Rais Samia, ni vyema Watanzania wenye sifa za kuwa viongozi wa kimataifa wang'ae kwa umahiri wao, sio kuwang'arisha kwa nguvu ya fedha au siasa

Rais Samia, ni vyema Watanzania wenye sifa za kuwa viongozi wa kimataifa wang'ae kwa umahiri wao, sio kuwang'arisha kwa nguvu ya fedha au siasa

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Dr. Faustine Ndugulile ameondoka katika kipindi ambacho alitazamiwa kuwa mkuu wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika. Ametuachia majonzi makubwa sana! Sasa tunatamani mtu mwingine achukue nafasi yake.

Kwa bahati mbaya kila mtu siku hizi anaamini fedha na siasa ndio inampa mtu haki au sifa za kuwa kiongozi!

Lakini napenda kusema kuwa ni vizuri watanzania wenye uwezo na weledi katika nyanja mbalimbali wakapatiwa nafasi ya kujulikana na kung'aa kulingana na umahiri wao. Na kama kuna nafasi zozote za uteuzi au uchaguzi, basi mng'ao wao utaonekana na kuwafanya wachaguliwe au kuteuliwa.

Tuachane na huu mtindo ulioingia wa kutumia nguvu nyingi kung'arisha watu hata wale wasioweza kung'aa.

Ninaomba sana Tanzania isitumie nguvu kubwa ya kisiasa na fedha kufanya kampeni ili watanzania wachaguliwe kwenye nafasi mbalimbali ndani na nje ya nchi. Tujitahidi kuinua elimu yetu na professionalism yetu kwani kwa jinsi mambo yalivyo sasa inahitaji kutumia siasa na fedha nyingi mno kumpata mtu mwenye "weledi" wa kimataifa au hata kitaifa.

Tuweke nguvu zetu na fedha zetu kwenye mambo muhimu ya taifa letu kama vile maji, umeme, huduma za afya, elimu na uchumi.
 
Na tuache kuwapiga vita wanaoruka kwa mbawa zao, wanaotokea from nowhere na kutafuta means za kwenda kimataifa kivyaovyao! Kutokuwa anajulikana au anatoka kwenye familia zinazojulikana au kutokuwa affiliated na chama fulani isiwe sababu ya kuzuia watu kuexcell kimataifa, wapate support bila ubaguzi so long as ni watanzania!
 
Dr. Faustine Ndugulile ameondoka katika kipindi ambacho alitazamiwa kuwa mkuu wa Shirika la Afya Duniani kanda ya Afrika. Ametuachia majonzi makubwa sana! Sasa tunatamani mtu mwingine achukue nafasi yake.

Lakini napenda kusema kuwa ni vizuri watanzania wenye uwezo na weledi katika nyanja mbalimbali wakapatiwa nafasi ya kujulikana na kung'aa kulingana na umahiri wao. Na kama kuna nafasi zozote za uteuzi au uchaguzi, basi mng'ao wao utaonekana na kuwafanya wachaguliwe au kuteuliwa.

Tuachane na huu mtindo ulioingia wa kutumia nguvu nyingi kung'arisha watu hata vile wasioweza kung'aa.

Ninaomba sana Tanzania isitumie nguvu kubwa ya kisiasa na fedha kufanya kampeni ili watanzania wachaguliwe kwenye nafasi mbalimbali ndani na nje ya nchi. tujitahidi kuinua elimu yetu na professionalism yetu kwani kwa jinsi mambo yalivyo sasa inahitaji kutumia siasa na fedha nyingi mno kumpata mtu mwenye weledi wa kimataifa au hata kitaifa.

Tuweke nguvu zetu na fedha zetu kwenye mambo muhimu ya taifa letu kama vile maji, umeme, huduma za afya, elimu na uchumi.
Huu ni mtindo wetu wa kisasa ndani umeonyesha mafanikio ya kishindo sasa ni muda wakuupeleka kimataifa.
 
Back
Top Bottom