Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza umemtupia zigo la lawama? Elewa tu watu wanaamini ana baraka zako

Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza umemtupia zigo la lawama? Elewa tu watu wanaamini ana baraka zako

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Eti amri ya mkuu wa mkoa imekuwa sheria!

Screenshot_20210721-103649_Twitter.jpg
 
Hakuna namna CCM itatawala nchi bila kutumia nguvu, haina njia mbala ya kuitawala nchi kwa sasa,kwa sababu hawana hoja za kisiasa za kuituliza nchi,kwani kuna uongo gani haujasemwa na CCM? hawana uongo mpya ndugu zangu! hata akishuka malaika aingie CCM lazima atumie nguvu kutawala maana hatakuwa na jipya na hii ndio inathibitisha kuwa mwisho wa njia uko karibu.
 
Mama alisema "ukinizingua nakuzingua"
Yaani aiseee, mie nilipoona ile hotuba aliyoitoa Mama njiani Morogoro na kuwaonya wananchi kwamba' wasijejikuta wakaingizwa mkenge'.. basi nikajuwa tu yale matazamio chanya aliyowapa mwanzoni, sasa kibao kimegeuka na inabidi wawe wapole tu....... kazi iendelee.
 
Eti amri ya mkuu wa mkoa imekuwa sheria!

View attachment 1861956
Huku mbowe anasema kuna korona..mara chanjo iwe lazima..kisha anawaita watu wakusanyike..hizi beer zilizoshushwaa bei zinawaharibu viongozi wa chadema..how comes unasema kuna korona na unawakusanya watu!!
Haihitaji akili kubwa kuwatambua wapinzani wa tz..yaan ni wajinga zaidi ya ujinga wenyewe.
 
Of course, LAZIMA atakuwa na baraka za rais directly or indirectly! Lau kama asingekuwa na hizo baraka, hivi sasa ingekuwa ameshatoa agizo la watu wao kuachiwa mara moja!!

Ninachoona haya ni maagizo ya rais moja kwa moja! Na hata kama rais hakuagiza moja kwa moja, kufumbia macho matendo ya kishenzi kama hayainakuwa anatoa ujumbe kwa polisi kwamba waendelee kukamata raia wasio na hatia!

Na hapa kuna tatizo lingine... insecurity!!

Kwa kawaida, baadhi ya wanawake wakipata madaraka huwa wanasumbuliwa sana na hili suala! Katika hili, baadhi yao, tena kwa wingi tu hudhani jambo fulani linafanywa dhidi ya mamlaka yao kwa sababu wanaofanya wanamdharau kwa kumuona yeye ni mwanamke tu!!

Mtu anapokuwa na mawazo mabovu kama hayo, mara nyingi hufanya maamuzi ya ovyo kama defensive mechanism ya kutaka ku-prove "she's tough"!

Sijui ni lini Mwenyezi Mungu atatuondolea Janga la CCM na Watu wake!!!
 
Yaani aiseee, mie nilipoona ile hotuba aliyoitoa Mama njiani Morogoro na kuwaonya wananchi kwamba' wasijejikuta wakaingizwa mkenge'.. basi nikajuwa tu yale matazamio chanya aliyowapa mwanzoni, sasa kibao kimegeuka na inabidi wawe wapole tu....... kazi iendelee.
Njia aliyoitumia Mbowe haikuwa muafaka wa kutoa kauli kama zile. Rais alionyesha kuwa licha ya kwamba alikuwa ni msaidizi wa aliyepita lakini kuna mambo alikuwa hafurahishwi nayo kwa kuwa mamlaka hakuwa nayo ilibaki kuwa kama ilivyokuwa ijapokuwa CCM bado ni CCM.

Kawatoa watu magerezani na kuwafutia kesi wakiwemo wapinzani. Wafanyabiashara ile task force iliyokuwa ikitumika kuchukua kodi ameivunja vunja na mengineyo tofauti tofauti. Ubabe wa viongozi kwa kiasi fulani umepungua na Uhuru kwa kiasi chake umerudi.

Sasa ni nini kilichomfanya Mbowe na Chadema kutoa kauli kali za namna ile? Kisa kuambiwa nipeni muda? Kwa nchi yetu ilivyokuwa ilikuwa inahitaji kushtuka Rais aliposema nipeni muda?
 
Chama Cha Mapinduzi Ni kioga Sana.

CCM wakisikia neno katiba mpya wanakonda Sana kwa mawazo.

Wanajua fika katiba mpya itaweka usawa wa kila kitu.

Na CCM usawa wa kila kitu ndo hawataki kwa sababu siku zote huwa wanaingia madarakani kwa unyang'anyi.
Mfano Ni huu uchaguzi uliopita.

Wakiruhusu katiba mpya maana yake wameruhusu tume yenye usawa,na tume yenye usawa maana yake CCM kwa heri.

Hofu imewatawala hawana namna nyingine Ni kuzuia mikutano ya kudai katiba mpya.

CCM Ni waoga Sana,pamoja na kuwatumia TISS JW PT na wengine kama hawa lakini hawajiamini.

CCM Ni waoga na waongo,wanajinasibu kuwa wanashindaga kwa kishindo maana yake wanapendwa.Sasa kama wanapendwa wanaogopa Nini kuruhusu kelele za hao wanaoitwa wachache ili waendelee kuwashinda na wakose Cha kusema?
Wajisifu kuwa waliomba katiba mpya tumewapa na uchaguzi tumewashinda.wanaogopa Nini sasa?
CCM Ni waoga sana,kwa hofu hii ya kudai katiba mpya,presha zikizidi mnaweza kuwakuta CCM wote wamekufa kwa usiku mmoja tu.
Ni waoga hatari.
 
Back
Top Bottom