Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tukio la kushuhudia ufungaji wa lango la handaki mchepuko (diversion tunnel) ili kuruhusu maji kuanza kujaa katika bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere litakalofanyika siku ya Alhamis, 22 Disemba 2022.
Akizungumza na waandishi wa Habari katika eneo la mradi wa umeme wa Mto Rufiji, Waziri wa Nishati, January Makamba amesema mradi huo una hatua kubwa mbili ambazo zina hadhi ya kushuhudiwa, hatua ya kwanza ni kufunga lango la njia ya mchepusho wa maji na ya pili ni kuwasha mitambo ya kufua umeme.
"Kwa jumla hadi leo (Disemba 18, 2022) mradi huu umefikia hatua ya 78%, ni hatua kubwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
“Tumemaliza kujenga tuta, barabara, tumemaliza kujenga nyumba za wafanyakazi kwa hiyo kuna mafanikio katika kipindi chote, sasa tumefikia kwenye mafanikio makubwa tangu tuanze ujenzi wa mradi huu na yenyewe ni kujaza maji kwenye bwawa, kazi ya kujenga handaki la kuchepusha maji ilifanyika miaka mitatu iliyopita na handaki hilo lina urefu wa mita 700 na ujenzi uligharimu Tsh. Bilioni 235.”
Waziri Makamba amesema kutokana na umuhimu wa hatua hiyo ya mradi ulipofikia wakati wa uzinduzi Rais atabonyeza kitufe ambacho kitashusha geti la kuziba handaki lilikuwa linachepusha maji na rasmi maji yataanza kujaa kwenye bwawa.
Ameongeza kuwa Shughuli hiyo itauzuliwa na watu takribani 2,000 wakiwamo viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na viongozi wengine kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mawaziri, Makatibu Wakuu, wakuu wa Mikoa na Wilaya zinazozunguka Bonde la Mto Rufiji, viongozi wa dini, Viongozi wa Chama na Wananchi
Pia Serikali ya Misri ambapo ndipo wanatoka wakandarasi wanaojenga mradi huo, mawaziri, viongozi wa Serikali pamoja na Vyombo vya Habari vya nchi hiyo watahudhuria wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje Nchini Misri.
Akizungumzia faida za mradi huo Makamba amesema ndani ya Serikali mradi huu ni mpana zaidi na utasaidia pia katika masuala ya Kilimo chini ya Mto Rufiji, uvuvi, kuondoa mafuriko, Upatikanaji wa huduma za maji wa uhakika kwa Jiji la Dar es Salaam, Utalii, miundombinu na usafirishaji pamoja na kupata umeme wa uhakika.
Naye Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Maharage Chande ameeleza kuwa inakadiriwa kwamba misimu miwili ya mvua itaweza kufanya bwawa Hilo la Julius Nyerere kujaa maji, hivyo zinatazamiwa mvua za masika Machi 2023 na 2024 kuweza kujaza Bwawa hilo.
Mradi wa kufua umeme kwa njia ya maji wa Julius Nyerere unakadiriwa kuzalisha Megawati 2115, ulianza kujengwa mwaka 2019 na unatarajiwa kukamilika Juni 2024 na umegharimu kiasi cha Shilingi Trilioni 6.5 ukiwa umebakisha 22% kukamilika.
Chanzo: Beatrice Sanga-MAELEZO
PIA SOMA
TUHUMA ZA UFISADI NA HUJUMA
HISTORIA
Akizungumza na waandishi wa Habari katika eneo la mradi wa umeme wa Mto Rufiji, Waziri wa Nishati, January Makamba amesema mradi huo una hatua kubwa mbili ambazo zina hadhi ya kushuhudiwa, hatua ya kwanza ni kufunga lango la njia ya mchepusho wa maji na ya pili ni kuwasha mitambo ya kufua umeme.
“Tumemaliza kujenga tuta, barabara, tumemaliza kujenga nyumba za wafanyakazi kwa hiyo kuna mafanikio katika kipindi chote, sasa tumefikia kwenye mafanikio makubwa tangu tuanze ujenzi wa mradi huu na yenyewe ni kujaza maji kwenye bwawa, kazi ya kujenga handaki la kuchepusha maji ilifanyika miaka mitatu iliyopita na handaki hilo lina urefu wa mita 700 na ujenzi uligharimu Tsh. Bilioni 235.”
