi ndio Damu ya Serikali

Rais Samia: Kodi ndio Damu ya Serikali

Kwa hii Serikali ya sasa, utekaji na mauaji ya wakosoaji, ndiyo damu ya Serikali.
 
Watanzania wanalipa kodi wakibananishwa, kwa sababu wanaona dhahiri serikali haipo kwaajili ya ustawi wao. Kodi yao inafisadiwa, na hakuna anayeadhibiwa. Kodi yao inatumika kuwalipa watekaji na wauaji, huku serikali ikidai haina hela za kuwaajiri madaktari, wauguzi na walimu. Kodi yao inatumika hovyo kununua magoli na kuwalipa wasanii machawa, huku walipa kodi wakiogelea kwenye umaskini na huduma duni.

Watanzania wataendelea kulipa kodi kwa kubananishwa, ni pale ambapo hakuna namna ya kukwepa, mpaka siku ambayo watawala watakapoelewa kuwa kodi ni pesa ya wananchi, siyo ya Rais Samia au waziri Mwigulu, na hivyo inatakiwa kuheshimiwa na kuthaminiwa; siyo kama ilivyo sasa ambapo kodi ya watanzania inaonekana ni pesa isiyo na mwenyewe!!
 
Sasa huwa inashangaza unakuta mfanyabiashara au mtu ni mkwepa kodi mkubwa lakini huyo huyo analalamika juu ya ubovu wa huduma fulani ya serikali.bila kujua kuwa serikali haina pesa ila wananchi ndio wenye pesa na tunaopaswa kuchanga kupitia mfumo wa kodi ili serikali ilete na kusambaza huduma kwa
Uchawa uliopitiliza huleta kichaa unashangaa wafanyabiashara kutolipa kodi mbona hushangai Raisi kutolipa kodi kwenye mapato yake? Mnafiki mkubwa wewe

Yeye damu yake kwenye kodi iko wapi kama kodi ndio damu ya serikali?
Alipe kofi asihubiri kitu ambacho yeye hafanyi abahimiza watu kulipa kodi wakati yeye halipi kodi

Vipi chawa unasemaje kuhusu hilo la Raisi kutolipa kodi kwenye mapato yake halafu anasukumizia watanzania wengine kuwa wawe na moyo wa kulipa kodi
 
Serikali na kodi... Mfumo wa wazi wa wizi na unyonyoji!
images (29).jpeg
images (28).jpeg
download (5).jpeg
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan kwa uchungu,hisia kali na msisitizo mkali sana.amesema ya kuwa Kodi ndio Damu ya serikali.ambapo kila Mtanzania anapaswa kulipa kodi.

Hii maana yake nini watanzania wenzangu? Hii ni katika kuwakumbusha watanzania wajibu wao au wetu sote katika ujenzi wa Taifa letu. Maana yake ni kuwa watanzania ni lazima tujisikie fahari kulipa kodi kwa hiyari ya mioyo yetu.tukitaka maendeleo ya aina yoyote ile ni lazima tuwajibike kulipa kodi bila kutafuta chochoro za kukwepa kodi.

Ni ulipaji wa kodi stahiki utafanya serikali yetu kuwa na uwezo wa kujenga zahanati na vituo vya afya vya kutosha.kuajiri watumishi wa afya wa kutosha na katika ngazi zote,kununua vifaa tiba na madawa ya kutosha na ya kila ugonjwa. Kujenga na kuboresha ama kukarabati shule ,kuongeza vyumba vya madarasa ili kuendana na ongezeko la wanafunzi,kuajiri walimu wa masomo yote pamoja na kuwa na maabara za kisasa kwa masomo yote ya sayansi.

Ni ulipaji kodi stahiki utakao iwezesha serikali yetu kuwa na uwezo wa kujenga miundombinu ya barabara, usambazaji wa maji safi na salama,upandishaji wa mishahara kwa watumishi wa umma ili kuwaongezea morali ya kazi na kumudu gharama za Maisha,ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo pia itatoa fursa mbalimbali za ajira kwa vijana pamoja na kuchochea mzunguko wa fedha mitaani na biashara kushamiri.

Sasa huwa inashangaza unakuta mfanyabiashara au mtu ni mkwepa kodi mkubwa lakini huyo huyo analalamika juu ya ubovu wa huduma fulani ya serikali.bila kujua kuwa serikali haina pesa ila wananchi ndio wenye pesa na tunaopaswa kuchanga kupitia mfumo wa kodi ili serikali ilete na kusambaza huduma kwa wananchi.

Kwa hiyo ni wajibu wetu wananchi kumuunga mkono Rais wetu kwa kulipa kodi bila kukwepa.hata Mataifa yaliyoendelea yamefika hapo yalipo kutokana na ulipaji wa kodi.Nchi za wenzetu ni wakali na wachungu sana linapokuja suala la ulipaji kodi.na ni kosa kubwa sana ikibainika wewe ni mkwepa kodi au umewahi kukwepa kulipa kodi mwaka fulani katika biashara fulani au kitu fulani.

Ndio maana ni kawaida sana kuona wachezaji wakubwa wenye majina makubwa ulaya wakiburuzwa mahakamani bila kujali ukubwa na umaarufu wa majina yao kwa makosa ya ukwepaji kodi.wenzetu walishajuwa kuwa kodi ndio moyo na kitovu cha maendeleo ya Nchi na ni Damu iendeshayo serikali kama alivyosema Mama yetu Mpendwa Daktari Samia Suluhu Hasssan.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Pia soma:Rais Samia: Uchumi wetu unakua lakini tunachokusanya, kingi kinaingia mifukoni kwa Watu

Mmmmhhhh mbona kila siku wanasema hela ni yako ni ni wewe unatoa na kufanya sasa hii kodi yetu unaitakia kwa kazi gani????[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
 
Uchawa uliopitiliza huleta kichaa unashangaa wafanyabiashara kutolipa kodi mbona hushangai Raisi kutolipa kodi kwenye mapato yake? Mnafiki mkubwa wewe

Yeye damu yake kwenye kodi iko wapi kama kodi ndio damu ya serikali?
Alipe kofi asihubiri kitu ambacho yeye hafanyi abahimiza watu kulipa kodi wakati yeye halipi kodi

Vipi chawa unasemaje kuhusu hilo la Raisi kutolipa kodi kwenye mapato yake halafu anasukumizia watanzania wengine kuwa wawe na moyo wa kulipa kodi

Sijui inaweza ikawaje iwapo wote tutaiga na kutekeleza mfano wa boss wetu pamoja na wabunge wetu wa kutolipa kodi
 
Wewe kiongozi mkuu hulipi kodi kila kitu bure halafu na una pato la kufuru,unahamasisha watu waliona na kipato Duni ndio walipe kodi.hii sijaielewa kabisaa
Yaani wanasiasa pamoja na mishahara mikubwa na marupurupu manono eti wao hawalipi kodi. Hata tozo za miamala ya simu nasikia haziwagusi baadhi yao kama si wote. Mimi Mwl wa 700K kwa mwezi najikuta takribani 200K imefyekwa na serikali ikiwa ni kodi na makato kibao. Nchi ngumu sana hii.
 
Back
Top Bottom