Rais Samia kufanya ziara ya kikazi ya Siku Tano Nchini Uturuki kuanzia Tarehe 17-21 Mwezi huu

Rais Samia kufanya ziara ya kikazi ya Siku Tano Nchini Uturuki kuanzia Tarehe 17-21 Mwezi huu

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Habari ni kuwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan anatarajia kufanya ziara ya kikazi nchini Uturuki kwa mualiko maalum wa Rais wa nchi hiyo Mheshimiwa Erdogan. Hii imeelezwa na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mheshimiwa Januari Makamba.

Inaelezwa kuwa ziara hii inalenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia,biashara,uchumi,siasa na masuala mengine mbalimbali.inaeleza ya kuwa akiwa nchini humo Mheshimiwa Rais atapata fursa ya kuhudhuria kongamano kubwa la biashara na uwekezaji litakalofanyika mji wa Instanmbul ,ambapo hapo Mheshimiwa Rais atakutana na wafanyabiashara na wawekezaji mbalimbali wakubwa.

Lakini pia Mheshimiwa Rais atakutana na makampuni makubwa 15,ambapo atatumia nafasi kuweza kuwashawishi kuja kuwekeza hapa nchini.imeelezwa pia ya kuwa imepita miaka 14 tangia Rais kutoka Tanzania kuitembelea nchi hiyo,lakini pia imepita miaka 7 tangia Rais wa nchi hiyo aje aitembelee Tanzania,ambapo mara ya mwisho ilikuwa ni 2017 wakati wa utawala wa hayati dkt John Pombe Magufuli.

Imeelezwa pia kuwa uturuki ni miongoni mwa nchi 20 zenye uchumi mkubwa hapa Duniani,na hivyo kuwa nchi muhimu katika kushirikiana nayo na kuweza kufaidika kwa fursa mbalimbali.lakini pia imeelezwa pia kuwa biashara na maingiliano ya nchi hizi mbili yameongezeka sana kwa sasa jambo linalochochea umuhimu wa kukaa pamoja kwa viongozi wetu katika kuimarisha ushirikiano zaidi kwa maslahi ya pande zote mbili.

Kazi iendelee,Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
 
Kazi iendelee SGR

Uhusiano kati ya Türkiye na Tanzania

Ubalozi wa Uturuki jijini Dar es Salaam ulifunguliwa mwaka 1979. Ingawa ulifungwa mwaka 1984 kutokana na ufinyu wa bajeti, ulifunguliwa tena tarehe 18 Mei 2009.

Uhusiano baina ya nchi hizo mbili ulishika kasi baada ya ziara ya aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Türkiye, H.E. Abdullah Gül kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Februari 2009 na kufunguliwa tena kwa Ubalozi wa Uturuki jijini Dar es Salaam mwaka huo huo.

H.E. Jakaya Kikwete, Rais wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya ziara ya kiserikali nchini Türkiye mwaka 2010. Ziara ya Jakaya Kikwete nchini Türkiye ilikuwa hatua muhimu kwa vile ilikuwa ni ziara ya ngazi ya kwanza ya rais kutoka Tanzania kwenda Türkiye na iliakisi kasi iliyopatikana katika mahusiano baina ya nchi hizo mbili.

Rais mstaafu wa Zanzibar Mh. Ali Mohamed Shein alifanya ziara rasmi nchini Türkiye mwaka 2011.

H.E. Rais Recep Tayyip Erdoğan alitembelea Tanzania tarehe 22-23 Januari 2017, akifuatana na Mawaziri wa Mambo ya Nje, Nishati na Maliasili na Uchumi. Katika ziara hiyo, mikataba 10 ilisainiwa ambayo inatoa msingi wa kisheria wa mahusiano yetu katika nyanja za sekta ya ulinzi, elimu, maendeleo, afya, utalii, uchumi wa sekta ya ulinzi na mawasiliano.

Mkutano wa kwanza wa Tume ya Pamoja ya Uchumi ya Türkiye na Tanzania ulifanyika mwaka 2012 jijini Dar es Salaam. Katika hafla ya Mkutano, nchi mbili zilipitia uhusiano wa kiuchumi wa nchi mbili na kutathmini uwezekano wa ziada wa ushirikiano.

Mkutano wa pili wa JEC kati ya Tanzania na Türkiye ulifanyika Ankara tarehe 11-12 Januari 2017.

Kiasi cha biashara kati ya nchi hizo mbili kilikuwa dola milioni 250 mwaka 2020. Kuanzishwa kwa Ubalozi wa Jamhuri ya Türkiye nchini Tanzania na kuanzishwa kwa safari za ndege za moja kwa moja za Shirika la Ndege la Uturuki kati ya Istanbul-Dar es Salaam mwaka 2010 na Istanbul-Kılımanjaro mwaka 2012 ilitolewa. kasi kubwa katika mahusiano ya kiuchumi baina ya nchi hizo mbili.

Source : mfa.gov.tr /relations-between-turkiye-and-tanzania.
 
Rais wa Tanzania Samia Suluhu anatarajiwa kuzuru Uturuki wiki hii. Mama anaupiga mwingi kila siku anapaa tu anaenda kututafutia wanawe chakula..
 
huyu mama hachoki kutupambania watanzania wanyonge wallah

mama piga kazi tuko na wewe bega kwa bega
 
Kazi gani anapiga dola inazidi kupaa na kusababisha maisha kuwa magumu.
Au wewe nawe ni chawa?!
Mbona pesa ya Kenya inaimarika sana dhidi ya dola kwann yetu inazidi kudorora??
Okay basi tuseme afanyi kazi yoyote unapiga kazi ni wewe mkuu🙏🏽
 
Rais Samia anatarajia kuanza ziara ya siku 4 Nchini Uturuki tarehe 17/4/2024 Kwa Mualiko wa Rais huyo wa Taifa kubwa bwana Recep Yayib Erdogan.

Huenda Samia ndio atakuwa Rais wa kwanza kufanya ziara rasmi baada ya bwana Erdogan kuchaguliwa Kwa awamu nyingine ya Uongozi.

Kila la Heri madam president,tunatarajia harakati zako za kufungua masoko ya bidhaa za Tanzania zitaendelea.

Msisahau kuwaambia Waturuki wanazingua kwenye ujenzi wa Sgr na Barabara.

View: https://twitter.com/Hakingowi/status/1779887483766866125?t=w3QblGwyYqLwGvJj2VXQBQ&s=19

My Take
Chini ya Samia diplomasia imeimarika sana ,Kila mbabe wa Dunia anataka Urafiki na Tanzania kuanzia Kwa Joe Hadi Kwa Putin na Sasa ni Kwa wazee wa Yappi Merkez.

Kazi iendelee.

View: https://www.instagram.com/p/C5zjL_niAYz/?igsh=MWkzaXBmYWUxNXU2
 
Back
Top Bottom