Waziri Makamba amesema kutokana na umuhimu wa hatua hiyo ya mradi ulipofikia wakati wa uzinduzi Rais atabonyeza kitufe ambacho kitashusha geti la kuziba handaki lilikuwa linachepusha maji na rasmi maji yataanza kujaa kwenye bwawa.
Ameongeza kuwa Shughuli hiyo itauzuliwa na watu takribani 2,000 wakiwamo viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na viongozi wengine kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mawaziri, Makatibu Wakuu, wakuu wa Mikoa na Wilaya zinazozunguka Bonde la Mto Rufiji, viongozi wa dini, Viongozi wa Chama na Wananchi
Pia Serikali ya Misri ambapo ndipo wanatoka wakandarasi wanaojenga mradi huo, mawaziri, viongozi wa Serikali pamoja na Vyombo vya Habari vya nchi hiyo watahudhuria wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje Nchini Misri.
Akizungumzia faida za mradi huo Makamba amesema ndani ya Serikali mradi huu ni mpana zaidi na utasaidia pia katika masuala ya Kilimo chini ya Mto Rufiji, uvuvi, kuondoa mafuriko, Upatikanaji wa huduma za maji wa uhakika kwa Jiji la Dar es Salaam, Utalii, miundombinu na usafirishaji pamoja na kupata umeme wa uhakika.
Naye Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Maharage Chande ameeleza kuwa inakadiriwa kwamba misimu miwili ya mvua itaweza kufanya bwawa Hilo la Julius Nyerere kujaa maji, hivyo zinatazamiwa mvua za masika Machi 2023 na 2024 kuweza kujaza Bwawa hilo.
Mradi wa kufua umeme kwa njia ya maji wa Julius Nyerere unakadiriwa kuzalisha Megawati 2115, ulianza kujengwa mwaka 2019 na unatarajiwa kukamilika Juni 2024 na umegharimu kiasi cha Shilingi Trilioni 6.5 ukiwa umebakisha 22% kukamilika.
Chanzo: Beatrice Sanga-MAELEZO
PIA SOMA
- Arab Contractors na Elsewedy Electric Kukabidhiwa Rasmi Eneo la Rufiji (PHPP) Kesho
- Arab Contractors wakabidhiwa Billion 688.6 kama malipo ya awali mradi wa umeme wa maporomoko ya mto Rufiji
- Serikali Yakabidhi Eneo La Mradi Wa Umeme Wa Maji Mto Rufiji Kwa Mkandarasi Tayari Kwa Kazi Kuanza
- Rais Magufuli kuzindua mradi wa umeme Mto Rufiji Julai 26, 2019
- SADC yamuunga mkono Rais Dkt Magufuli ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme Rufiji
- Uzinduzi Mradi wa Umeme, mto Rufiji: Rais Magufuli aagiza sehemu ya Selous kuwa Hifadhi ya Taifa
- Mbunge Sospiere Mukweli ameniogopesha kwa kauli yake kuhusu ujenzi wa bwawa la Rufiji; je, kuna haja ya wabunge wote kupimwa akili?
