Rais Samia kuwaongoza Watanzania katika kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha Waziri Mkuu mstaafu Hayati Sokoine

Rais Samia kuwaongoza Watanzania katika kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha Waziri Mkuu mstaafu Hayati Sokoine

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,058
Reaction score
14,382
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kesho, Ijumaa Aprili 12.2024 anatarajia kuwaongoza Watanzania katika kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine

Akizungumza na wanahabari leo, Alhamisi Aprili 11.2024 Monduli juu, Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda amewaomba wananchi wa Arusha kujitokeza kwa wingi ili kushiriki katika maadhimisho hayo

Akimzungumzia Hayati Sokoine, Makonda amemtaja kama mtu aliyekuwa muadilifu na mchapakazi huku akitoa wito kwa Watanzania kumuenzi kwa kufanya kazi kwa bidii na kuwaenzi viongozi waadilifu na wachapakazi wa sasa wenye sifa na uchapakazi wa kufanana na Hayati Sokoine

Makonda amemtaja Hayati Sokoine kama mtumishi mahiri na mwenye ujasiri wa kusukuma gurudumu la maendeleo ya Watanzania bila kuogopa na kuhofia vikwazo mbalimbali

Mkuu wa mkoa huyo ametembelea makazi ya Hayati Sokoine eneo la Enguiki Monduli, kukagua maandalizi ya shughuli ya kesho ya kumbukizi ya miaka 40 tangu kifo cha Hayati Edward Moringe Sokoine aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Hayati Moringe alikuwa Waziri Mkuu mara mbili, tangu tarehe 13 Februari 1977 hadi 7 Novemba 1980, tena tangu tarehe 24 Februari 1983 hadi kifo chake, alipofariki kufuatia ajali ya gari

Uongozi wake unatajwa kuwa wa mfano kwa jinsi alivyokuwa na uadilifu na kufuatilia utendaji kazi huku akikemea ulaji rushwa na ubadhirifu wa mali za umma.
 
Mawazo kama yako sio yanadumaza akili lakini pia uwezo wa kufikiri
Kwamba marais, makamu na mawaziri wakuu waliofariki tuwe tunawafanyia kumbukizi kila mwaka? wewe mpuuzi unaelewa gharama za kumtoa Rais wa Tanzania kutoka Dar/Dom kwenda mikoani? unajua kuna watu wangapi wanalipwa kila siku zaidi ya 250,000 per diem per day miezi miwili kabla ya tukio ajili tu ya kumbukizi ya marehemu ya siku moja? hatuna dawa hosps, madawati, kuna wagonjwa wangapi wanachangiwa na Malisa G wamekosa milioni 3 ya matibabu wamehangaika kwa miaka? shame on you
 
Kesho tutarajie hotuba ya hovyo kutoka kwa RC Arusha
 
NIni kimetokea kwenye familia ya Sokoine hadi selikali nzima iende kuazimisha kumbukumbu ya kifo chake. Nani anayemuenzi sokoine hata kwa mawazo tu. Tusaidizane, nini kimetokea mwaka huu.
 
Yawezekana ni njja ya kuwapoza Wamasai waliofukuzwa Ngorongoro
 
Back
Top Bottom