Rais Samia nakukumbusha kuwa siku hazigandi, zayoyoma. Samaki mkunje angali mbichi, akikauka hakunjiki

Rais Samia nakukumbusha kuwa siku hazigandi, zayoyoma. Samaki mkunje angali mbichi, akikauka hakunjiki

Hii ya sasa ina matobo mengi yanayoruhusu kuvunjwa ikiwa ni pamoja na mahakama kuwa na kigugumizi inapotakiwa itoe haki dhidi ya Kiongozi wa mhimili mwingine ndio maana jobo anafanya anavyotaka kwa sababu anafahamu hakuna yeyote anayeweza kumwajibisha.

Katiba yenyewe ya Sasa bado inavunjwa tu na viongozi wengine Kama spika ndugai.Sijui mpy ya nn.Waafrika tujifunze kwanza kuheshimu Sheria na katiba yetu.
 
IMG-20210507-WA0106.jpg
 
Iliyopo ina matobo mengi yanoyoruhusu kuvunjwa. Katiba Mpya itaondoa ubunge wa viti maalum na wa kuteuliwa.

Cc Mag3 wewe Mag 3 kwanini unang’angania katiba mpya wakati iliopo inavunjwa na supika kama alivyosema mtoa mada au wewe unapenda nguo mpya tuu?
 
Nadhani mimi na wewe ni moja ya watu wanaopingana sana

Mara nyingi tunataka kitu kimoja ila kwa mitazamo tofauti

JPM pamoja na kujipendekeza sana CCM, na kuwapa vyeo vya ubunge..lakini kimoja cha maumivu makubwa ni kuziba mianya ya CCM kila nchi hii...hata kama hakufanikiwa

CCM wamempoteza na kummaliza huyu, na wengi walijua 2 years back, yule mnayesema mwendazake, nduli , dikteta ali wa screw zaidi CCM.

Mama Samia alikupaje faraja? wakati hata yeye ndani ya masaa 48 angeweza kutokuwa Rais ni kuwa kapewa chukua ila sio kwa mtazamo huo wenu. Mkuu wa majeshi hakuwa mjinga kusema tutakuheshimu wewe Rais, hii itaongelewa vyema sana baadae

CCM halisi hao unaowaita wadhalimu, haswaaa ndio wamerudi na wanatamalaki. Trust me. Kama corruption ndio inaanza

Samia alitakiwa aseme mazuri yote ambayo dunia nzima na watanzania ataonyesha utofauti na JPM atawale kwa amani

Kwani CCM wana shida na kuongea? au demokrasia, watawapa wapinzani viti 30, wapinzani watakuwa wenyeviti wa kamati za bunge.

CCM watateua baadhi ya wapinzani kuwa wakuu wa taasisi au mawaziri, tujenge taifa, hii lengo ni KULA vizuri na kusahaulishwa kwenye katiba na Tume huru, Tume huru wataendelea kutoa ubunge kwa wapinzani kwa order maalumu.

JPM hakuwa mnafiki na zaidi hizi za kudanganya Taifa na ushamba wake alinyoosha na kuonyesha weakness ni katiba mpya na tume huru.

Kila kizuri ambacho watu walikitaka watakipata, ila sio katiba mpya au tume huru. kwa CCM ya sasa ambayo ina NJAA kali sana.

Kosa la JPM ni kuruhusu baadhi ya watu wake kuwa wababe, na yeye kushindwa kuchukua hatua.Kosa lake ni kuweka wapinzani mbali sana ambao matokeo ya 2015 na reaction ya upinzani ya kebehi, matusi na dharau..angeweza kuvimeza tu na akakaa nao kushirikiana nao, zile kejeli akazichukulia personal.

Lakini kama kuumiza CCM na kukata mirija yao...The man did so very well...hata kama wako walifungua mirija mipya ambayo hakuifahamu

Kama kuna kichaa angeweza kubadili katiba kwa kishindo na kwa manufaa ya Taifa, bado angekuwa JPM pia..kwa caliber yake angeweza.

Kwa mama, tuandae post nyingi sana
 
Looo, nilikuona mahala nikadhani una kiasi cha uelewa wa mambo, kumbe uko hivi? Wewe bado ni mwanafunzi wa sekondari?
Kwa nini usitumie muda wako humu ukisoma na kujifunza namna ya kujadili hoja.
Umesoma yaliyoandikwa kwenye mada?
Sasa haya yanahusikaje na mada inayojadiliwa hapa! Unafanya udharaulike bure.
Ndugu yangu Kalamu, pole sana na hilo lisikushangaze. JF imekuwa kama kokoro...humo ndani utakuta hadi vyura na kono kono kwani kokoro inazoa tu kila itakachokutanan nacho. Kinachotakiwa kwa sasa ni uvumilivu tu kwani hata mods wanaonekana wamechoka.
 
Rais wetu Mh. Samia Suluhu Hassan, ada ya mja hunena, mwungwana ni kitendo na siku njema huonekana asubuhi.
Wewe ni Rais wetu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliyoapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea.
Kupitia hiyo Katiba sisi wananchi tuliamua rasmi na kwa dhati kujenga jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani.

Mh. Rais, tarehe 29 Machi, 2021 uliapishwa kuliongoza Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar-es-Salaam.
Leo tarehe 9 Mei, 2021 ni siku ya arobaini toka ulipoapishwa na kuwa Kiongozi Mkuu wa taifa hili lenye watu karibia milioni sitini (60,000,000!)
Kama kiongozi matendo yako ni lazima yalete faraja na matumaini kwa Watanzania wote na kuhamasisha zaidi ushiriki wao katika hatma ya taifa.

Pamoja na kuapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea Katiba, epukana kabisa na matendo yanayoweza kutafsiriwa kwamba yanapingana na Katiba.
Mh. Rais kumbuka kauli huumba hivyo epukana pia na zile kauli ambazo zinaweza kutafsiriwa na wasaidizi wako kama ruhusa ya kuvunja Katiba.
Hali hii inahusu hasa yale maagizo yanayotolewa papo kwa papo bila kupima yatakavyopokelewa na watendaji wakuu wa vyombo vya dola.

Mh. Rais tuko wengi ambao kuapishwa kwako kulitupa japo faraja kutokana na mizengwe ya awali iliyokuwa ikifanywa na mahafidhina.
Amini usiamini asilimia kubwa ya wananchi bila kujali tofauti zao walipokea mabadiliko ya uongozi wa juu kabisa wa nchi kwa matumaini.
Yawezekana walisukumwa na sababu mbali mbali lakini lililowaunganisha ni uhitaji wa hewa safi kupitia dirisha ambalo ujio wako ungewafungulia.

Ni hilo dirisha lingewezesha kiapo chako kiwe na maana kwa kuturudisha kwenye utawala wa sheria unaoheshimu, kulinda na kutetea Katiba
Ingawa wengi tulikupokea bila kujali unatoka miongoni mwa watu wale wale na chama kile kile, tuliguna kidogo uliposema kazi iendelee...!
Kiongozi bora hafuati tu nyayo za aliyemtangulia, hapana, huyo si kiongozi bora, ni mfuasi...kiongozi bora huvumbua njia salama wapite anaowaongoza.

Tafadhali Mh. Rais, acha kupaka ukuta rangi nyumba ipendeze huku msingi una nyufa; shughulikia kwanza msingi nyumba iwe imara na salama!
Tunayo Katiba ya mwaka 1977 lakini cha ajabu ni kuwa hata hii. pamoja na mapungufu yake, tunashindwa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea!
Tunayo Rasimu ya Warioba lakini kwa Mh. Samia Suluhu Hassan, hata kuitaja tu imekuwa shida, shida ni nini? Je kuku wetu anataga kwenye miba?

Mwanga uliojitokeza unaanza kufifia ghafla huku safari hatujafika hata nusu, je kulikoni? Chukua hatua, katika kuidai Katiba mpya sahau suluhu!
Shughulikia sheria zote ambazo zinaisigina Katiba kwa namna moja au nyingine kwani tuna kiu kubwa ya utawala unaozingatia haki na usawa.
Ngoja Ngoja yaumiza matumbo na linalowezekana leo lisingojee kesho; kwa kweli baada ya miaka minne ya giza uvumilivu uko mashakani
Mkuu mada kama hii ndio nilitarajia ije hapa ubaoni kitambo. Hili ndilo linalopaswa kujadiliwa na si zile ngonjera nyingine ambazo haziwezi kutuvusha wala kutatua matatizo tuliyonayo zaidi ya kuchangamsha baraza na kujiliwaza kwa mapumbazo hewa. Tuna matatizo mengi yanayotokana na ombwe la katiba huku sheria kandamizi na baadhi ya viongozi wasiofaa wakitumia mamlaka na madaraka waliyopewa vibaya lakini hakuna namna ya kuwawajibisha wakiwa ofisini au wakitoka nje ya ofisi labda iwe hivyo kwa baraka ya Mkuu wa nchi!! Zipo haki ambazo si hisani kupewa lakini tunalazimika kuziomba haki zile na wakati mwingine hazipatikani na hakuna anayejali... wako wanaohujumu miradi wakiwa katika ofisi za umma, wako wanaowahujumu wananchi na kuwakandamiza wakitumia nafasi zao, wako ambao kwa madaraka yao wanaamua kupora haki za wengine kisha kuwasemea kana kwamba wao ndio sheria yenyewe...
Wako ambao hawathamini walipa kodi (ama viingilio michezoni) wanapodai haki zao badala ya kushughulika na chanzo cha tatizo (intelijensia inafeli wapi!?) Anahukumiwa aliyetendwa kwa virungu na mabomu ya machozi kana kwamba mlipaji ndiye aliyekosea!!!? Na kama haitoshi MWISHO WA SIKU HUTOLEWA KAULI NYEPESI NYEPESI KUFUNIKA KOMBE... Wanajua "yatapita wananchi watasahau!!!" Je hii ndio Tanzania tuitakayo?
AHSANTE SANA.
 