- Mradi wa Kufua Umeme Rufiji (MW 2115) uchimbaji kina cha lango la kuingilia maji kwenye mitambo wakamilika
- Kampuni ya ElSewedy Electric Co inayotengeneza bwawa la umeme Rufiji imewekewa vikwazo, haitaweza kukopesheka nje
- Waziri Makamba: Msitegemee wala kutarajia bwawa la mto Rufiji kujazwa maji mwezi Machi
- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asema Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya mradi wa umeme wa mto Rufiji
- Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere Hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda
- Waziri Makamba: Ujenzi wa tuta kwenye bwawa la mwl Nyerere umekamilika
- Maji katika bwawa la Nyerere kuanza kujazwa 15/11/2021 na 13/04/2022 litakuwa limejaa tayari kwa majaribio
- PM Majaliwa: Bwawa la umeme kukamilika Juni 2022
- Tanesco:- Bwawa la Nyerere litakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2115 hata kama mvua haijanyesha kwa miaka 2
- Waziri Kalemani: Bwawa la Nyerere kujazwa Maji Novemba 15, 2021. Umeme wa maji ni nafuu kuliko wa vyanzo vingine
- Kutokukamilika kwa Mradi wa Umeme Rufiji mwaka 2022 kama ilivyotakiwa na sasa Kukamilika 2024 ni Kumtukana na Kumdhalilisha Hayati Dkt. Magufuli
- Rais Samia kuzindua zoezi la ujazaji maji katika Bwawa la Julius Nyerere, Disemba 22
- Makamba: Ujenzi wa Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere umefikia asilimia 67
- Makamba: Sisi tumeamua kuwa wakweli, bwawa la Nyerere linaisha Juni 2024. Adai tarehe ya mwanzo isingewezekana kwa namna yoyote
- Makamba: Itachukua misimu miwili ya mvua kujaza Bwawa la Nyerere
- Maji yatakayojazwa Bwawa la Nyerere (JNHPP) yanaweza kuzalisha Umeme kwa mwaka mmoja bila kutegemea mvua
- Rais Samia akishiriki shughuli ya kuanza kujaza maji Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), 22/12/2022
- TANESCO: Bwawa la Nyerere halitapunguza bei ya umeme
- Serikali: Mashine ya kwanza ya Kufua Umeme Bwawa la Nyerere itawashwa Mwezi Februari 2024
- Rais Samia: Uzalishaji Umeme Bwawa la Nyerere kuanza Januari 2024
- TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma
- Kamati ya Bunge: Bwawa la Nyerere litakamilika Juni 2024, Tsh. Trilioni 5.85 zimelipwa tayari
- Biteko: Shida ya umeme sasa basi, megawati 235 zimeingia Grid ya Taifa
- Rais Samia: Suluhu ya Umeme itapatikana Aprili 2024 baada ya kuanza uzalishaji wa Megawatt 470-500 katika Bwawa la Mwalimu Nyerere!
- Dotto Biteko: Tumezima mtambo wa bwawa la Mwl Nyerere
- TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma
- Profesa Tibaijuka: Mafuriko ya Rufiji hayajasababishwa na Ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ila limeshindwa kuregulate mafuriko!
- Mtambo wa pili bwawa la Nyerere kuwashwa, kumaliza kabisa mgao wa umeme nchini
TUHUMA ZA UFISADI NA HUJUMA
- Mtaalam: Watanzania mnadanganywa Stiglers Gorge haiwezekani kwani Kina cha Maji Mto Rufiji kinapungua mno
- Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam
- Hotuba ya bajeti Nishati; Miradi ya Rufiji na gesi itaumiza nchi: Mnyika aonya
- Tuambiwe ukweli: Stiglers Gorge inaweza kuwa maafa makubwa kwa taifa badala ya furaha
- Lissu: Serikali na benki hazina uwezo wa kujenga bwawa la Umeme Rufiji
- CAG: Bwawa la Nyerere liliharakiswa
- Polepole: Bwawa la Nyerere ni mradi wa kufa na kupona hatutakubali wahuni wauchezee, Winchi ni kitu kidogo sana!
- Inaumiza sana kuona mradi wa bwawa la Nyerere unahujumiwa wazi wazi
- Unakataje miti milioni 4 ili kujenga la umeme (JNHPP)
- Makamba: Mradi wa JNHPP upo nyuma kwa siku 477 (yaani mwaka na zaidi ya siku 100)
- UFISADI: Mpina aibua tuhuma za upigaji wa Sh. Trilioni 1.5 Bwawa la Nyerere
HISTORIA
- Mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere katika maporomoko ya mto rufiji unaotekelezwa na Serikali uliasisiwa na Baba wa Taifa mwaka 1975
- CAG: Mradi wa Umeme wa Bwawa la Nyerere unatumia upembuzi wa mwaka 1970
- Mhandisi Mkazi, Upembuzi yakinifu wa 1980 unatumika bwawa la JNHPP
- Mwalimu Nyerere aliomba fedha Mradi wa Bwawa la Umeme Rufiji