Rais Samia, kuna Fursa nyingine huko 'Kazungula Bridge'

Rais Samia, kuna Fursa nyingine huko 'Kazungula Bridge'

Kuna kazi kubwa sana Mama Samia anatakiwa kuifanya. Nayo ni kufanya uwekezaji wa kimaendeleo kulingana na faida za kiuchumi na sio Kwa sababu ya nani anatoka wapi. Kati ya Mambo ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi Kwa kiwango kikubwa hapa Tanzania ni hili.
Ebu fikiria Lami inayoishia Kibaoni kwao Pinda unaweza kukaa bale barabarani masaa zaidi ya matatu bila kuona gari wala pikipiki ikipita kwenye hiyo barabara...unajiukiza ilijengwa kwasababu Pinda ni Waziri mkuu?

Je barabara na daraja lililokua linaunganisha Tabora na Katavi imelaza watu njiani miaka mingi sana. Sehemu ya masaa matano watu wanakaa siku mbili barabarani na ni njia ya kufungua uchumi wa nchi na nchi achilia mbali mkoa kwa mkoa.
Ukibahatika kutembea ndani ya nchi hii unaweza kushangaa mengi sana.

Chukulia ile boarder ya kuunganisha Kenya na Tanzania upande wa Rorya - Shirati. Upande wa Kenya wamejenga majengo yao vizuri na wanakusanya mapato ila upande wa Tanzania shida kwelikweli. Licha ya ushauri uliokwisha tolea na ofisi ya CAG kuhusu ujenzi wa hizi boarde
 
Sahihisho dogo: kigezo rasmi cha SGR (Standard Gauge Railway) ni urefu kati ya reli ya kushoto na kulia (gauge) ambayo ni sentimita 1,435. Unaweza kufananisha na urefu wa axle ya magurudumu ya treni. Njia inaweza kuwa au isiwe ya umeme.

TAZARA imejengwa kwa kigezo cha Cape Gauge (sentimeta 1,067). Hii ndiyo gauge ya mtandao wote wa reli kusini mwa Afrika kuanzia Zambia hadi Cape Town. TAZARA iliunganishwa na mtandao huu kwa kusudi maalum. Ni kampuni binafsi ya GAUTRAIN ya Afrika ya Kusini pekee ndio yenye mtandao wake wa SGR ndani ya nchi hiyo kwa huduma ya abiria.

Bila shaka naamini ulitaka kusema miundombinu ya TAZARA iimarishwe na njia kuwekewa umeme lakini si kuibadilisha kuwa SGR. Lengo la uzi lingepotea.
Hakuna shida pia ile reli ikibadilishwa na kuwa kwa viwango vya SGR na kuwekewa umeme Pia.
 
Ebu fikiria Lami inayoishia Kibaoni kwao Pinda unaweza kukaa bale barabarani masaa zaidi ya matatu bila kuona gari wala pikipiki ikipita kwenye hiyo barabara...unajiukiza ilijengwa kwasababu Pinda ni Waziri mkuu?

Je barabara na daraja lililokua linaunganisha Tabora na Katavi imelaza watu njiani miaka mingi sana. Sehemu ya masaa matano watu wanakaa siku mbili barabarani na ni njia ya kufungua uchumi wa nchi na nchi achilia mbali mkoa kwa mkoa.
Ukibahatika kutembea ndani ya nchi hii unaweza kushangaa mengi sana.

Chukulia ile boarder ya kuunganisha Kenya na Tanzania upande wa Rorya - Shirati. Upande wa Kenya wamejenga majengo yao vizuri na wanakusanya mapato ila upande wa Tanzania shida kwelikweli. Licha ya ushauri uliokwisha tolea na ofisi ya CAG kuhusu ujenzi wa hizi boarder.
Kuna shida sana ya vipaumbele vyenye tija kwenye maendeleo kwa hapa Tanzania.

Tuzidi kumuhamasisha mama Samia kufanya mabadiliko chanya kwa mustakabali wa maendeleo ya kweli ya Tanzania yetu
 
👏👏👏 Ulivyoanza kulizungumzia hili kwa kulinganisha ndio umenifumbua macho, mitazamo yenye fikra pana namna hii ndio inayobadilisha mambo makubwa kuwa mazuri na kwa muda mfupi, inshallah natamani uzi huu uonwe na wenye vyeo vyao.
Kweli kabisa
 
Back
Top Bottom