Rais Samia: Nashangaa Umeme kukatika Marekani!

Rais Samia: Nashangaa Umeme kukatika Marekani!

Bulesi

Platinum Member
Joined
May 14, 2008
Posts
14,275
Reaction score
13,929
Rais Samia alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi huko Marekani[ U.S.A.] alipata wasaa wa kuwahutubia waTanzania wanaoishi huko.

Alipokuwa anatoa hotuba yake palitokea tukio moja lililomfanya akumbuke nyumbani; ingawa alikuwa ughaibuni nalo lilikuwa pale UMEME ulipokatika wakati akitoa hotuba!!

Mheshimiwa Rais ikabidi aweke kibwagizo kuwa kumbe hata huku UMEME unakatika, ingekuwa nyumbani tukio kama hili January angesulubiwa!!

Tukumbuke tu kuwa tatizo la ukatikaji wa Umeme nyumbani sio sawa na ughaibuni; kwanza ule Umeme ulipokatika pale Nadhani Ilikuwa tatizo la switch ambapo Umeme ulirudi baada ya muda mchache tu ili hali sisi nyumbani umeme ukikatika unakatika kweli , kunasehemu watu wanakosa umeme wa kufanyia kazi hata wiki nzima hivyo hatuwezi kufananisha matatizo yetu ya umeme na wenzetu.

January ni lazima afanye kazi yake kwa weledi ingawa mfano ya Samia inaonesha kama vile kumkingia kifua kuwa hata Marekani pia unakatika, lakini umeme wa Marekani unarudi saa hizo hizo kwahiyo asilaze damu kwani atasulubiwa hata kama atakingiwa kifua mpaka hapo watu watakapopata huduma jinsi zinavyostahili!

Mama kasema kuwa yeye huwa hawakemei vijana wake bali husema nao kwa kuwapiga macho basi tunangojea kama January ataelewa mara atakapopigwa jicho!
 
Kashiba pizza na burger za marekani huyo. Arudi sasa au anasubiri acheze Iddi huko huko.

Ila wasipokuwa makini anaweza asirudi tena huku inaelekea kanogewa huko. Maana kama kuhutubia nadhani amebakisha omba omba tu. Hata wenyeji wake hawajui wampeleke wapi tena kutembea.
 
Anaogopesha kidogo...

Maana kwa kauli aliyoitoa anaonyesha haamini kama kukatika katika kwa umeme ni tatizo.

Na nachelea kusema, kwangu tatizo sio umeme kukatika...tatizo ni kiongozi kutokuona kama kukatika katika kwa umeme ni tatizo.

Hii mentality mbaya saana.
 
Angenyamaza tu,vyombo vya habari ndio vingeripoti.Udhaifu wetu ulinganishwe na mtu,siyo yeye ajilinganishe na nchi aliko
 
Kashiba pizza na burger za marekani huyo. Arudi sasa au anasubiri acheze Iddi huko huko.

Ila wasipokuwa makini anaweza asirudi tena huku inaelekea kanogewa huko. Maana kama kuhutubia nadhani amebakisha omba omba tu. Hata wenyeji wake hawajui wampeleke wapi tena kutembea.
[emoji28][emoji28][emoji28]

Ataanza kwenda kwenye mabembea kama mentor wake.

#MaendeleoHayanaChama
 
Rais Samia alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi huko Marekani[ U.S.A.] alipata wasaa wa kuwahutubia waTanzania wanaoishi huko. Alipokuwa anatoa hotuba yake palitokea tukio moja lililomfanya akumbuke nyumbani; ingawa alikuwa ughaibuni nalo lilikuwa pale UMEME ulipokatika wakati akitoa hotuba!! Mheshimiwa Rais ikabidi aweke kibwagizo kuwa kumbe hata huku UMEME unakatika, ingekuwa nyumbani tukio kama hili January angesulubiwa!!

Tukumbuke tu kuwa tatizo la ukatikaji wa Umeme nyumbani sio sawa na ughaibuni; kwanza ule Umeme ulipokatika pale Nadhani Ilikuwa tatizo la switch ambapo Umeme ulirudi baada ya muda mchache tu ili hali sisi nyumbani umeme ukikatika unakatika kweli , kunasehemu watu wanakosa umeme wa kufanyia kazi hata wiki nzima hivyo hatuwezi kufananisha matatizo yetu ya umeme na wenzetu. January ni lazima afanye kazi yake kwa weledi ingawa mfano ya Samia inaonesha kama vile kumkingia kifua kuwa hata Marekani pia unakatika, lakini umeme wa Marekani unarudi saa hizo hizo kwahiyo asilaze damu kwani atasulubiwa hata kama atakingiwa kifua mpaka hapo watu watakapopata huduma jinsi zinavyostahili! Mama kasema kuwa yeye huwa hawakemei vijana wake bali husema nao kwa kuwapiga macho basi tunangojea kama January ataelewa mara atakapopigwa jicho!
Kukatika umeme kwa sababy ya hitilafu popote pale inatokea ila kukatika umeme kwa upuuzi wa umeme mdogo so tunatakiwa tugawe leo wapate hawa kesho wapate wale huo upumbavu Marekani hamna kabisa
 
ingekuwa nyumbani tukio kama hili January angesulubiwa!!
200 (2).gif
 
Utakuja kushangaa kwamba ata kukata umeme hilo jengo ni mchezo umechezwa.

Walioko Marekani watuambie je ni mtaa mzima ulikatika?

January anaraha sanaa.
 
Back
Top Bottom