Rais Samia kuanza safari ya kikazi nchini DR Congo

Rais Samia kuanza safari ya kikazi nchini DR Congo

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Wakuu Kazi Iendeleee.

Taarifa zilizopo ni kwamba Rais Samia ana ziara ya kikazi nchini Congo.

Ataanza ziara hiyo wakati atakapotoka Zambia kwenye inauguration ya Hakainde Hichilema.

Akifika Congo atapokekewa na Mwenyeji Wake Rais Felix Tshisekedi.

Hakika Ziara zimeanza na Zimetaradadi
 
Kama mshauri wake ni vasco da gama unategemea nini?

Halafu nchi anazosafiri kwenda zina mchango mdogo kwenye uchumi wetu.

Asafiri kutafta wawekezaji wa maana huko Ulaya walete mitaji kutusaidia ku exploit hizi natural resources tulizonazo.

Sio muda utasikia ana ziara Somalia.

Yaani hapa tumeingia cha kike kweli.
 
Kama mshauri wake ni vasco da gama unategemea nini?

Halafu nchi anazosafiri kwenda zina mchango mdogo kwenye uchumi wetu.

Asafiri kutafta wawekezaji wa maana huko ulaya walete mitaji kutusaidia ku exploit hizi natural resources tulizonazo.

Sio muda utasikia ana ziara Somalia.

Yaani hapa tumeingia cha kike kweli.
Burundi ina mchango mdogo wa uchumi kwetu?

Kenya na Rwanda zina mchango mdogo kwa uchumi wetu?

Hivi yale magari 3000 yaliyopokelewa bandarini YANAPEKEKWA "huko Ulaya usemako"?

Ulaya waje kuwekeza kitu gani?!

Kwa hiyo "REGIONAL ECONOMY" kwako ni kupoteza muda? 😲😲

#NchiKwanza
#KaziIendelee
#SiempreJMT
 
Zanzibar-ASP
Mfano wako wala hauakisi mada tajwa.

Unalinganisha mambo ya wapika biriani jikoni kwako na ya AMIRI JESHI WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA Khaaa 😲😲?!!

You are not serious.

#KaziIendelee
#NchiKwanza
 
Wakuu Kazi Iendeleee.

Taarifa Zilizopo Ni Kwamba Rais Samia Ana Ziara Ya Kikazi Nchini Congo.

Ataanza Ziara Hyo Wakati atakapotoka Zambia Kwenye Inauguration ya HH.

Akifika Congo atapokekewa na Mwenyeji Wake Rais Felix Tshisekedi.

Hakika Ziara zimeanza na Zimetaradadi
Wanamkimbizakimbiza ili wapige kiulaini sana
 
Wakuu Kazi Iendeleee.

Taarifa Zilizopo Ni Kwamba Rais Samia Ana Ziara Ya Kikazi Nchini Congo.

Ataanza Ziara Hyo Wakati atakapotoka Zambia Kwenye Inauguration ya HH.

Akifika Congo atapokekewa na Mwenyeji Wake Rais Felix Tshisekedi.

Hakika Ziara zimeanza na Zimetaradadi
Hii ziara inaweza kuwa ya kimkakati na ya muhimu pengine kuliko ziara zote zilizofanyika toka mama aingie ikulu. Ni jambo la wazi kuwa katika nchi zote za maziwa makuu, DRC imejaaliwa kuwa na idadi kubwa ya watu takriban watu 120,000,000.

Itakumbukwa kuwa Tanzania tumejaaliwa kuwa na bandari, ambapo miongoni mwa nchi zinazotumia bandari yetu ni DRC.

Tanzania imekuwa ujenzi mkubwa wa reli ya mwendokasi ambayo inategemewa kuwa msaada mkubwa wa usafirishaji wa watu na mizigo kuelekea nchi za Rwanda, Burundi na DRC. Kimkakati, kama ujenzi huo utakamilika, Tanzania itakuwa imalamba dume kwa sababu tutaweza kujiinua kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji pamoja na kufaidika na masoko ya bidhaa zetu kupitia wato miliuoni miamoja waliopo mashariki mwa Kongo.

Mnyonge mnyongeni lakini haki haki yake apewe. Ziara ya Rais wetu huko DRC haipaswi kubezwa kwa sababu kiuchumi inalipa tofauti na nchi kama Rwanda, Burundi na Uganda ambazo zinapitisha mizigo yao katika bandari yetu ya Dar Es Salaam lakini, mizigo yao kidogo kuliko ile DRC kutokana na idadi ya watu katika nchi hizo ni ndogo.

Hongera Mh. Raisi wetu kwa kupanga ziara ya kimkakati ya DRC ambayo ni muhimu sana kwa musakabali wa uchumi wa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom