skilled masala
Senior Member
- May 2, 2019
- 118
- 160
Masala Sayi
Chuo Kikuu cha Iringa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, anatarajia kuwa na ziara ya kikazi nchini Burundi kesho tarehe 16, Julai 2021.
Ziara hiyo imekuja kama mwaliko wa Rais wa Taifa hilo Mh. Evariste Ndayishimiye.Taarifa iliyotolewa na Mkurungezi wa mawasiliano ya Rais ikulu Ndugu, Jaffar Haniu imebainisha kuwa Rais Samia akiwa nchini humo atashiriki shughuli mbali mbali ikiwemo kuhutubia mkutano wa jukwaa la wafanyabiashara wa Burundi na Tanzania.
"Mh. Rais Samia atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Burundi Mh. Rais Evariste Ndayishimiye, kisha atashuhudia utiaji saini wa hati za makubaliano na kungumza na vyombo vya Habari, Mh Rais Samia atahudhuria na kuhutubia Jukwaa la wafanyabiashara wa Burundi na Tanzania kwa lengo la kujadili fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania na Burundi" ilibainisha taarifa hiyo.
Aidha ziara hiyo itakayodumu kwa siku mbili, itakuwa ziara ya nne kwa Rais Samia kufanya nje ya nchi tangu alipo apishwa rasmi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Chuo Kikuu cha Iringa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, anatarajia kuwa na ziara ya kikazi nchini Burundi kesho tarehe 16, Julai 2021.
Ziara hiyo imekuja kama mwaliko wa Rais wa Taifa hilo Mh. Evariste Ndayishimiye.Taarifa iliyotolewa na Mkurungezi wa mawasiliano ya Rais ikulu Ndugu, Jaffar Haniu imebainisha kuwa Rais Samia akiwa nchini humo atashiriki shughuli mbali mbali ikiwemo kuhutubia mkutano wa jukwaa la wafanyabiashara wa Burundi na Tanzania.
"Mh. Rais Samia atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Burundi Mh. Rais Evariste Ndayishimiye, kisha atashuhudia utiaji saini wa hati za makubaliano na kungumza na vyombo vya Habari, Mh Rais Samia atahudhuria na kuhutubia Jukwaa la wafanyabiashara wa Burundi na Tanzania kwa lengo la kujadili fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania na Burundi" ilibainisha taarifa hiyo.
Aidha ziara hiyo itakayodumu kwa siku mbili, itakuwa ziara ya nne kwa Rais Samia kufanya nje ya nchi tangu alipo apishwa rasmi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.