Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan atakuwa mubashara au live au waweza kusema ataonekana moja kwa moja kutokea Ikulu katika uapisho wa viongozi mbalimbali aliowateua hapo siku ya jana usiku.
Ambapo katika uapisho huo Rais wetu mpendwa anatarajiwa kutoa hotuba nzito kwelikweli kama ilivyo kawaida yake baada ya kufanya uapisho, hasa katika kutoa maelekezo, matarajio kwa mhusika, maonyo na makatazo pamoja na kugusia Masuala mbalimbali Mtambuka.
Lakini katika siku ya leo inaonyesha hotuba yake itakuwa ya kipekee sana na ambayo itaitetemesha nchi na kuteka anga la siasa za Tanzania. Maana tangia tu kutangazwa kwa uteuzi huo imeonyesha na kuonekana upepo kubadilika ghafla na kuteka mitandao mbambali ya kijamii.
Sasa kama tu taarifa ya uteuzi imeteka mijadala hapa nchini usiku kwa usiku, unafikiri hali itakuwaje pale Amiri Jeshi Mkuu atakapofungua kinywa chake kuzungumza? Kumbuka ya kuwa pia huyu ndiye Rais na kiongozi ambaye anafuatiliwa sana hotuba zake na mamilioni ya watanzania,kwa kuwa hotuba zake hutoa Dira, muelekeo na ramani juu ya Masuala mbalimbali.ni katika hotuba zake ambapo huzitumia katika kuhutubia Taifa pamoja na kutoa maelekezo kwa wizara,taasisi,mashirika na idara mbalimbali za serikali.
Nawakumbusheni pia kuwa Rais wetu mpendwa ni moja au miongoni mwa Wanawake Mia Moja DUNIA wenye ushawishi.Na ndio maana kwa ushawishi wake na kukubalika kwake kitaifa na kimataifa miezi michache iliyopita huko Nchini Ufaransa ,aliweza kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano wa kujadili matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia na kuachana na matumizi ya nishati ya kuni na mkaa ambayo imeonekana kuwa na madhara makubwa kiafya hasa kwa wanawake ambao wamekuwa wahanga wakubwa wa athari hizo.
Ndio maana pia kwa ushawishi na kukubalika kwake ilipelekea Makamu wa Rais wa Marekani na anayetarajiwa kuwa Rais wa Marekani Mheshimiwa Mwana Mama shupavu na madhubuti Kamala Harris aliweza kuichagua Tanzania kuwa sehemu ya Nchi chache sana alizotembelea alipofanya ziara barani Afrika miezi kadhaa iliyopita.
unafikiri ni kwanini? Jibu ni kutokana na ushawishi na kukubalika kwa Mama yetu Mpendwa kitaifa na kimataifa.kunakotokana na uchapakazi kazi wake,kuimarisha demokrasia,kukuza uchumi tena uchumi jumuishi wenye kugusa maisha ya kila mtu na usiomuacha mtu nyuma,kumuinua na kumpa nuru mtoto wa kike kwa kuhakikisha anapata Elimu pasipo vikwazo,kuimarisha Utawala bora na utawala wa sheria,kuzingatia na kuheshimu haki za binadamu na misingi yote ya kisheria na Mengine mengi sana.
Ndio sababu pia vyuo mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali Dunia vimekuwa vikimpatia Udaktari wa heshima Rais wetu na Mama yetu mpendwa katika kutambua mchango na matokeo chanya ya uongozi wake katika maeneo mbalimbali. Rai yangu ni kuwaasa watanzania kutumia uhuru huu aliouweka na kuuachia Rais Samia kuleta tija kwa ustawi wa Taifa letu na siyo kuutumia vibaya kwa kuvunja misingi yote ya haki na demokrasia,kutoa lugha za uchochezi zenye kuhatarisha usalama na utulivu wa Taifa letu na kutoa lugha zenye kuchocheo ubaguzi kwa misingi ya Udini,ukabila, ukanda,jinsia n.k.
Ikumbukwe ya kuwa haki yako inapoishia ndio haki ya mwingine inapoanzia.lakini pia hakuna haki katika katiba yetu ya kumtukana na kumdhalilisha mtu mwingine pasipo sababu,hakuna uhuru usio na mipaka,hakuna demokrasia isiyo na misingi yake na mipaka yake,lakini pia demokrasia siyo cocacola kwamba ifanane DUNIA nzima. Tujitahidi kuheshimu na kuheshimiana katika kukosoana na siyo kudhalilishana, kutukanana na kutoa lugha zenye kuchocheo vurugu na uhasama.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan atakuwa mubashara au live au waweza kusema ataonekana moja kwa moja kutokea Ikulu katika uapisho wa viongozi mbalimbali aliowateua hapo siku ya jana usiku.
