Rais Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa

Rais Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa

Uki-give in katika suala moja, basi na wengine wote wanapata picha kwamba huyu tukimtikisa huwa ana-give in, na hapo wote wataanza kukusumbua, hadi Kenya atasema mlima Kilimanjaro ni wake, na ataleta mikataba yake ya kikoloni anayoijua yeye, lazima uwe na principles.
Huyu jamaa anachekesha sana kama mafuta yapo upande wa Malawi waache wachimbe ila kama yapo Tanzania ni ya kwetu hatuwezi kugawana rasilimali kwa sababu tu ya kuridhishana
 
Rudi darasani kijana! Huku umerusha upupu mtupu! Nashukuru waelewa wa mambo wamekujibu!
Nadhani unaona aibu kwa kuongea bila ufahamu wa hivi vitu. Kuna wakati ni bora kukaa kimya, sio lazima utoe comments kwenye kila thread. Ukikosa cha kusema nenda kule kwenye thread za Mwajuma kamfumania mumewe na rafiki yake akagoma kupika, huko utakuwa na wigo mpana wa ku-comment, maana hizi thread sio size yako.
 
Huyu jamaa anachekesha sana kama mafuta yapo upande wa Malawi waache wachimbe ila kama yapo Tanzania ni ya kwetu hatuwezi kugawana rasilimali kwa sababu tu ya kuridhishana
Mkuu, unaelewa jiolojia ya mafuta kabla hata ya kusema hivyo? Mafuta yanakuwa ndani ya mwamba, na ukisema kila mtu achimbe upande wake inawezekana kabisa mkawa mnachimba tola reservoir moja. Pili kumbuka context ya thread ziliwekwa kama reference ni kwamba uwezekano wa kukubaliana mpaka uko wapi ni mdogo. Sasa tutachimbaje kila mtu upande wake wakati hautujaelewana kila mtu upande wake ni wapi? Tutaishia kutoelewana juu ya hilo hadi mafuta yapoteze thamani.

Hivi kwa nini watu wengine mnakuwa wagumu sana kusoma na kuelewa maandishi na mnaishia kusema huyu anachekesha?
 
Mkuu, unaelewa jiolojia ya mafuta kabla hata ya kusema hivyo? Mafuta yanakuwa ndani ya mwamba, na ukisema kila mtu achimbe upande wake inawezekana kabisa mkawa mnachimba tola reservoir moja. Pili kumbuka context ya thread ziliwekwa kama reference ni kwamba uwezekano wa kukubaliana mpaka uko wapi ni mdogo. Sasa tutachimbaje kila mtu upande wake wakati hautujaelewana kila mtu upande wake ni wapi? Tutaishia kutoelewana juu ya hilo hadi mafuta yapoteze thamani.

Hivi kwa nini watu wengine mnakuwa wagumu sana kusoma na kuelewa maandishi na mnaishia kusema huyu anachekesha?
Mimi hoja yangu ni wapi mafuta yanapatika hayo mengine siyo ya msingi, Zanzibar waliondoa maswala ya mafuta na gesi baada ya kuhisi wanaweza kupata mafuta baharini
 
Mimi hoja yangu ni wapi mafuta yanapatika hayo mengine siyo ya msingi, Zanzibar waliondoa maswala ya mafuta na gesi baada ya kuhisi wanaweza kupata mafuta baharini
Nchi za Uingereza, Norway na Denmark waligundua mafuta kule North Sea. Sasa ili wasiingie kwenye huu ubishi wa kijinga kama tulio nao na Malawi, wakaamua kufanya ubia wakijua mwamba wa mafuta utakuwa umesambaa sehemu zote, badala ya kila nchi kujikakamua kuchimba upande wake. Kwa hiyo nimeanzia hapo - shule inasaidia hatuongei tu vitu hivi. Haina maana kugombana na Malawi juu ya mpaka kwa ajili ya mafuta wakati ni wazi mwamba wa mafuta ndani ya ziwa Nyasa utakuwa umesambaa sehemu ya Malawi na Tanzania

1621533033373.png
1621533359347.png
 
Na hayo magari ya kutumia mafuta mtatengeneza wenyewe? Na spare zake?

Na kuchimba mafuta kwa ajili ya soko la ndani ya nchi peke yake is not economical
Kwani mafuta tunatumia kwenye magari na bodaboda tu? Vipi Boti na Meli kubwa za mizigo? Vipi ndege za abiria na mizigo na za kivita? vipi magenerator? hata sabuni za kufulia nazo, Lami?

In short mafuta bado yataendelea kutumika tu na hasa Africa. Kama ishu ya kupiga vita mafuta kisa inachafua mazingira, basi ni bora waekeze kwenye Research and Development na kupunguza uchafuzi wa mazingira. Mfano Diesel pekee came a long way, tangu unakuta ki sedan kinatoa moshi hadi sasa unakuta Range Rover diesel haitoi moshi. Sijaona souce of energy ambayo tunaweza kutumia bila kuharibu mazingira. Hizo Batteries nazo ndo ivo ivo. Nuclear power ingekuwa good replacement ila shida ipo kwenye radiation na waste.
 
Mafuta yanakaribia kugunduliwa kwenye maeneo karibu ya Ziwa eyasi , tabora na simiyu kwa mujibu wa waziri wa nishati na uzalishaji ukianza watatumia bomba la tanga

Mama alitoa maelekezo wataalamu wa Tanzania washirikiane na wataalamu wa Uganda matokeo yameanza kuonekana

Kuhusu ziwa tanganyika hakuna waasi ni vibaka wa kawaida tu, waasi wapo upande wa kaskazini jimbo la kivu mpaka wa DRC na Rwanda na uganda
 
Nchi za Uingereza, Norway na Denmark waligundua mafuta kule North Sea. Sasa ili wasiingie kwenye huu ubishi wa kijinga kama tulio nao na Malawi, wakaamua kufanya ubia wakijua mwamba wa mafuta utakuwa umesambaa sehemu zote, badala ya kila nchi kujikakamua kuchimba upande wake. Kwa hiyo nimeanzia hapo - shule inasaidia hatuongei tu vitu hivi. Haina maana kugombana na Malawi juu ya mpaka kwa ajili ya mafuta wakati ni wazi mwamba wa mafuta ndani ya ziwa Nyasa utakuwa umesambaa sehemu ya Malawi na Tanzania

View attachment 1792106View attachment 1792109
Sidhani kama umetia shule, ungetumia shule ungeelewa nini kiini cha ugomvi wa Malawi na Tanzania.
Ugomvi wa Malawi na Tanzania unatokana na Malawi kutaka kujimilikisha ziwa lote Nyasa lakini wewe umeleta hoja mfu nyie ndio mkonTanzania mkijifanya watanzania kumbe sio watanzania si ajabu ni ukoo wa kina Karume
 
Kwani mafuta tunatumia kwenye magari na bodaboda tu? Vipi Boti na Meli kubwa za mizigo? Vipi ndege za abiria na mizigo na za kivita? vipi magenerator? hata sabuni za kufulia nazo, Lami?

In short mafuta bado yataendelea kutumika tu na hasa Africa. Kama ishu ya kupiga vita mafuta kisa inachafua mazingira, basi ni bora waekeze kwenye Research and Development na kupunguza uchafuzi wa mazingira. Mfano Diesel pekee came a long way, tangu unakuta ki sedan kinatoa moshi hadi sasa unakuta Range Rover diesel haitoi moshi. Sijaona souce of energy ambayo tunaweza kutumia bila kuharibu mazingira. Hizo Batteries nazo ndo ivo ivo. Nuclear power ingekuwa good replacement ila shida ipo kwenye radiation na waste.
Sasa wewe, unafikiri hadi wakaamua kukomesha matumizi ya mafuta yote hayo hawajafikiria? Wewe unaingilia field za watu na kutoa point ambazo hazina mshiko. Hiyo neclear power utatumia kwenye magari? Na unajua athari na gharama zinazotokana na nuclear power? Kwa taarifa yako nchi zilianza kuondokana na nuclear power kabla hata hawajaanza kufikiria kuondokana na mafuta.

