Rais Samia: Madiwani na Wenyeviti wa Halmashauri wanachukua Mikopo ya 10% kwa Vikundi Feki

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Your browser is not able to display this video.

Rais Samia amesema Serikali inashughulikia namna itakavyotoa tena Mikopo ya 10% ya Halmashauri kwaajili ya Vikundi ambayo ilisitishwa baada ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2022/23 kuonesha kulikuwa na ubadhirifu mkubwa

Akizungumza wakati akiwaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Dar es Salaam, Rais Samia amesema kuna baadhi ya Watu hawadaiwi Fedha hizo kwasababu ni Watumishi wakiwemo Madiwani na Wenyeviti wa Halmashauri na Wanaounda Vikundi Bandia wanapewa Pesa wakati Vikundi havipo

Rais amesema Fedha hizo zilitengwa kwaajili ya Wananchi lakini zikaanza kutolewa kinyume na taratibu kutokana na baadhi ya Wasimamizi kukosa Uadilifu kwenye majukumu yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…