Ambapo katika uapisho huo Rais wetu mpendwa anatarajiwa kutoa hotuba nzito kwelikweli kama ilivyo kawaida yake baada ya kufanya uapisho, hasa katika kutoa maelekezo, matarajio kwa mhusika, maonyo na makatazo pamoja na kugusia Masuala mbalimbali Mtambuka.
Lakini katika siku ya leo inaonyesha hotuba yake itakuwa ya kipekee sana na ambayo itaitetemesha nchi na kuteka anga la siasa za Tanzania. Maana tangia tu kutangazwa kwa uteuzi huo imeonyesha na kuonekana upepo kubadilika ghafla na kuteka mitandao mbambali ya kijamii.
Sasa kama tu taarifa ya uteuzi imeteka mijadala hapa nchini usiku kwa usiku, unafikiri hali itakuwaje pale Amiri Jeshi Mkuu atakapofungua kinywa chake kuzungumza? Kumbuka ya kuwa pia huyu ndiye Rais na kiongozi ambaye anafuatiliwa sana hotuba zake na mamilioni ya watanzania,kwa kuwa hotuba zake hutoa Dira, muelekeo na ramani juu ya Masuala mbalimbali.ni katika hotuba zake ambapo huzitumia katika kuhutubia Taifa pamoja na kutoa maelekezo kwa wizara,taasisi,mashirika na idara mbalimbali za serikali.
Nawakumbusheni pia kuwa Rais wetu mpendwa ni moja au miongoni mwa Wanawake Mia Moja DUNIA wenye ushawishi.Na ndio maana kwa ushawishi wake na kukubalika kwake kitaifa na kimataifa miezi michache iliyopita huko Nchini Ufaransa ,aliweza kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano wa kujadili matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia na kuachana na matumizi ya nishati ya kuni na mkaa ambayo imeonekana kuwa na madhara makubwa kiafya hasa kwa wanawake ambao wamekuwa wahanga wakubwa wa athari hizo.
Ndio maana pia kwa ushawishi na kukubalika kwake ilipelekea Makamu wa Rais wa Marekani na anayetarajiwa kuwa Rais wa Marekani Mheshimiwa Mwana Mama shupavu na madhubuti Kamala Harris aliweza kuichagua Tanzania kuwa sehemu ya Nchi chache sana alizotembelea alipofanya ziara barani Afrika miezi kadhaa iliyopita.
unafikiri ni kwanini? Jibu ni kutokana na ushawishi na kukubalika kwa Mama yetu Mpendwa kitaifa na kimataifa.kunakotokana na uchapakazi kazi wake,kuimarisha demokrasia,kukuza uchumi tena uchumi jumuishi wenye kugusa maisha ya kila mtu na usiomuacha mtu nyuma,kumuinua na kumpa nuru mtoto wa kike kwa kuhakikisha anapata Elimu pasipo vikwazo,kuimarisha Utawala bora na utawala wa sheria,kuzingatia na kuheshimu haki za binadamu na misingi yote ya kisheria na Mengine mengi sana.
Ndio sababu pia vyuo mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali Dunia vimekuwa vikimpatia Udaktari wa heshima Rais wetu na Mama yetu mpendwa katika kutambua mchango na matokeo chanya ya uongozi wake katika maeneo mbalimbali. Rai yangu ni kuwaasa watanzania kutumia uhuru huu aliouweka na kuuachia Rais Samia kuleta tija kwa ustawi wa Taifa letu na siyo kuutumia vibaya kwa kuvunja misingi yote ya haki na demokrasia,kutoa lugha za uchochezi zenye kuhatarisha usalama na utulivu wa Taifa letu na kutoa lugha zenye kuchocheo ubaguzi kwa misingi ya Udini,ukabila, ukanda,jinsia n.k.
Ikumbukwe ya kuwa haki yako inapoishia ndio haki ya mwingine inapoanzia.lakini pia hakuna haki katika katiba yetu ya kumtukana na kumdhalilisha mtu mwingine pasipo sababu,hakuna uhuru usio na mipaka,hakuna demokrasia isiyo na misingi yake na mipaka yake,lakini pia demokrasia siyo cocacola kwamba ifanane DUNIA nzima. Tujitahidi kuheshimu na kuheshimiana katika kukosoana na siyo kudhalilishana, kutukanana na kutoa lugha zenye kuchocheo vurugu na uhasama.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.