Ngoja nikueleweshe kidogo; usichanganye kati ya ambient air pollution ya mafuta na greenhouse gas emission ya mafuta. Unaweza ukapunguza sana ambient air pollution lakini greenhouse gas emission zikabaki pale pale. Kwenye ambient air pollution hatua imepigwa katika kupunguza kiwango cha sulfur and particulates, na kukomesha kuweka Lead kwenye mafuta, ndio maana unasikia kuanzia sasa Leaded Petrol hairuhusiwi, au Diesel inayoruhusiwa ni 50ppm au 10ppm. Hiyo ni pollution, lakini hata ukiwa na na unleaded Petrol au Diesel safi ambayo tunaita Ultra-low-sulfur diesel (ULSD), bado haipunguzi greenhouse gas emissions. Unakuwa umepunguza pollutants.

Ndio maana basi, msukumo mkubwa wa kukomesha mafuta uko kwenye kuzuia emissions za greengose gases ambazo zinasababisha climate change, na ndio maana kwa sasa hata mvua za dhoruba zinainyemelea Tanzania ambapo ni jambo la ajabu. Tunaona mvua kubwa za mafuriko na ukame ukiongezeka kwa ajili ya climate change, ambayo kwa kiwango kikubwa inasababishwa na matumizi ya mafuta. Ndio maana dunia imeamua kuachana na mafuta, sasa watu kama nyie acheni kung'ang'ania tekinolojia zilizopitwa na wakati
 
Sidhani kama umetia shule, ungetumia shule ungeelewa nini kiini cha ugomvi wa Malawi na Tanzania.
Ugomvi wa Malawi na Tanzania unatokana na Malawi kutaka kujimilikisha ziwa lote Nyasa lakini wewe umeleta hoja mfu nyie ndio mkonTanzania mkijifanya watanzania kumbe sio watanzania si ajabu ni ukoo wa kina Karume
Acha upoyoyo. Sasa kusema ugomvi wa Tanzania na Malawi ni Malawi kutaka kujimilikisha ziwa lote, na kusema kuna mgogoro wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania kuna tofauti gani? Wewe unafikiri Malawi wameibuka tu na kusema tunataka Ziwa lote? Kama wangefanya hivyo kungekuwa na haja ya kuwaweka watu kama kina Mbeki wasuluhishe?

Yaani leo Kenya wakiibuka na kusema Mlima Kilimanjaro ni wetu, unadhani dunia itahangaika kuweka tume za kusuluhisha kati ya Tanzania na Kenya? Kinakachotokea ni Kenya kushutumiwa na UN na jumuia za kimataifa na kuambiwa waache kabisa kuleta mgogoro usiokuwapo la sivyo watachukuliwa hatua za kimataifa.

Usuluhishi unakuja pale ambapo nchi inayodai mpaka inakuwa na sababu za msingi, na ukiangalia madai ya Malawi juu ya ziwa Nyasa yana msingi, lakini pia madai ya Tanzania juu ya mpaka kuwa katikati ya ziwa yana msingi. Ndio maana zinaundwa tume za usuluhishi za kina Mbeki na Chisano.

Vitu huvielewi lakini unatanguliza domo lako kubwa kuropoka, eti umeleta hoja mfu.
 
Kwani mafuta tunatumia kwenye magari na bodaboda tu? Vipi Boti na Meli kubwa za mizigo? Vipi ndege za abiria na mizigo na za kivita? vipi magenerator? hata sabuni za kufulia nazo, Lami?

