Rais Samia kusaini EPA huko Brussels?

Rais Samia kusaini EPA huko Brussels?

Status
Not open for further replies.
Acha ushabiki maandazi kama wa yule marehemu.... utamudu bidhaa ya ulaya wewe?

EPA ilikataliwa kishabiki sana.
 
wenzio huku west africa juice zao nyingi za kutoka Europa. Wenye viwanda kazi kwao hili washindane na imported goods. Je mazao yetu yana kiwango cha kushindana na wakulima wa mabeberu au ndo tutauza tu kwa wenzetu hapa Africa?
Swala ni kusaini afu kama kuna vikwazo vya kuzuia Mazao yetu lazima yawekwe sawa..

Kupinga kila kitu ni ujinga mwingine.Hata sasa tuna import karibu kila ekutoka China Sasa unakwepa nini?
 
Vita ya uchumi ilimshinda Nyerere nani mwingine ataweza? Ujamaa wake ulianguka chali akasalimu amri akabaki kukejeli economic reforms kila akiongea.
Pia umesababisha wananchi kuwa mazuzu kusubiria kila kitu serikali na kulaumu,hatujui ubunifu na kuchangamkia fursa.

Ndio maana mimi naona turuhusu afu kwa njia hiyo tutajifunza kuwa aggressive badala ya kubaki na kurithishana maujinga yetu.

Naunga mkono Rais kusaini.
 
Inasikitisha mno hii tabia ya ku undo kila lilofanyika awamu ya tano.

Hata kama hatukumpenda Magufuli basi wakati tukiachana na mambo yake tuangalie kama alifanya kwa maslahi ya Taifa ama la.
Kuna maslahi ya taifa na maslahi ya watu wa taifa.Magu alipendelea maslahi ya taifa na mama anapendelea maslahi ya watu wa taifa.
 
Ile Trade Agreement EPA iliyokuwa inapingwa kwa kila hali na CCM sasa kusainiwa na Raisi wa Tanzania Samia huko Brussels kwenye EU- Afrika Union summit..
Hii Agreement Rais aliyesoma na kuelewa madhara yake alikuwa Mheshimiwa Mkapa kisha Mheshimiwa Kikwete akamwuunga mkono. Ingefaa tuelezwe Umoja wa Ulaya wamekubali nini sasa ndiyo tunakubali masharti yao. Dosari kubwa ya mkataba uliokuwa unakataliwa ni kwamba Jumuiya ya Ulaya walikuwa wanazembea upande wao wa kutuendeleza katika sekta za uzalishaji, hususan kutoka viwandani.
 
Ile Trade Agreement EPA iliyokuwa inapingwa kwa kila hali na CCM sasa kusainiwa na Raisi wa Tanzania Samia huko Brussels kwenye EU- Afrika Union summit...

Kwanza umekurupuka. Unaongea uvumi, pili unatakiwa kuweka mkataba hapa na sio kuongea kishabiki. Hatuwezi kuchangia uzushi na bila vielelezo. Kama ni mawazo yako binafsi sema kwamba unaongea bila kujua mkataba ukoje.
 
Tukisaini ndio tutapata access kubwa ya Soko la Ulaya,kwa sasa iko bilateral zaidi .

Nani amekudanganya ? Kwa sasa hivi Tanzania tunaqualify kuuza chochote EU bila ya kodi maadamu tunatimiza masharti na kupata certificate, hatuhitaji EPA au kuiweka vingine wanaouza mazao leo EU hakuna kitakachobadilika, au unafikiri hizo parachichi zinazouzwa sasa hivi zinashindanishwa kwenye world market ? Hakuna, tunapewa upendeleo maalumu tayari !
 
Nani amekudanganya ? Kwa sasa hivi Tanzania tunaqualify kuuza chochote EU bila ya kodi maadamu tunatimiza masharti na kupata certificate, hatuhitaji EPA au kuiweka vingine wanaouza mazao leo EU hakuna kitakachobadilika!
Vingi tuu vitabadilika,badala ya Nchi kujaa bidhaa hafifu za China sokoni sasa walau tutapata bidhaa mbadala kutoka EU.
 
Vingi tuu vitabadilika,badala ya Nchi kujaa bidhaa hafifu za China sokoni sasa walau tutapata bidhaa mbadala kutoka EU.

Kwa gharama ya Viwanda vyetu ? Vipi kuhusu ajira za watu wetu waliojiriwa kwenye hivi viwanda vyetu? Vipi kuhusu mapato ya kodi tunayoyapata sasa hivi kwa kutoza kodi imports ? Nani atafidia hiyo yote ?
 
Kwanza umekurupuka. Unaongea uvumi, pili unatakiwa kuweka mkataba hapa na sio kuongea kishabiki. Hatuwezi kuchangia uzushi na bila vielelezo. Kama ni mawazo yako binafsi sema kwamba unaongea bila kujua mkataba ukoje.

Kama unaona ni uzushi basi potezea tu.
 
Kwa gharama ya Viwanda vyetu ? Vipi kuhusu ajira za watu wetu waliojiriwa kwenye hivi viwanda vyetu? Vipi kuhusu mapato ya kodi tunayoyapata sasa hivi kwa kutoza kodi imports ? Nani atafidia hiyo yote ?
Saizi bidhaa za china zinajaa kwa gharama ya viwanda vya nani? Mna viwanda nyie au ni vya investors? Wao wataji tune kuendana na bit.

Kwani EPA ni kuruhusu bidhaa kutotozwa Kodi?
 
Nimesoma na kusema ilkabidi nicheke tuu! Kusema kweli Rais wetu si mwenye tabia ya kusoma vitu hata kidogo! Sitashangaa yeye akisaini kwakuwa kaambiwa! Rais wetu yeye huwa akikutana na mkataba ni kusaini tuu wala sina hakika kama anao muda wa kusoma hata kidogo...
Umeongea ukweli! Rais Samia sio mtu ambae anaweza kusoma jambo na akalichambua ye mwenyewe kwa mapana lakini ata akishauliwa bado ni kazi bure maana naamini uo mkataba alishawahi kuusikia enzi za JPM akiusema hauna maslahi kwetu!

Samia anaamini kwenye Ubepari, Samia anaamini ili taifa liendelee lazima mzungu ashirikianenae direct, Samia atakubali masharti mengi ya ovyo kutoka upande wa Magharibi cos anawatetema pia anawanyenyekea pia.

Naamini yule alietuambia Baba wa Mikata hana kazi kule na sitaki kuamini kama kaendanae maana kwahakika yule hawezi kuukubali ule mkataba.
 
Hii Agreement Rais aliyesoma na kuelewa madhara yake alikuwa Mheshimiwa Mkapa kisha Mheshimiwa Kikwete akamwuunga mkono. Ingefaa tuelezwe Umoja wa Ulaya wamekubali nini sasa ndiyo tunakubali masharti yao. Dosari kubwa ya mkataba uliokuwa unakataliwa ni kwamba Jumuiya ya Ulaya walikuwa wanazembea upande wao wa kutuendeleza katika sekta za uzalishaji, hususan kutoka viwandani.

Pia kuna mpaka fishing hapo, usisahahu EU kuna overfishing na wameshamaliza samaki wao wote sasa wanakuja kuvua kwenye bahari yetu tax free!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom