Rais Samia: Kulikuwa na vinenoneno miradi haitaendelea, inaendelezwa kuliko ilivyokuwa ikiendelea

Rais Samia: Kulikuwa na vinenoneno miradi haitaendelea, inaendelezwa kuliko ilivyokuwa ikiendelea

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Rais Samia Suluhu akiwa mkoani Mara kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji ameongelea suala la miradi ya Serikali. Ameuongelea mradi huo ulioanzishwa na Serikali ya awamu ya tano lakini ukakwamishwa na mkandarasi na kuamua kumbadilisha ili kumalizia mradi. Pia Rais Samia ameongelea spidi ya maendeleo ya miradi kwenye Serikali ya awamu sita.
========

Rais Samia: Serikali yenu tulisema kazi iendelee na kazi inaendelea, najua ndugu zangu kulikuwa na vinenoneno kadhaa, elimu haitaendelea, miradi haitaendelea na mambo mengine kadhaa, lakini nadhani mnajionea wenyewe kwa macho yenu kwamba miradi inaendelea na inaendelezwa kuliko ilivyokuwa ikiendelea, kwahiyo kazi iendelee.

Mwisho Rais ameongelea miradi ya mkoa wa Mara kusuasua na kusema leo mchana atalisemea wakati akizindua hospitali ambapo watatafuta sababu ya kusuasua na pengine kuitafutia dawa na wakiona wanachukua hatua wananchi wajue wanatafutiwa dawa.
 
Kila siku vineno vineno .... Maneno maneno mama acha TAARAB fanya kazi
 
Mwambieni mama hakuna hakimu mzuri Kama muda.

Amepata urais kwa kudra za mwenyezi Mungu Ni vizuri afanye kazi asije akamuaibisha MUNGU

Aache tambo na majigambo ccm hawajawahi kuwa watu wazuri

2025
 
Hili jambo la ajabu namna hii lingekuwa limetokea kwenye nchi zinazojitambua usingemkuta Samia Ikulu sasa hivi...
Endelea kupambana kumuondoa ikulu na video yako, hujakatazwa na yoyote bado na maendeleo si mabaya. Taratiiiibu unafahamika na wengi.
 
Back
Top Bottom