Rais Samia kuingia na mlinzi wa kiume msikitini, ni jambo la kawaida. Tuache Mihemko isiyo na Tija

Rais Samia kuingia na mlinzi wa kiume msikitini, ni jambo la kawaida. Tuache Mihemko isiyo na Tija

Nyafwili

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2023
Posts
4,240
Reaction score
10,561
Rais SSH kuingia na mlinzi wa kiume mskitini ni jambo la kawaida kutokana na sababu mbali mbali , hasa kama kuna tishio la usalama au kutokana na idadi kubwa ya watu wanaokusanyika kwa pamoja.

Screenshot_20240617-174202.png
Tujiepushe na mihemko isiyo na tija na badala yake tufikirie suluhisho zinazojenga na kuheshimu maadili ya jamii husika na kuhakikisha usalama na utulivu wa Rais.

Katika Quran, hakuna aya inayosema moja kwa moja kuwa ni marufuku kwa mwanaume kuingia sehemu ya wanawake msikitini. hadithi za Mtume Muhammad (S.A.W) pamoja na mila na desturi za Kiislamu. Kwa mfano, katika hadithi za Mtume Muhammad (S.A.W), kuna maelekezo yanayohimiza heshima na mipaka baina ya wanaume na wanawake wakati wa ibada ili kuepusha fitna na kudumisha heshima.( kuepusha matamanio ya kimapenzi ndani ya ibada. )

Ibn 'Umar aliripoti kwamba Mtume Muhammad (S.A.W) alisema, "Usiwazuie wanawake wa Allah kwenda kwenye misikiti ya Allah" (Sahih Muslim, Kitabu 4, Hadithi 891). Hadithi hii inaonyesha kwamba wanawake wanaruhusiwa kwenda msikitini, lakini haina amri maalum kuhusu maeneo maalum ndani ya msikiti. Kwa hiyo, mpangilio wa ndani wa msikiti kuhusu maeneo ya wanawake na wanaume unaweza kutegemea mila, desturi, na mantiki za kiutawala za msikiti huo na siyo tamko la S. A. W.

Katika mazingira ambapo kuna haja ya kuwepo na walinzi wa kiume kwa sababu za kiusalama, ni kwamba tunahakikisha hatua hizi zinachukuliwa kwa njia inayoheshimu mipaka ya kijinsia na dini, kulinda usalama bila kuvuruga utulivu wa ibada.( na hiki ndo amefanya RAIS SSH wa JMT)

Mtazamo huu unategemea hadithi kama ile inayosimuliwa na Umm Atiyyah, ambaye alisema kwamba wanawake waliokuwa kwenye hedhi waliambiwa wakae mbali na mahali pa kusalia/swalia wakati wa sala za Eid (imesimuliwa na Al-Bukhari na Muslim)

Surah Al-Baqarah (2:222), "Wanakuuliza habari ya hedhi. Sema: Huu ni unajisi. Basi jitengeni na wanawake wakati wa hedhi, wala msiwakaribie mpaka watwahare.( Tusilaumu sana yawezekana mlinzi wa kike alikuwa kwenye Surah Al-Baqarah 2:222 ).

Pia soma: Mlinzi wa kiume wa Rais kuvaa juba (vazi la kike) na kuketi msikitini sehemu ya wanawake ni sawa?
 
Rais SSH kuingia na mlinzi wa kiume mskitini ni jambo la kawaida kutokana na sababu mbali mbali , hasa kama kuna tishio la usalama au kutokana na idadi kubwa ya watu wanaokusanyika kwa pamoja.
View attachment 3019544


Wewe umemuona wapi huyo mwanaume?

PSU wanawake wapo msilete uzushi wa kijinga.
 
Assalamu 'alaikum. Kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (s.a.w.), wanaume na wanawake wanasali katika sehemu tofauti wakati wa ibada katika msikiti. Hii ni kwa sababu ya mambo ya utaratibu na adabu katika ibada.

Kuhusu mavazi, Mtume (s.a.w.) ameamuru wanaume wavae kanzu au nguo ndefu zinazofunika kiganja na magoti. Wanawake wamekwishaelekezwa kuvaa hijab, yaani kufunika vichwa, nyuso na mabega yao wakati wa ibada. Hii ni kwa ajili ya heshima na adabu katika kuabudu.

Hivyo basi, wanaume na wanawake wanasali katika sehemu tofauti, na wanaume wanavaa kanzu au nguo ndefu wakati wa ibada, wakati wanawake wanavaa hijab. Haya ni mafundisho yaliyotolewa na Mtume Muhammad (s.a.w.) kwa ajili ya uadilifu na utaratibu wa ibada.
 
Kama ni jambo la kawaida kulikua na ulazima Gani avae hijabu(disguise) kwanini asingevaa kanzu tu?
Watawala wa Kiafrika wana uoga wa ajabu sana! Inakuwaje sasa mwanaume avae mavazi ya kike na kujichanganya kwa wanawake ndani ya nyumba ya ibada!!

Yaani ndiyo kusema walinzi wa kike hawana uwezo wa kumlinda Boss wao sehemu kama hiyo!!
 
Watawala wa Kiafrika wana uoga wa ajabu sana! Inakuwane sasa mwanaume avae mavazi ya kike na kujichanganya kwa wanawake ndani ya nyumba ya ibada!! Yaani ndiyo kusema walinzi wa kike hawana uwezo wa kumlinda sehemu ya kama hiyo!!
Ina maana huko majeshini hakuna wanawake wenye mafunzo ya kumlinda rais hata hapo msikitini tu?
Hii ni dharau kubwa kwa wanausalama wa kike
 
Back
Top Bottom