In short mafuta bado yataendelea kutumika tu na hasa Africa. Kama ishu ya kupiga vita mafuta kisa inachafua mazingira, basi ni bora waekeze kwenye Research and Development na kupunguza uchafuzi wa mazingira. Mfano Diesel pekee came a long way, tangu unakuta ki sedan kinatoa moshi hadi sasa unakuta Range Rover diesel haitoi moshi. Sijaona souce of energy ambayo tunaweza kutumia bila kuharibu mazingira. Hizo Batteries nazo ndo ivo ivo. Nuclear power ingekuwa good replacement ila shida ipo kwenye radiation na waste.
Hi mbona watu wagumu sana kuelewa mambo madogo kama haya? Mbona nimejibu hoja yako hapo juu?

Ni hivi, matumizi ya mafuta kwenye magari ni karibu 70% ya mafuta yanayozalishwa. Sasa ukipunguza hiyo 70% kwenda labda 30%, bei ya mafuta itashuka sana, kwa kuwa unakuwa umepunguza demand ya mafuta. Exploration na production ya mafuta kwa ajili ya matumizi yaliyobaki inakuwa sio economically feasible kwa uzalishaji mdogo mdogo. Watakaoweza kuendelea kuzalisha mafuta ni makampuni makubwa ambayo wao economies of scale zinafanya production cost zao kuwa chini. Hivyo wazalishaji wadogo kama Tanzania, Uganda nk itabidi wafunge production zao kwa kuwa itakuwa hasara wao kuendelea kuzalisha mafuta.

Sasa kama shule yako ni ndogo hapo nitakuwa nimekuchanganya sana!
 
Acha upoyoyo. Sasa kusema ugomvi wa Tanzania na Malawi ni Malawi kutaka kujimilikisha ziwa lote, na kusema kuna mgogoro wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania kuna tofauti gani? Wewe unafikiri Malawi wameibuka tu na kusema tunataka Ziwa lote? Kama wangefanya hivyo kungekuwa na haja ya kuwaweka watu kama kina Mbeki wasuluhishe?

Yaani leo Kenya wakiibuka na kusema Mlima Kilimanjaro ni wetu, unadhani dunia itahangaika kuweka tume za kusuluhisha kati ya Tanzania na Kenya? Kinakachotokea ni Kenya kushutumiwa na UN na jumuia za kimataifa na kuambiwa waache kabisa kuleta mgogoro usiokuwapo la sivyo watachukuliwa hatua za kimataifa.

Usuluhishi unakuja pale ambapo nchi inayodai mpaka inakuwa na sababu za msingi, na ukiangalia madai ya Malawi juu ya ziwa Nyasa yana msingi, lakini pia madai ya Tanzania juu ya mpaka kuwa katikati ya ziwa yana msingi. Ndio maana zinaundwa tume za usuluhishi za kina Mbeki na Chisano.

Vitu huvielewi lakini unatanguliza domo lako kubwa kuropoka, eti umeleta hoja mfu.
Poyoyo ni wewe unayekuja na hoja zisizo nq mashiko mara ulaya wameacha kutumia mafuta hivi unafahamu ni mwaka wa ngapi nchi za Scandinavia zimeacha.kutumia mabasi yanayotumia mafuta na diesel halafu unakurupuka kurupuka au unatafuta cheo ungeweka na namba yako ya simu kabisa
 
Halafu ulivyo kilaza hujui investment ya uchimbaji wa mafuta na geai return yake inarudi baada ya muda gani
 
Poyoyo ni wewe unayekuja na hoja zisizo nq mashiko mara ulaya wameacha kutumia mafuta hivi unafahamu ni mwaka wa ngapi nchi za Scandinavia zimeacha.kutumia mabasi yanayotumia mafuta na diesel halafu unakurupuka kurupuka au unatafuta cheo ungeweka na namba yako ya simu kabisa
Poyoyo twice, hata haieleweki unabisha nini sasa, maana unaunga mkono hoja bila kujitambua
 
Halafu ulivyo kilaza hujui investment ya uchimbaji wa mafuta na geai return yake inarudi baada ya muda gani
Kilaza ni wewe, return za investment haina muda maalum kama unavyofikiria. Inategemea ni development off shore, onshore, na kama offshore ni deep sea nk. Na pia inategemea reservoir pressure, crude type nk. Inategemea pia cost za well development, acquisition agreement na hata vitu kama production sharing agreement, levies nk.

Sasa upo hapo? Domo kubwa masikio madogo, kujifanya unajua kumbe huna kitu. Nani alikuambia kuna fixed time ya return kwenye oil production? Mtafute nimtukane.
 
Moderators wa JF mnazingua sana. Mmebadilisha kichwa cha thread na kutoka nje kabisa ya topic. Lengo haikuwa kusema kuna dalili za mafuta, bali kuweka mkazo kwamba lazima tuharakishe ku-utilize hii resource kwa kuwa kuna kasi ya kuacha kutumia mafuta duniani. Kwa nini mnafix vitu ambavyo havina tatizo, na kuishia kuharibu? Ndio maana kuna wakati niliacha kabisa kuandika thread kwa ajili ya mambo yenu kama haya


Raisi Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa. Tusipoyachimba ndani ya miaka kumi ijayo hayatakuwa na faida tena kwetu

Raisi Samia, nadhani una taarifa kwamba kuna kila dalili za mafuta ndani ya Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa. Hakuna maendeleo yaliyofanyika kuchimba mafuta katika maeneo haya kutokana na vikwazo viwili;
  1. Upande wa ziwa Tanganyika kuna kikwazo cha waasi wa DRC. Si rahisi kuendeleza mradi wa mafuta ziwani Tanganyika ikiwa waasi hawa wa DRC hawajaondolewa kabisa. Na mafuta haya yataendelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na DRC, ndio maana Tanzania ilikuwa tayari kupeleka jeshi DRC kusaidia kuondosha waasi ili tuchimbe haya mafuta kwa ushirikiano na DRC. Inaonekana zoezi la kuondoa waasi limekwama, na hiki kimekuwa kikwazo.
  2. Upande wa ziwa Nyasa kuna mafuta. Lakini pindi ilipoonekana Ziwa Nyasa lina mafuta tuliingia katika mgogoro wa mpaka kati yetu na Malawi. Wakijua rasilimali ya mafuta iloiyomo ziwani, Malawi walianza kudai ziwa Nyasa lote liko upande wa Malawi na ndio maana wao wanalitambua kama Ziwa Malawi. Nilipendekeza humu JF kwamba tuachane na suala la mgororo wa mpaka na jirani zetu Malawi tukubaliane nao kwamba rasilimali yoyote ya mafuta ndani ya ziwa tutagawana 50/50 bila kujali iko upande gani. Sijui kama nilisikilizwa.
Sasa kuna tatizo. Kutokana na tatizo la mabadiliko ya mazingira (climate change), mataifa makubwa duniani yameweka mkakati wa kuacha kutumia mafuta kwa ajili ya magari na mitambo. Norway kwa mfano, wanasema kufikia 2050 wataacha kabisa shughuli za kuchimba mafuta. Uingereza wanasema watapiga marufuku magari ya kutumia diesel kufikia 2025 nadhani. Japan, Germany na hata China, wote wanasema ndani ya miaka 15 ijayo wanataka kutoka kwenye kutumia mafuta kwenye magari na kuingia kwenye magari ya umeme (from internal combustion engines to electric vehicles)

Sasa hii inamaanisha nini kwa nchi kama Tanzania ambazo hadi sasa zimekalia tu uchumi wa mafuta bila kuuendeleza? Ina maana ndani ya miaka 20 ijayo, mafuta yatakuwa si mali kitu. Hata ukigundua una mafuta mengi kama bahari ya Hindi, hayatakusaidia tena kwa kuwa dunia imeanza kuondoka toka tekinolojia ya mafuta kwenda teknolojia ya umeme!

Hivyo basi, kama kweli tunataka kufaidika na rasilimali ya mafuta tuliyonayo, ni lazima iendelezwe ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo. La sivyo haya mafuta yatakuwa na rasilimali isiyohitajika tena duniani, na ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo tutaanza kushuhudia kuporomoka kwa bei ya mafuta kadiri magari ya umeme yanavyoingia sokoni. Leo hii hata Lamborghini wamesema wataacha kutengeneza gari za mafuta!

Kwa hiyo kaza mwendo tuweke mkakati wa kuchimba mafuta Lake Tanganyika na Nyasa. Tatua changamoto zinazokabili maeneo haya. Waambie TPDC waache ku-weka areas with the highest oil potential for last. Ikiwezekana, wafanye mkupuo mmoja wa kugawa vitalu vya kufanya oil and gas exploration kwa nchi nzima, time is of essence, waache mwendo wa bata.

Tukiweza kuchimba mafuta ndani ya miaka kumi ijayo, yatachangia sana kuinua uchumi wetu, tutakuwa na barabara za rami hadi vijijini! Tukichelewa, haya mafuta hayatatusaidia, yatakuwa obsolete resource!

Angalia pia:

Suluhisho la mgogoro na Malawi ni hili; sio suala la ziwa wala mpaka

Suala la uwepo wa mafuta katika ziwa Nyasa na kusababisha mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi limeishia wapi?

Katika awamu hii chini ya Rais mpya Malawi, Magufuli atumie fursa hii kutatua mgogoro wa mpaka kati ya Malawi na Tanzania
Uko tushachelewa sana tungwekeza kwenye kilimo both organic and modern farming, na viwanda especially agri business na mining hasahasa refinery mana haiwezekani ndo nchi ya 2 au 3 afrikaans then hatuna refinery kabisa au si za kutosha. Yani hii nchi imechelwa kila kitu na kila siku tunazidi kurudi nyuma. Tuwekeze viwanda na kilimo na sio mimafuta ambayo tumeshachelewa sana.
 
Kilaza ni wewe, return za investment haina muda maalum kama unavyofikiria. Inategemea ni development off shore, onshore, na kama offshore ni deep sea nk. Na pia inategemea reservoir pressure, crude type nk. Inategemea pia cost za well development, acquisition agreement na hata vitu kama production sharing agreement, levies nk.

Sasa upo hapo? Domo kubwa masikio madogo, kujifanya unajua kumbe huna kitu. Nani alikuambia kuna fixed time ya return kwenye oil production? Mtafute nimtukane.
Wewe umechemka kwanza umshauri rais kama nani mtu mwenyewe una mbele wala nyuma
 
Kichwa maji , akili fupi bichwa kubwa ! idiot .Rudi Facebook k wewe
Utumwa wa akili unakusumbua sana, yani unaamini mzungu ndio mungu wako. Huwezi kupanga jambo lako bila kumuwaza mzungu.
Nyie ndio mnauza utu wenu pumbavu sana, kila kitu unawaza wazungu, wazungu wasipofanya hivi.
Hi dunia sio ya wazungu tu.
Ndio maana wazungu wanawaelekeza muoane pumbavu kama wewe unaweza kuwasapoti.
Maisha yanawezekana bila wazungu.
Usitake kunilazimisha niamini unavyoamini, acha kulazimisha mawazo yako yawe kweli kwa watu wote ni upumbavu.
 
Wewe umechemka kwanza umshauri rais kama nani mtu mwenyewe una mbele wala nyuma
Kiwango cha shule yako hata Kiswahili hakikukusaidia kukielewa, itakuwa issue kama hizi za elimu ya juu? Wewe kama kimya watu waliosoma wajadili hili suala.
 
Back
Top Bottom