Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi chetu Samia Suluhu Hasssan, Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika Tamasha la Kitaifa la Utamaduni litakalofanyika Songea.
Tamasha la Tatu la Kitaifa la Utamaduni linatarajiwa kufanyika katika Mji wa Songea, mkoani Ruvuma, kuanzia tarehe 20 hadi 23 Septemba 2024. Lengo kuu la tamasha hili ni kuwakumbusha Watanzania kuhusu umuhimu wa utamaduni wetu na kuuenzi.
Tamasha hilo la siku nne litafunguliwa rasmi na Waziri wa Utamaduni, Sanaa, na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro, huku kilele cha tamasha hilo kikitarajiwa kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kauli mbiu ya tamasha hilo mwaka huu ni “Utamaduni Wetu ni Utu Wetu, Tuuenzi na Kuuendeleza, Kazi Iendelee”, ikisisitiza umuhimu wa kulinda na kuendeleza tamaduni za Kitanzania.
Soma Pia: Magu, Mwanza: Rais Samia ashiriki Tamasha la Utamaduni, Mila na Desturi za Tanzania, atawazwa kuwa Chifu wa Machifu
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili..
Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi chetu Samia Suluhu Hasssan, Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika Tamasha la Kitaifa la Utamaduni litakalofanyika Songea.
Tamasha la Tatu la Kitaifa la Utamaduni linatarajiwa kufanyika katika Mji wa Songea, mkoani Ruvuma, kuanzia tarehe 20 hadi 23 Septemba 2024. Lengo kuu la tamasha hili ni kuwakumbusha Watanzania kuhusu umuhimu wa utamaduni wetu na kuuenzi.
Tamasha hilo la siku nne litafunguliwa rasmi na Waziri wa Utamaduni, Sanaa, na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro, huku kilele cha tamasha hilo kikitarajiwa kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kauli mbiu ya tamasha hilo mwaka huu ni “Utamaduni Wetu ni Utu Wetu, Tuuenzi na Kuuendeleza, Kazi Iendelee”, ikisisitiza umuhimu wa kulinda na kuendeleza tamaduni za Kitanzania.
Soma Pia: Magu, Mwanza: Rais Samia ashiriki Tamasha la Utamaduni, Mila na Desturi za Tanzania, atawazwa kuwa Chifu wa Machifu
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili..