Rais Samia: Mimi ni Mzanzibari

Binafsi ni Mtanzania bara...🤣

Tanganyika tulishaizika ili tuwe na taifa bora zaidi liitwalo Tanzania....

Tanganyika imekwenda ....hairudi ngo'oo ng'ooo ng'ooo........

SIEMPRE SERIKALI MBILI ZA JMT
Mkuu Tanzania Bara ndo taifa gani hilo??
 


Unasema wa2mia simu janja wako zaidi ya 30M, na comments zinazokomentiwa hazifiki elufu kumi,, na kati ya izo 10000 ni baadhi tu wacompenda na kumkejeli, kumkashifu na kumtukana uyu mama.
 

Njombe, Mara, Gairo hakujawahi kutambulika kimataifa. Zanzibar imetambulika kimataifa na mpaka uhuru ilipewa. Kwa hiyo ni vitu havilingani. Lakini lazima tujiulize kwa nini Mzanzibari akijiita Mzanzibari anaonekana msaliti lakini mtu wa Scotland akijiita Scottish au mtu wa Texas akijiita Texan au mtu wa Chechnya akijiita Chechen hawaonekani kama wasaliti wa Uingereza na Marekani na Urusi?
 
Kama uzanzibar sio Dhambi kwanini uchaga, usukuma, uhaya, umakonde, ujita, uzaramo ,unyakyusa iwe Dhambi??????????????.????????!!!!!!!!
Yes yeye ni mzanzibar. Tumuache Mama afanye kazi. Tutamuhukumu kama akifanya yasiyo haki. Unzanzibar wake sio dhambi na wala sio tatizo. Watanzania tunataka usawa na maendeleo. Sio blah blah zisizo kwisha na kuendekeza wizi wa mali ya umma
 
Unasema wa2mia simu janja wako zaidi ya 30M, na comments zinazokomentiwa hazifiki elufu kumi,, na kati ya izo 10000 ni baadhi tu wacompenda na kumkejeli, kumkashifu na kumtukana uyu mama.
Mawazo yako yanachakata mambo kwa kutumia masafa mafupi sana ndugu yangu...

Kwa hiyo kumbe kipimo chako wewe cha watumia social media ni idadi ya comments za humu Jamii Forums...?

Labda nikuulize swali moja dogo sana, kwamba, kwani wewe elimu yako ni ya kidato cha ngapi ndugu?
 
Una matatizo ya akili, Njombe na Gairo hazitambuliki? Anyway Zanzibar sio nchi basi
 
Una matatizo ya akili, Njombe na Gairo hazitambuliki? Anyway Zanzibar sio nchi basi
Iliwahi kutambuliwa lini kama sovereign state? Ndiyo nachokiongelea hicho siyo kutambulika kama sehemu. Zanzibar ilishatambuliwa kama sovereign state.
 
Naona mama ana jaribu kuwajibu sana watu wa mitandao, mi nadhani ange wapotezea hawafiki hata 10% ya watanzania
je WATANGANYIKA mpo mmeyasikia hayo mtajua hamjui vuka ngambo nawe ujitangaze ukirudi uniambie
 
Mnajidharilisha sana kwa tabia hiyo ya kupingapinga hata mambo yasiyo na maana!
 
Watanzania tuna Mambo mengi tena Muhimu tu ya Kufanya na siyo huu Upopoma ( Upuuzi ) wako uliouleta hapa.

Sijaona tatizo kwa Rais kutamka hivyo.
Katiba yetu ina sema Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Serikali zetu ni Serikali ya Maopinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano.

Sasa hakuna shida kusema mia natoka Zanzibar.
Na kaingia kuwa makamo wa Raisi kwa sababu ya Uzanzibari.
 
Tusimung'unye maneno.
Tunayoyaona sasa ni matokeo ya mengine mazuri, lakini mengine mabaya ya Awamu ya 5, chini ya JPM.
Cha kusikitisha ni ukabila uliiendeshwa na JPM.
Alipendelea wazi wazi watu wa kanda ya ziwa, haswa kwao Chato.
Ukupiga line up ya mawaziri enzi yake unakuta mawaziri hadi 8-10 kutoka eneo la kanda ya ziwa, miradi hivyo hivyo.

Mtoto wa dada yake, Doto James, ndiye akawa Katibu Mkuu, Fedha na Paymaster General.

JPM aliunda kundi ka henchmen, wafuasi watiifu kwake, ambalo sasa hata kama ni makosa, linaitwa Sukuma Gang.

Sasa hapo wanapoanza kutumbuliwa, wao ndio wanalia ukabila.

Mama Samia usimtazame nyani usoni, rekebisha mambo tu.
 
Bado kama nchi hatujawahi kupata kiongozi wa kutujengea taasisi imara za mifumo ya uongozi na utawala. Tunaboronga mradi siku ziende.
 
Yupo sahihi kabisa kujiita Mzanzibari, sababu ni nchi inayojitegemea. Kujiita Mtanzania ni sawa na kujiita Mtanganyika. Kwa kuwa serikali ya Tangayika haipo, hivyo serikali ya Tanzania inasimama badala ya Tanganyika, ni sawa angejiita Mtanganyika, ambaye kwa Mzanzibari sio sahihi.
 
Wewe ni namna gani? Amesema yeye ni mzanzibari, unajua kuwa hakuna kabila mzanzibari? Wazanzibari wote wana makabila mbali mbali, sasa kosa lipo wapi kwa alichosema?
 
Mara ngapi mwenda zake alijisema yeye ni msukuma?. Huyu mama kasema utaifa wake hakusema kabila lake. Hivo tanzania ni nchi mbili. Tanganyika na Zanzibar. Wazanzibari watabaki kuwa wazanzibari. Na Nyinyi tafuteni nchi yenu inaitwaje. Kila mtu ana kabila lake.
 
Katiba yetu ina sema Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Serikali zetu ni Serikali ya Maopinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano.

Sasa hakuna shida kusema mia natoka Zanzibar.
Na kaingia kuwa makamo wa Raisi kwa sababu ya Uzanzibari.
Na kusema ukweli, wala hakuwa na maana ya kujitambulisha kwamba yeye ni mtu wa tofauti na watanzania. Alitumia mfano tu na akaeleza why is not good kuanza ukabila usiokuwa na mashiko.

Watanzania hatujadili mambo ya msingi tunakuwa knity picky tu bila objectivity.

Tujifunze kuwa critical yes but with substances siyo hizi cheap politics...

Watu wetu hawajifunzi good citizenry ambayo ni ya msingi sana kwenye maendeleo ya nchi yeyote
 
Hana kabila, lakini ni mdini mzuri.
Ni afadhali we mdini kuliko kuwa mlughalugha...Mtu yeyote mdini anamwogopa Mungu, hiyo ni njema sana against aliye mlugha lugha yeye hata kama lugha yake haina msingi anataka tu ndiyo ipewe nafasi...

I love leaders wakiwa wa dini maana atleast wanaye wanaomwogopa kwenyw subconscious zao
 
Tena hadi kukiongea alikiongea hadharani, ila wakati huo hatukuwa na shida wapendwa wake....I love JPM mpaka nakuaga biased lakini kwa hilo la ukabili japo yeye hakuwa ki hivyo watu hao hao dhaifu walimtumia kwa faida binafsi badala ya maslahi mapana ya taifa letu na watu wa aina hiyo hiyo bado wanaendelea kutugawanya mpaka sasa.

I understood JPM, alikuwa anatafuta support na akaona group kubwa ni hilo na kwasababu kweli asingekuwa na hiyo support angeogopa kufanya baadhi ya maamuzi...He was pro nchi...What about the rest of us ambao some ni wafaidika wakubwa mbona baada ya yeye kuondoka tukaukana hata hiyo consortium ambayo haikuwa rasmi?

Tanzanians stop being naive...Mtu yeyote asiyeweza ku negotiate anaye jaribu ku rule kwa ku divide ni coward na wala hana leadership skills na wengi wanaogopa sana meritocracy!

Watu wa jinsi hiyo hiyo ndiyo ambao kwa sasa wanakuja na tohozi kama sukuma gang, last time ilikuwa wakaskazini hawatakiwi...Ukichunguza, these are the very same people, ambao kwa miaka mingi wameonyesha mediocrity kwenye leadership ya nchi hii...Next time itakuwa group lingine just to make themselves relevant...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…