Rais Samia, kwanini 'unatufichaficha' wananchi wako hata tunayotakiwa kuambiwa?

Rais Samia, kwanini 'unatufichaficha' wananchi wako hata tunayotakiwa kuambiwa?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Nasema kwakuwa najua na nimekitumikia ninachokisema. Nimekuwa kiongozi kwenye vyombo vya ulinzi; chamani na serikalini. Najua kuwa yapo mambo ya kusemwa hadharani na yale ya kuhifadhiwa na kumalizwa sirini. Yale ya hadharani ni ya kusakia 'support' kwa wananchi. Wananchi wasikie na waamue...kimaoni.

Kauli fulanifulani za Rais zinapaswa kuwekwa wazi ili kuona wananchi wanachukuliaje maagizo au uamuzi wa Rais. Ni jambo jema kujua mambo hayo kwakuwa nchi hii ni yetu na yote yaliyomo ni kwa ajili yetu. Kama ni jambo la kutufurahisha tuambiwe. Kama ni jambo la kutuchukiza na kutufanya tueleze maoni yetu makalimakali mitandaoni tuambie pia.

Tusifichwefichwe. Na kama imeshaamuliwa tufichwe, tusidokezewe kabisa. Tunapodokezewa, tunaongezea ya kwetu ya uongo na ya kweli. Tunajitengenezea habari za heri na za shari. Si jambo jema. Ni juzi tu Rais Samia umetudokeza kuwa kuna watanzania wenzetu wameweka 'cha juu kwelikweli' kwenye ununuzi wa ndege yetu ya mizigo. Hujatutajia ingawa umewataka watupishe.

Ni akina nani hasa? Wapisheje? Sisi wanatuachaje kama watanzania? Ukasema tena kuwa kuna mfanyabiashara mkubwa mmoja amekopa benki zetu tofauti na kutokomea nje ya nchi. Ni nani? Kwanini hayo yametokea huku vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vikifanya kazi usiku na mchana? Mafumbo huleta mafundo. Kutufumba ni kututaka tuambiane vile tunavyofikiri. Tuwekwe wazi.

Karibu tena Tanzania Kamala Harris, Makamu wa Rais wa Marekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Nasema kwakuwa najua na nimekitumikia ninachokisema. Nimekuwa kiongozi kwenye vyombo vya ulinzi; chamani na serikalini. Najua kuwa yapo mambo ya kusemwa

Unafichuaje mambo ambayo na wewe ni mdau? The best way ni kujifatunatafuna tu huku akijua mijinga anayoongoza inasahau haraka so litapita hilo kama upepo
 
Nasema kwakuwa najua na nimekitumikia ninachokisema. Nimekuwa kiongozi kwenye vyombo vya ulinzi; chamani na serikalini. Najua kuwa yapo mambo ya kusemwa h
Ajiuzulu apishe wenye uwezo wa kukemea na kuchukua hatua.

Jana nilibahatika kuona na kusikia anasema.

Nanukuu

Wanaochota fedha kwenye halmashauri zetu hawashibi Tu.

Nawaza hao anaowazungumzia ni akina nani? Anasubiria mpaka wamuambie wameshiba kuiibia serikali ndio achukue hatua.

Au anataka tufanyaje Sisi. Timiza wajibu wako aache kulia Lia. Haezi akae pembeni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Do not expect anything at all.

The problem is hii Nchi inaongozwa na genge la wahuni pamoja na familia zao ambao wanarithishana kijiti kutoka kizazi kimoja kwenda kingine.
Waliotuibia wanabembelezwa watupishe Sasa kama mtu kaiba mabilion ya dola ataona shida gani kitupisha? Na aingie mwingine Tena kuiba? Na akiiba atupishe? Hizi mahakama za Tanzania ni Kwa ajili ya maskini na wezi wa kuku?

Sent from my RMX2189 using JamiiForums mobile app
 
Harafu tunaambiwa kwamba Kuna wapinzani wanasema nchi iko kwenye uelekeo mzuri,Kwa kua wao wamehakikishiwa maisha yao kua salama,Nchi hii ina viongozi na wananchi wapumbavu mno.
 
Kila mmoja ana jukumu lake na hao wasaidizi wenyewe inaonekana ni majizi tu
Haiwezekani Rais tu ndio ayaone haya
Ofisi karibu zote wanaiba na wakubwa wao wapo na hatusikii watu wamefukuzwa kazi
Ila mpaka PM apite mahali au Rais ndio waanze kuchongeana au kutengeneza drama zao

Hakuna anachoficha ila ni mwendelezo wa matukio yanayotokea kila siku na kila mwaka au tusema tangu tumepewa uhuru tu watu wakaanza kupiga

Nchi masikini kabisa lakini tunajua kuongea tu

Ila majizi duniani yapo sana tu siku hizi na wazungu wamejua bei kupandisha kwa kisingizio cha crisis na matukio yanayotokea

Tutaumia sana ila kundi hilo la majizi yetu ni mtandao mkubwa sana na kila wakipiga wanagawana yaani kama majambazi wamevamia mahali halafu wanagawana

Ila tunaomba Mungu sana waje kugombana kwenye migao
 
Ajiuzulu apishe wenye uwezo wa kukemea na kuchukua hatua.

Jana nilibahatika kuona na kusikia anasema.

Nanukuu

Wanaochota fedha kwenye halmashauri zetu hawashibi Tu.

Nawaza hao anaowazungumzia ni akina nani? Anasubiria mpaka wamuambie wameshiba kuiibia serikali ndio achukue hatua.

Au anataka tufanyaje Sisi. Timiza wajibu wako aache kulia Lia. Haezi akae pembeni

Sent using Jamii Forums mobile app
Pesa kuchotwa halmashauri ni tangu mkapa huko, possibly mwinyi
 
Tofauti ya Magufuli ya Samia ni kwamba magufuli aliweza kutumbua bila kuwaza mara mbili, Samia Ni mpaka ashauriwe na washauri ambao nao ni wapigaji
 
JPM alikuwa anaweka mambo wazi, na alisema kabisa "hakuna mtu mwingine atakayewaambia ukweli, mimi ndio rais nazijua siri zote, na nawaambieni ukweli ndugu zangu".

Hata akitengua uteuzi ilikuwa lazima ukuweke wazi kwanini unakuondoa, tena hadharani.

Inawezekana mama siyo msema kweli mpenzi wa Mungu.
 
yule mhuni aliamua kujilipa ndio maana kakopa kwenye bank za umma, kajilipa ile hasara pale banda la ngozi na pale karibu na Tazara, dah ndio hivyo tena wanasema naye ni mwananchi tumsamehe tu.
 
Mama Samia.
Bora uwafukuze kazi kuliko kuwaacha waliokula pesa za watanzania.
Baadhi ya watanzania wenzetu, wanashinda na kulala njaa kabisa.
Ni dhambi kuiba hela za watanzania hawa maskini.
Hili si la kufumbia macho.
Usiogope chama wala mtu yeyote.
Ukweli ndiye rafiki yako wa milele.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Ajiuzulu apishe wenye uwezo wa kukemea na kuchukua hatua.

Jana nilibahatika kuona na kusikia anasema.

Nanukuu

Wanaochota fedha kwenye halmashauri zetu hawashibi Tu.

Nawaza hao anaowazungumzia ni akina nani? Anasubiria mpaka wamuambie wameshiba kuiibia serikali ndio achukue hatua.

Au anataka tufanyaje Sisi. Timiza wajibu wako aache kulia Lia. Haezi akae pembeni

Sent using Jamii Forums mobile a

Jiwe=satan
 
Back
Top Bottom