Rais Samia ni Dkt. Magufuli mwenye Mtazamo tofauti na Hayati Magufuli

Rais Samia ni Dkt. Magufuli mwenye Mtazamo tofauti na Hayati Magufuli

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,832
Reaction score
2,390
Mara kadhaa, mama Samia anasema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Huenda ni watu aina moja kwa sababu wametokana na uchaguzi mmoja.
Ukifuatilia kauli zake hasa katika hotuba ya leo, dira ya Taifa katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo na Ilani ya CCM vinaonyesha tofauti kubwa katika utekelezaji wake.
Mama Samia anakiri kwamba;

  1. Viongozi waliopita walifanya kazi nzuri na mema yao yanastahiki kuendelezwa. Hapa aliwataja kwa majina kuanzia Nyerere mpaka JPM. Haamini katika maneno ya kwamba nchi hii ililiwa sana huko nyuma. Hataki kuonesha kwamba yeye na mwenzake wanaanza upya katika mapambano ya wizi na ufisadi. Anawaheshimu waliopita.
  2. Mama Samia anakiri wazi kuwa sera zetu juu ya uwekezaji hazitabiriki, kodi haileweki na pia kuna bureaucracy ya kutosha kwa wawekezaji. Hii ni kwamba anaona ni namna gani serikali iliyopita ilivyokuwa ikipuuza uwekezaji na kuamini itakuwa dona kantry katika mazingira ya kujitegemea peke yake.
  3. Mh. Rais amekiri wazi kuwa uwekezaji ulizorota na akasisitiza kuweka ile Wizara chini ya ofisi ya Waziri Mkuu ili kazi ifanyike. Hili ni eneo lililo tofauti sana na mtangulizi wake. Awamu ya tano, wawekezaji walikimbia kodi nyang'anyi, vitisho na kubadilikabadilika kwa Sera.
  4. Amewaita wapinzani kufanya nao mazungumzo. Licha ya kwamba hili linahitaji tahadhari kwa sababu ni mwanzo, ameonyesha yupo tayari huenda hata kuondoa vikwazo vya wanasiasa kukutana na wapenzi na wanachama wao.
  5. Rais Samia, ametambua licha ya kwamba utambuzi wake unaendelea, Corona ipo na anahitaji ufanyike utafiti wa kina ili kuweza kukabiliana nayo kama Taifa. Hakuamua kwenda kupima papai au kupuuza chanzo. Hatari ya kukanusha dawa za Kisayansi zilikuwa zinaenda kufanya jamii isiamini katika tiba za aina zozote ikiwamo zile za kufubaza virusi vya ukimwi, chanzo za TB nk.
  6. Mama Samia ametamka wazi uchumi kusuasua kwa kutaja ukuaji wa asilimia 4.7. Huko nyuma takwimu zilikuwa hazieleweki na hata wataalam wa IMF na World Bank hawakupata fursa ya kuhakiki hali ya uchumi. Kiujumla hali ya ukuaji wa uchumi ni mbaya na lazima tukubali tupo hapo ili tuweze kusonga mbele. Huenda kuanzia sasa tutaona takwimu zinazoakisi uhalisia katika maeneo yote.
  7. Kwenye uwekezaji wa kwenye ndege, amehitaji uboreshaji. Hiki ni kiashiria kwamba, nchi itajikita kwenye kuweka mifumo imara na wataalam ili kuongeza tija na si ndege.
Kwa mitazamo hii mama Samia ameamua kubadili mtazamo wa kuendelea kuwa Magufuli na kutenda tofauti na Magufuli
 
Hata bandari ya Bagamoyo amekuwa tofauti na Magu hapa utasemaje yeye na Magu wapo sawa
Hata akikutana anataka wajadili jinsi ya kufanya siasa zenye tija kwa nchi.

Maana yake baada ya kukutana hatutarajii kuwaona akina Lisu wakiponda Atcl, Sgr, bwawa la Nyerere kuwa ni miradi ya hovyo badala yake wataanza kusema hiyo ni miradi ya Watanzania.

Kwa akili zao wanahisi mama ataenda kuwaruhusu kufanya maandamano kila siku.
 
Maandamano hutokana na kuminya demokrasia,,pale ambapo watu huwa huru kufanya shughuli zao za kisiasa mijadala hutawala na maandamano huwa hayana tija.
 
Maandamano hutokana na kuminya demokrasia,,pale ambapo watu huwa huru kufanya shughuli zao za kisiasa mijadala hutawala na maandamano huwa bhayana tija.

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
Inaonekana bado kijana mdogo, enzi ya JK maandamano yalikuwa kila kona kila siku hata watoto wa Primary na uhuru wa kuropoka ulikuwa mwingi pia na ufisadi ulitamalaki.
 
Mkimpa Uenyekiti anawakomoa, kwa sasa anakua upande wenu sababu hana nguvu
 
Toka Lin mtu atoke Kiembesamaki na mwingine atoke Chato wawe kitu kimoja
 
Kwani Kikwete aliwai kuiba akaweka wapi?? Yale mahoteli waliyojenga Chato na ndugu zake unadhani kwa fedha gani?
Mkuu, akaweka wapi Swiss Bank?..Simtetei lakini labda Magu mwingine..Niambie violations of financial rules nitakuelewa.
 
Kwenye sekta binafsi kiashiria ni kuchukua hatua nyingine badala ya consolidation ya huduma za kibenki na usafiri.

Ukweli, Serikali ilipambana sana kuua private airlines ambazo zilikuwa nafuu na kuleta za kwake ambazo ni ghali, ubunifu mdogo, gharama kubwa za uendeshaji na Usimamizi mbovu wenye malengo ya kuridhisha wanasiasa na sio tija.
 
Back
Top Bottom