Nadhani mimi na wewe ni moja ya watu wanaopingana sana

Mara nyingi tunataka kitu kimoja ila kwa mitazamo tofauti

JPM pamoja na kujipendekeza sana CCM, na kuwapa vyeo vya ubunge..lakini kimoja cha maumivu makubwa ni kuziba mianya ya CCM kila nchi hii...hata kama hakufanikiwa

CCM wamempoteza na kummaliza huyu, na wengi walijua 2 years back, yule mnayesema mwendazake, nduli , dikteta ali wa screw zaidi CCM.....

Mama Samia alikupaje faraja? wakati hata yeye ndani ya masaa 48 angeweza kutokuwa Rais!!!...ni kuwa kapewa chukua ila sio kwa mtazamo huo wenu...Mkuu wa majeshi hakuwa mjinga kusema tutakuheshimu wewe Rais....hii itaongelewa vyema sana baadae


CCM halisi hao unaowaita wadhalimu, haswaaa ndio wamerudi na wanatamalaki....trust me.Kama corruption ndio inaanza

Samia alitakiwa aseme mazuri yote ambayo dunia nzima na watanzania ataonyesha utofauti na JPM....atawale kwa amani

Kwani CCM wana shida na kuongea? au demokrasia...watawapa wapinzani viti 30...wapinzani watakuwa wenyeviti wa kamati za bunge...

CCM watateua baadhi ya wapinzani kuwa wakuu wa taasisi au mawaziri....tujenge taifa...hii lengo ni KULA vizuri.... na kusahaulishwa kwenye katiba na Tume huru, Tume huru wataendelea kutoa ubunge kwa wapinzani kwa order maalumu..

JPM hakuwa mnafiki na zaidi hizi za kudanganya Taifa....na ushamba wake .. .alinyoosha na kuonyesha weakness ni katiba mpya na tume huru.



Kila kizuri ambacho watu walikitaka watakipata ...ila sio katiba mpya au tume huru. kwa CCM ya sasa ambayo ina NJAA kali sana...

Kosa la JPM ni kuruhusu baadhi ya watu wake kuwa wababe, na yeye kushindwa kuchukua hatua.Kosa lake ni kuweka wapinzani mbali sana ...ambao matokeo ya 2015 na reaction ya upinzani ya kebehi, matusi na dharau..angeweza kuvimeza tu na akakaa nao kushirikiana nao...zile kejeli akazichukulia personal...

Lakini kama kuumiza CCM na kukata mirija yao...The man did so very well...hata kama wako walifungua mirija mipya ambayo hakuifahamu

Kama kuna kichaa angeweza kubadili katiba kwa kishindo na kwa manufaa ya Taifa, bado angekuwa JPM pia..kwa caliber yake angeweza.

Kwa mama, tuandae post nyingi sana
Pana hoja za msingi kwenye hili Mkuu kwa watakaoelewa na waelewe...
 
Nadhani mimi na wewe ni moja ya watu wanaopingana sana
Mara nyingi tunataka kitu kimoja ila kwa mitazamo tofauti
Hapana, mimi na wewe ni kama mbingu na ardhi. Unayoyaamini na kuyatetea toka nikufahamu humu JF hatujawahi kutaka vitu vinavyofanana ila kwa tabia chafu iliyojengeka ndani ya taifa hili ya unafiki, umdhaniye ndiye mara nyingi huwa siye.
JPM pamoja na kujipendekeza sana CCM, na kuwapa vyeo vya ubunge..lakini kimoja cha maumivu makubwa ni kuziba mianya ya CCM kila nchi hii...hata kama hakufanikiwa
Unaona? Kwa unafiki unatetea hata kisichohitaji utetezi. Ama hujui historia ya JPM au kwa makusudi huo ndio upeo wako wa kufikiri pamoja na kuwa kwenye kundi la wanaojiita wasomi, msomi my foot! Unajidhalilisha mdogo wangu...pata japo kaujasiri kadogo wa kuita koleo kwa jina lake rasmi.
CCM wamempoteza na kummaliza huyu, na wengi walijua 2 years back, yule mnayesema mwendazake, nduli , dikteta ali wa screw zaidi CCM.....
Yawezekana? Labda, kwa hiyo hakuwa anaumwa na ndio sababu ya kubugia kikombe cha babu akiwa waziri wa ujenzi katika serikali ya Kikwete?

