Rais Samia na awamu ya pili ujenzi wa sekondari za kata zote nchini

Rais Samia na awamu ya pili ujenzi wa sekondari za kata zote nchini

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Deogratius Ndejembi,
amesema serikali imedhamiria kujenga shule za sekondari katika kata zote nchini awamu ya pili.

Alisema shule hizo zitajengwa katika halmashauri zote 184 nchini na kila halmashauri itapata shule moja.
Ndejembi alisema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la Maimuna Mtanda (Viti Maalumu).
aliyetaka kujua ni lini serikali itajenga shule za sekondari katika kata ambazo wanafunzi wake wanatembea umbali
mrefu, akitolea mfano Chilangala na Mukomatu zilizopo Jimbo la Newala Mjini.

Aidha, katika swali la pili, alitaka kujua mkakati wa serikali wa kupeleka walimu katika shule hizo. Akijibu maswali hayo, Ndejembi alisema dhamira ya serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu ni kujenga shule katika kata zote nchini.

"Niwatoe shaka waheshimiwa wabunge kwamba, serikali imedhamiria kwenda katika awamu ya pili ya kujenga shule hizi katika kata, muda siyo mrefu, mtaanza kuona zikijengwa katika halmashauri zote 184 katika nchi yetu, kila halmashauri itapata walau shule moja katika awamu ya pili,"alisema.

Ndejembi akijibu swali la pili la mbunge huyo, alisema serikali imetangaza ajira 21, 200 kuajiri walimu na watumishi wa sekta ya afya. Alisema ajira hizo zitaziba mapengo ya walimu ambao wanahitajika katikamaeneo hayo.

Akijibu swali la msingi la Anastazia Wambura (Viti Maalumu), aliyetaka kujua shule ngapi za sekondari zimejengewa katika Mkoa wa Mtwara ambao una zaidi ya kata 50 ambazo hazina shule.

Ndejembi akijibu swali hilo, alisema mradi serikali kupitia mradi wa kuboresha elimu ya sekondari, imejenga shule 231 za kata na shule 10 za wasichana za kitaifa katika mikoa 10. Kwa mujibu wa Ndejembi, hiyo ni awamu ya kwanza ya ujenzi kupitia mradi wa kuboresha elimu ya sekondari ambapo tayari Mkoa wa Mtwara umeshajengewa shule 10 za kata katika maeneo yenye msongamano mkubwa wa wanafunzi
 
Mshaurini waziri wa Tamisemi na Mkulu, wasiishie kujenga majengo kila kata na hakuna vitabu vya kiada na ziada ili kujifunza kuwezekane. Elimu ili ikamilike lazima kuwe na walimu wa kutosha a mazingira mazuri ya walimu kuishi ya walimu.

Kama uwoano wa Mwl kwa wafanafunzi ni 1:100 na hamna vitabu, walimu hana nyumba karibu, hakuna huduma za kibinadamu kwa walimu;

Jitihada za kujenga majengo bila vitabu, maabara zenye vifaa na technicians wa lab;
Shule zitakuwa eneo la watoto kwenda kukua miaka minne na sio sehemu ya ku-reinforce behavioural change.

Je, ujenzi huu utaendana na kasi ya kuandaa walimu wa kutosha na bajeti yao ya mishahara na maslahi mengine kazini??
 
Shule za kata kwa ajili ya nini tena? Maana zilizopo tayari zinatosha. Kinachotakiwa kwa sasa ni serikali kuboresha miundombinu ya hizo shule! Mfano ujenzi wa mabweni (hosteli), ujenzi wa nyumba za walimu, maabara, nk!

Baada ya hapo serikali ingejenga sasa vyuo vya ufundi kila kata nchini, ili kuwasaidia wale watoto wasiopenda kukariri masomo ya sekondari (halafu jamii inawaona hawana akili) kuweza kujifunza elimu ya ufundi stadi, ujasiriamali, michezo, nk. Kwa faida yao ya baadaye.
 
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Deogratius Ndejembi,
amesema serikali imedhamiria kujenga shule za sekondari katika kata zote nchini awamu ya pili.
o tayari Mkoa wa Mtwara umeshajengewa shule 10 za kata katika maeneo yenye msongamano mkubwa wa wanafunzi
Shule nyingi ubora sifuri,ni bora vyuo vya veta tu,watoto wanatoka moja kwa moja wanataaluma,sio kukariri sentence za mkoloni
 
Shule za kata kwa ajili ya nini tena? Maana zilizopo tayari zinatosha. Kinachotakiwa kwa sasa ni serikali kuboresha miundombinu ya hizo shule! Mfano ujenzi wa mabweni (hosteli), ujenzi wa nyumba za walimu, maabara, nk!

Baada ya hapo serikali ingejenga sasa vyuo vya ufundi kila kata nchini, ili kuwasaidia wale watoto wasiopenda kukariri masomo ya sekondari (halafu jamii inawaona hawana akili) kuweza kujifunza elimu ya ufundi stadi, ujasiriamali, michezo, nk. Kwa faida yao ya baadaye.
Shule hazitoshi mkuu,mpango ni kuifanya elimu ya sekondari kuwa ya lazima kwa wote,tuna vijana wangapi wanaotakiwa kuwa sekondari(14-19 yrs)?!
 
Shule nyingi ubora sifuri,ni bora vyuo vya veta tu,watoto wanatoka moja kwa moja wanataaluma,sio kukariri sentence za mkoloni
Tukubaliane kwamba huu ni mtizamo wako tu
 
Shule hazitoshi mkuu,mpango ni kuifanya elimu ya sekondari kuwa ya lazima kwa wote,tuna vijana wangapi wanaotakiwa kuwa sekondari(14-19 yrs)?!
Mimi ninachoelewa mpaka sasa, hizi shule za sekondari za kata, kwa sehemu kubwa zinatumika kukuzia tu watoto! Ila siyo kutoa elimu bora ya kumsaidia mtoto katika maisha yake.

Hivyo badala ya kuwapotezea watoto muda wao, serikali ingewekeza sasa kwenye elimu ya ufundi stadi, ujasiriamali, nk. kwa kujenga vyuo vya VETA kila kata nchini, ili kutengeneza Taifa la watu wanao jitegemea, na wenye ujuzi baada ya kuhitimu masomo yao.

Wanafunzi wachache wenye ufaulu wa juu, ndiyo wapelekwe sekondari (ambako miundombinu yake itakuwa imeboreshwa, kama nilivyo elezea hapo juu).
 
Mimi ninachoelewa mpaka sasa, hizi shule za sekondari za kata, kwa sehemu kubwa zinatumika kukuzia tu watoto! Ila siyo kutoa elimu bora ya kumsaidia mtoto katika maisha yake...
Elimu ya o level ni muhimu,ni basic,yapaswa mtu kuwa nayo,wakati wa jakaya watu wakipinga shule za kata kwamba elimu duni na hakuna walimu,Leo nyingi tu zinafsnya vizuri
 
Elimu ya o level ni muhimu,ni basic,yapaswa mtu kuwa nayo,wakati wa jakaya watu wakipinga shule za kata kwamba elimu duni na hakuna walimu,Leo nyingi tu zinafsnya vizuri
Kufanya vizuri kwa baadhi ya hizo shule bado hakuwasaidii watoto wengi ambao baada ya kumaliza masomo yao, hurejea mtaani na kugeuka kuwa wazurulaji, makahaba, nk.

Kwa mtazamo wangu, ni bora serikali ingewekeza sasa kwenye ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi kwenye kila kata nchini! Badala ya hizo shule.
 
Back
Top Bottom