Rais Samia na Hayati Magufuli ni Marais wa mfano Afrika utekelezaji wa Miradi

Chunguza vizuri, kuna marais wanatwlekeza miradi mizito zaidi, tofauti ni hawaongei wala kujipigia chapuo. Africa ni kubwa na ina marais wengi, zunguka tena uje uandike hapa
Hili jukumu unapaswa ulifanye wewe kwa maana unaonekana una uhaba wa taarifa.
 
MBEYA Barabara zimesimama Wewe unaongea pumba tuuu
 
Msaidie Raisi wako kama una Akili TIMAMU ajue changamoto kubwa zinazowakabili watu wake kwa sasa na usiwe mbinafsi wa mawazo,chakula umnyime lkn mawazo mpe na ninakutuma kwa sababu mm si mbinafsi na mnafiki kama wewe umwambie Raisi SAMIA kuwa ana maadui wengi sana ndani ya CCM kuliko eneo lolote ndani ya TANZANIA.
 
Kua na maadui kisiasa ni jambo la kawaida hata yeye analijua.
 
Kwani jpm alitekeleza mradi gani. Leta mfano hata mmoja tu
Barabara nyingi kuu na za mitaani,bandari ya Dar phrase no.1-7,majenga kadhaa ya mahakama na mengine ya serikali n.k.
Tungekuwa naye,SGR ingekuwa imefika mwanza.bwawa la umeme lingekamilika 100% [siku nyingi]na tungepata umeme kwa bei nafuu,daraja la busisi lingekamilika 100%, hatimaye TZ.ingekuwa kimbilio la wageni, tungekuwa na maisha Bora huku tukifurahia kuwa waTz.na siyo jehanam tunayoiishi sasa hivi chini ya ufalme wa kishetani ccm.
 
Kutekana na kuua je. Au umesahau
 
Jaman mtakuja kujua hamjui, sipendi unafiki kwa kweli, ila huyu mama yenu hafai kwa kweli, RIP Magufuli ingawa ulikosea kitu kimoja cha kuua upinzani lakini ulipendwa na watu wengi kutoka ndani ya mioyo yao.
 
Jaman mtakuja kujua hamjui, sipendi unafiki kwa kweli, ila huyu mama yenu hafai kwa kweli, RIP Magufuli ingawa ulikosea kitu kimoja cha kuua upinzani lakini ulipendwa na watu wengi kutoka ndani ya mioyo yao.
Nani alimpenda magufuli zaidi yako. Yule kaua biashara zote tukaishi kama digidigi
 
Sisi tuliiuliwa bishara zetu hatuwezi kumkumbuka mbwa yule. Mama kafuafua biashara zote
Wewe na nani? Alitaka kutuleta pamoja kuondoa utabaka, RIP Magufuli, mimi sio mwanasiasa ila utawala wake ulinikosha. Huwezi kumpendeza kila mtu ila kwa sasa hv ndio too much. Iko siku mtamkumbuka hadi wewe uliyeuliwa biashara yako,. Unakizazi nacho kinategemea rasilimali zetu, utaelewa siku moja
 
Kuondoa tabaka kwa kuwafilisi watu huo ndo ujinga wenyewe. We kama hufanyi kazi baki na umaskini wako usitake wote tufanane kuwaza. Ndoto ya maskini kama nyie ni kuona tajiri anshuka ili mfanane. Kilichowatesa kipindi kile ni wivu dhidi ya wanaofanya kazi kwa bidii
 
Kazi nafanya na nimesoma vzr saaana, haiwezekani ufilisiwe tuu bila sababu yamkini kuna namna unafanya sasa ukadhibitiwa ndio unaona unafilisiwa, ninachoamini ww unalipa kodi kubwa kuliko mimi sasa kwa nini ufilisiwe??? Wale wote waliokuwa wanafanya biashara za magendo au za janjajanja ndio walimchukia ukiwapo wewe ila kama ungekuwa unafanya biashara kwa kufuata utaratibu wala usingechukia,
 
Ndo umuulize sasa jpm kwa nini alofilisi kila mfanya biashara. Jibu ni moja tu hakutaka mtu wa kumchalenge katika utawala wake wa kidictator. Maskini hata simu moja hana nguvu ya kuchallenge chochote. Kila kitu kwake ni sawa. Ndo mana hata uhuru wa habari akaupiga teke ili aonggoze anavyotaka yeye siyo katiba inavyotaka
 


Africa kuna watawala wa aina yake .

Yaani hata ukifika Somalia utasikia tutunze amani yetu.

Sudani napo tutunze amani yetu .🤣🤣🤣🤣🤣
Burundi napo tutunze amani yetu 🤣🤣🤣.

Nimekuja kugundua kuwa wanazungumzia amani yao na familia zao.

Hata maendeleo ya viwanda au miradi ya serikali mingi ni ile ya kwao na familia zao.

Watanunua malori yao na mabasi yao halafu watanunua unifomu za trafiki zenye kamera ili magari yao yasiguswe badala ya kuweka kamera barabarani kudhibiti madereva wazembe na pia kudhibiti uhalifu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…