Babuloliondo1.jpg

Hakuna kitu kibaya kama kudhani unafahamu kumbe hujafamu. Hapo tatizo lako moja kwa moja linakuwa kubwa zaidi, pole.
Mama Samia alikupaje faraja? wakati hata yeye ndani ya masaa 48 angeweza kutokuwa Rais!!!...ni kuwa kapewa chukua ila sio kwa mtazamo huo wenu...Mkuu wa majeshi hakuwa mjinga kusema tutakuheshimu wewe Rais....hii itaongelewa vyema sana baadae
Are you kidding me? Kwamba Rais Mh. Samia Suluhu Hassan hana tofauti na kinyago? Mbona hapa ni kama unamtukana? Ninavyojua Katiba yetu, pamoja na mapungufu yake inaeleza wazi kabisa jinsi Rais atakavyopatikana ikitokea aliye madarakani akaaga dunia.
CCM halisi hao unaowaita wadhalimu, haswaaa ndio wamerudi na wanatamalaki....trust me.Kama corruption ndio inaanza
Samia alitakiwa aseme mazuri yote ambayo dunia nzima na watanzania ataonyesha utofauti na JPM....atawale kwa amani
Kama nilivyosema toka mwanzo na kama madai yako ni kweli, tunalo taifa la wanafiki kuliko wengine tunavyofikiria. Sisi wengine hatushangai CCM ya wadhalimu kurudi madarakani. Mara ngapi wamedai watakaa madarakni hata kwa miaka mia?

Nilicho na hakika nalo ni kwamba hawatakaa madarakani milele...kuna siku wataondoka tu. Hata Kim Jung un wa Korea Kaskazini kuna siku ataondoka tu...mbona jiwe kaondoka?
Kwani CCM wana shida na kuongea? au demokrasia...watawapa wapinzani viti 30...wapinzani watakuwa wenyeviti wa kamati za bunge...CCM watateua baadhi ya wapinzani kuwa wakuu wa taasisi au mawaziri....tujenge taifa...hii lengo ni KULA vizuri.... na kusahaulishwa kwenye katiba na Tume huru, Tume huru wataendelea kutoa ubunge kwa wapinzani kwa order maalumu..
Nashangaa haya unayajua leo. CCM ni genge kama magenge mengine ya kihalifu yalivyo lakini iko siku wataondoka tu. Kama alivyowahi kuonya Mwalimu, kama hawaondoki kwa amani wataondoka kwa shari. Hii itatokea wakati wake ukifika na si leo wala kesho.

Ukishakua mwana CCM wewe ni mmoja wao hata kama unajidanganya eti uko tofauti.
JPM hakuwa mnafiki na zaidi hizi za kudanganya Taifa....na ushamba wake .. .alinyoosha na kuonyesha weakness ni katiba mpya na tume huru.
Kila kizuri ambacho watu walikitaka watakipata ...ila sio katiba mpya au tume huru. kwa CCM ya sasa ambayo ina NJAA kali sana...
Huwezi kumtofautisha jiwe na hilo genge, labda walizidiana ujanja tu. Wakati wenzie wanatumia ujanja ujanja na akili yeye alitumia mabavu. Alisema atahakikisha anaua upinzani (utadhani upinzani umewahi kuwa madarakani wakalififikisha taifa mahali ambapo alihitaji kulinyosha).

Uchafuzi wa mwaka 2020 ni ishara tosha kwamba naye alikuwa mwovu tu kama wenzake. Kizazi kipya kitainuka Tanzania ambacho hakitavumilia huu ukondoo wa kijinga wa Watanzania.
Kosa la JPM ni kuruhusu baadhi ya watu wake kuwa wababe, na yeye kushindwa kuchukua hatua.Kosa lake ni kuweka wapinzani mbali sana ...ambao matokeo ya 2015 na reaction ya upinzani ya kebehi, matusi na dharau..angeweza kuvimeza tu na akakaa nao kushirikiana nao...zile kejeli akazichukulia personal...
Kaniki rangi yake hata ukiifua kwa OMO au JIK haitakati ikawa nyeupe na kumbuka ndege wafananao huruka pamoja. Kaa ukijua kuna Watanzania walioikataa CCM toka inaasisiwa mwaka 1977 ikiwa mikononi mwa Baba wa Taifa.

Jiwe alikuwa katili toka utotoni na hata ubunge wake wa kwanza alishinda kwa mbinde. Hakuwahi hata mara moja kushinda uchaguzi wowote ule kihalali katika maisha yake kwani hakujua kabisa maana ya ushindani.
Lakini kama kuumiza CCM na kukata mirija yao...The man did so very well...hata kama wako walifungua mirija mipya ambayo hakuifahamu
Kama kuna kichaa angeweza kubadili katiba kwa kishindo na kwa manufaa ya Taifa, bado angekuwa JPM pia..kwa caliber yake angeweza.
Kwa mama, tuandae post nyingi sana
Hujui chochote unachosema, everything about Magufuli ilikuwa fake. Magufuli naweza kumfananisha na kiongozi wa juzi wa Marekani anayeitwa Trump. Bahati ya Marekani ni kwamba misingi ya utawala iko imara na ingeyumba kidogo tu, Trump hangeachia madaraka kama rafiki yake Putin wa Urusi.

Siku njema Waberoya.
 
Anasahau kuwa mdharau mwiba mguu huota tende. Linalonipa wasi wasi ni kuwa anaonekana anaweza akasalimu amri kwa wale wadhalimu wa miaka yote waliotufikisha tulipo. Akithubutu hakuna suluhu, itabidi mapambano yaendeleee...
Kinachotia wasiwasi zaidi ni ukimya kuliko matamshi yake.
1. Wamefariki watu 45 ( zaidi ya 30 wanawake) wakati wa kumsindikiza Mwendazake lakini hatujasikia pole au hata tume ya kuchunguza kwa nini jana hilo lilitokea.
2. Hakukemea watu kukamatwa kwa sababu wanakunywa pombe n.k. wakati wa msiba wa Mwendazake.
3. Kesi za wakina Mdude Nyangali zinaendelea kupigwa dana dana lakini hamna tamko baada ya la kwanza kudharauliwa.
4. Mkuu wa Wilaya ameamuru Wakili atiwe ndani mpaka hapo yeye mwenyewe atakapojisikia kutoa lakini kimya.
5. RPC anatishia raia kuwa atawadhuru akiwa amezungukwa na polisi waliovalia kivita lakini kimyaaaa. Mbaya zaidi raia hao ni wanawqke na vitisho vinafanywa siku ya wanawake.
6. Wananchi wamelalamikia serikali kutoa zawadi ya gari la kifahari kwa Rais Mstaafu nako kimyaaa.
7. Lugha za kejeli za Spika wa Bunge. Rais hana Mamlaka kikatiba kuingilia uendeshaji wa Bunge lakini ana uwezo mkubwa wa ku influence yanayotendeka ndani yake.

Huu ukimya unaweza kutafsiriwa kuwa anakubaliana na yanayotendeka na kuwapa ujasiri wanao yafanya kuendelea kuyafanya na wale waliokuwa wanasikilizia kuungana nao.

Amandla...
 
Kinachotia wasiwasi zaidi ni ukimya kuliko matamshi yake.
Kwa kweli hii inafikirisha sana...
1. Wamefariki watu 45 ( zaidi ya 30 wanawake) wakati wa kumsindikiza Mwendazake lakini hatujasikia pole au hata tume ya kuchunguza kwa nini jana hilo lilitokea.
2. Hakukemea watu kukamatwa kwa sababu wanakunywa pombe n.k. wakati wa msiba wa Mwendazake.
3. Kesi za wakina Mdude Nyangali zinaendelea kupigwa dana dana lakini hamna tamko baada ya la kwanza kudharauliwa.
4. Mkuu wa Wilaya ameamuru Wakili atiwe ndani mpaka hapo yeye mwenyewe atakapojisikia kutoa lakini kimya.
5. RPC anatishia raia kuwa atawadhuru akiwa amezungukwa na polisi waliovalia kivita lakini kimyaaaa. Mbaya zaidi raia hao ni wanawqke na vitisho vinafanywa siku ya wanawake.
6. Wananchi wamelalamikia serikali kutoa zawadi ya gari la kifahari kwa Rais Mstaafu nako kimyaaa.
7. Lugha za kejeli za Spika wa Bunge. Rais hana Mamlaka kikatiba kuingilia uendeshaji wa Bunge lakini ana uwezo mkubwa wa ku influence yanayotendeka ndani yake.
Labda ni kweli kuna masharti aliyopewa kama anavyodai Waberoya? Asiguse kusikogusika.

Huu ukimya unaweza kutafsiriwa kuwa anakubaliana na yanayotendeka na kuwapa ujasiri wanao yafanya kuendelea kuyafanya na wale waliokuwa wanasikilizia kuungana nao.

Amandla...
Kwamba tuendelee kutazama kama vile tunaangalia maigizo kwenye TV? In Tanzania anything is possibble. Ukimsikiliza Ndugai kule bungeni ni lazima mtu ujiulize, kulikoni?
 
Hapana, mimi na wewe ni kama mbingu na ardhi. Unayoyaamini na kuyatetea toka nikufahamu humu JF hatujawahi kutaka vitu vinavyofanana ila kwa tabia chafu iliyojengeka ndani ya taifa hili ya unafiki, umdhaniye ndiye mara nyingi huwa siye.

Unaona? Kwa unafiki unatetea hata kisichohitaji utetezi. Ama hujui historia ya JPM au kwa makusudi huo ndio upeo wako wa kufikiri pamoja na kuwa kwenye kundi la wanaojiita wasomi, msomi my foot! Unajidhalilisha mdogo wangu...pata japo kaujasiri kadogo wa kuita koleo kwa jina lake rasmi.

Yawezekana? Labda, kwa hiyo hakuwa anaumwa na ndio sababu ya kubugia kikombe cha babu akiwa waziri wa ujenzi katika serikali ya Kikwete?


Hakuna kitu kibaya kama kudhani unafahamu kumbe hujafamu. Hapo tatizo lako moja kwa moja linakuwa kubwa zaidi, pole.

Are you kidding me? Kwamba Rais Mh. Samia Suluhu Hassan hana tofauti na kinyago? Mbona hapa ni kama unamtukana? Ninavyojua Katiba yetu, pamoja na mapungufu yake inaeleza wazi kabisa jinsi Rais atakavyopatikana ikitokea aliye madarakani akaaga dunia.

Kama nilivyosema toka mwanzo na kama madai yako ni kweli, tunalo taifa la wanafiki kuliko wengine tunavyofikiria. Sisi wengine hatushangai CCM ya wadhalimu kurudi madarakani. Mara ngapi wamedai watakaa madarakni hata kwa miaka mia?

Nilicho na hakika nalo ni kwamba hawatakaa madarakani milele...kuna siku wataondoka tu. Hata Kim Jung un wa Korea Kaskazini kuna siku ataondoka tu...mbona jiwe kaondoka?

Nashangaa haya unayajua leo. CCM ni genge kama magenge mengine ya kihalifu yalivyo lakini iko siku wataondoka tu. Kama alivyowahi kuonya Mwalimu, kama hawaondoki kwa amani wataondoka kwa shari. Hii itatokea wakati wake ukifika na si leo wala kesho.

Ukishakua mwana CCM wewe ni mmoja wao hata kama unajidanganya eti uko tofauti.

Huwezi kumtofautisha jiwe na hilo genge, labda walizidiana ujanja tu. Wakati wenzie wanatumia ujanja ujanja na akili yeye alitumia mabavu. Alisema atahakikisha anaua upinzani (utadhani upinzani umewahi kuwa madarakani wakalififikisha taifa mahali ambapo alihitaji kulinyosha).

Uchafuzi wa mwaka 2020 ni ishara tosha kwamba naye alikuwa mwovu tu kama wenzake. Kizazi kipya kitainuka Tanzania ambacho hakitavumilia huu ukondoo wa kijinga wa Watanzania.

Kaniki rangi yake hata ukiifua kwa OMO au JIK haitakati ikawa nyeupe na kumbuka ndege wafananao huruka pamoja. Kaa ukijua kuna Watanzania walioikataa CCM toka inaasisiwa mwaka 1977 ikiwa mikononi mwa Baba wa Taifa.

Jiwe alikuwa katili toka utotoni na hata ubunge wake wa kwanza alishinda kwa mbinde. Hakuwahi hata mara moja kushinda uchaguzi wowote ule kihalali katika maisha yake kwani hakujua kabisa maana ya ushindani.

Hujui chochote unachosema, everything about Magufuli ilikuwa fake. Magufuli naweza kumfananisha na kiongozi wa juzi wa Marekani anayeitwa Trump. Bahati ya Marekani ni kwamba misingi ya utawala iko imara na ingeyumba kidogo tu, Trump hangeachia madaraka kama rafiki yake Putin wa Urusi.

Siku njema Waberoya.

Mkuu

Ndio nimekufahamu vizuri kabisa leo

Kila la heri katika mapambano ya kudai unayoyataka

cheers
 
Maisha ya kuwa mpinzani ni ya shida sana. Imagine inabidi utafute kitu cha kupinga na unakikosa so inabidi upinge tu hata kama hakuna cha kupinga.
Mimi naona maisha ya kuwa CCM ndiyo shida zaidi,unakuwa kama bwege fulani hivi,si unaona waliokuwa wanamshangilia JPM leo wamegeukia kwa SSH,mpaka naona aibu mimi
 
Rais wetu Mh. Samia Suluhu Hassan, ada ya mja hunena, mwungwana ni kitendo na siku njema huonekana asubuhi.

Wewe ni Rais wetu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliyoapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea.

Kupitia hiyo Katiba sisi wananchi tuliamua rasmi na kwa dhati kujenga jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani.

Mh. Rais, tarehe 29 Machi, 2021 uliapishwa kuliongoza Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar-es-Salaam.

Leo tarehe 9 Mei, 2021 ni siku ya arobaini toka ulipoapishwa na kuwa Kiongozi Mkuu wa taifa hili lenye watu karibia milioni sitini (60,000,000!)

Kama kiongozi matendo yako ni lazima yalete faraja na matumaini kwa Watanzania wote na kuhamasisha zaidi ushiriki wao katika hatma ya taifa.

Pamoja na kuapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea Katiba, epukana kabisa na matendo yanayoweza kutafsiriwa kwamba yanapingana na Katiba.

Mh. Rais kumbuka kauli huumba hivyo epukana pia na zile kauli ambazo zinaweza kutafsiriwa na wasaidizi wako kama ruhusa ya kuvunja Katiba.

Hali hii inahusu hasa yale maagizo yanayotolewa papo kwa papo bila kupima yatakavyopokelewa na watendaji wakuu wa vyombo vya dola.

Mh. Rais tuko wengi ambao kuapishwa kwako kulitupa japo faraja kutokana na mizengwe ya awali iliyokuwa ikifanywa na mahafidhina.
Amini usiamini asilimia kubwa ya wananchi bila kujali tofauti zao walipokea mabadiliko ya uongozi wa juu kabisa wa nchi kwa matumaini.

Yawezekana walisukumwa na sababu mbali mbali lakini lililowaunganisha ni uhitaji wa hewa safi kupitia dirisha ambalo ujio wako ungewafungulia.

Ni hilo dirisha lingewezesha kiapo chako kiwe na maana kwa kuturudisha kwenye utawala wa sheria unaoheshimu, kulinda na kutetea Katiba

Ingawa wengi tulikupokea bila kujali unatoka miongoni mwa watu wale wale na chama kile kile, tuliguna kidogo uliposema kazi iendelee.

Kiongozi bora hafuati tu nyayo za aliyemtangulia, hapana, huyo si kiongozi bora, ni mfuasi, kiongozi bora huvumbua njia salama wapite anaowaongoza.

Tafadhali Mh. Rais, acha kupaka ukuta rangi nyumba ipendeze huku msingi una nyufa; shughulikia kwanza msingi nyumba iwe imara na salama.

Tunayo Katiba ya mwaka 1977 lakini cha ajabu ni kuwa hata hii. pamoja na mapungufu yake, tunashindwa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea!

Tunayo Rasimu ya Warioba lakini kwa Mh. Samia Suluhu Hassan, hata kuitaja tu imekuwa shida, shida ni nini? Je kuku wetu anataga kwenye miba?

Mwanga uliojitokeza unaanza kufifia ghafla huku safari hatujafika hata nusu, je kulikoni? Chukua hatua, katika kuidai Katiba mpya sahau suluhu.

Shughulikia sheria zote ambazo zinaisigina Katiba kwa namna moja au nyingine kwani tuna kiu kubwa ya utawala unaozingatia haki na usawa.

Ngoja Ngoja yaumiza matumbo na linalowezekana leo lisingojee kesho; kwa kweli baada ya miaka minne ya giza uvumilivu uko mashakani.
Siku 40 unataka atende miujiza Hata kama angekua mkuu wa malaika haiwezekani kila kitu kifanywe mara moja
 
Rais wetu Mh. Samia Suluhu Hassan, ada ya mja hunena, mwungwana ni kitendo na siku njema huonekana asubuhi.

Wewe ni Rais wetu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliyoapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea.

Kupitia hiyo Katiba sisi wananchi tuliamua rasmi na kwa dhati kujenga jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani.

Mh. Rais, tarehe 29 Machi, 2021 uliapishwa kuliongoza Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar-es-Salaam.

Leo tarehe 9 Mei, 2021 ni siku ya arobaini toka ulipoapishwa na kuwa Kiongozi Mkuu wa taifa hili lenye watu karibia milioni sitini (60,000,000!)

Kama kiongozi matendo yako ni lazima yalete faraja na matumaini kwa Watanzania wote na kuhamasisha zaidi ushiriki wao katika hatma ya taifa.

Pamoja na kuapa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea Katiba, epukana kabisa na matendo yanayoweza kutafsiriwa kwamba yanapingana na Katiba.

Mh. Rais kumbuka kauli huumba hivyo epukana pia na zile kauli ambazo zinaweza kutafsiriwa na wasaidizi wako kama ruhusa ya kuvunja Katiba.

Hali hii inahusu hasa yale maagizo yanayotolewa papo kwa papo bila kupima yatakavyopokelewa na watendaji wakuu wa vyombo vya dola.

Mh. Rais tuko wengi ambao kuapishwa kwako kulitupa japo faraja kutokana na mizengwe ya awali iliyokuwa ikifanywa na mahafidhina.
Amini usiamini asilimia kubwa ya wananchi bila kujali tofauti zao walipokea mabadiliko ya uongozi wa juu kabisa wa nchi kwa matumaini.

Yawezekana walisukumwa na sababu mbali mbali lakini lililowaunganisha ni uhitaji wa hewa safi kupitia dirisha ambalo ujio wako ungewafungulia.

Ni hilo dirisha lingewezesha kiapo chako kiwe na maana kwa kuturudisha kwenye utawala wa sheria unaoheshimu, kulinda na kutetea Katiba

Ingawa wengi tulikupokea bila kujali unatoka miongoni mwa watu wale wale na chama kile kile, tuliguna kidogo uliposema kazi iendelee.

Kiongozi bora hafuati tu nyayo za aliyemtangulia, hapana, huyo si kiongozi bora, ni mfuasi, kiongozi bora huvumbua njia salama wapite anaowaongoza.

Tafadhali Mh. Rais, acha kupaka ukuta rangi nyumba ipendeze huku msingi una nyufa; shughulikia kwanza msingi nyumba iwe imara na salama.

Tunayo Katiba ya mwaka 1977 lakini cha ajabu ni kuwa hata hii. pamoja na mapungufu yake, tunashindwa kuiheshimu, kuilinda na kuitetea!

Tunayo Rasimu ya Warioba lakini kwa Mh. Samia Suluhu Hassan, hata kuitaja tu imekuwa shida, shida ni nini? Je kuku wetu anataga kwenye miba?

Mwanga uliojitokeza unaanza kufifia ghafla huku safari hatujafika hata nusu, je kulikoni? Chukua hatua, katika kuidai Katiba mpya sahau suluhu.

Shughulikia sheria zote ambazo zinaisigina Katiba kwa namna moja au nyingine kwani tuna kiu kubwa ya utawala unaozingatia haki na usawa.

Ngoja Ngoja yaumiza matumbo na linalowezekana leo lisingojee kesho; kwa kweli baada ya miaka minne ya giza uvumilivu uko mashakani.

E0NhMwdXIAAW0HL (1).jpeg
 
Mama kapata washauri kwa vile mtu wa mitandao sijui aanze na ushauri upi.
 
Nyie Wapinzani kwa kweli ni weupe sana vichwani! Unazungumzia Rasimu ya Warioba wakati mnajua kabisa tuko katika " Katiba inayopendekezwa"! Kwa akili za hovyo hivi ngoja Mhe. Job Ndugai aendelee kuwaburuza kwa sababu mambo mengi mnajitoa ufahamu sana!
 
Muda wa kubadili katiba sio sasa apambane uchumi uliodorora nchi ifunguke tuwe sawa sawa corona ipute huko baadae huko ndio tuongee katiba sio sasa.
Ndio muda muufaka sasa kubadili katiba toka 1977 katiba mbovu sana hii haikidhi mahitajio yetu ni 44 yrs sasa ni mawazo ya kale sana tuko karne 21 sasa hii katiba ni WATANGANYIKA sio ya WATANZANIA ndio maana watanganyika wajinga wanaipenda lkn time ikifika itakwenda kama alivoondoka yule nambari 10 basi na hii katiba iko siku itaondoka tu .
 
Mimi naona maisha ya kuwa CCM ndiyo shida zaidi,unakuwa kama bwege fulani hivi,si unaona waliokuwa wanamshangilia JPM leo wamegeukia kwa SSH,mpaka naona aibu mimi
Watu wengi wa Ccm wana utulivu wa nafsi na maisha yao yanaenda vizuri.
 
Back
Top Bottom