Rais Samia pamoja na ziara yako nzuri huko UAE, Suala la Ngorongoro liwe nje ya ajenda

Rais Samia pamoja na ziara yako nzuri huko UAE, Suala la Ngorongoro liwe nje ya ajenda

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Mheshimiwa Rais,

Umefanya ziara ya kikazi huko UAE, hilo ni jambo zuri tunalifurahia

Lakini wakati ukifanya Ziara hiyo, Watanzania hatujasahau kuwa Kampuni ya waarabu wa UAE iitwayo OBC imekuwa ikimezea mate ardhi ya wananchi inayokaliwa na wamasai huko Ngorongoro.

Tuna historia nzuri namna Mwana mfalme Brigedia Al Ali alivyopewa vitalu vya uwindaji kifisadi huko Loliondo enzi za utawala wa mzee Mwinyi, na tunajua namna alivyokuwa akikingiwa kifua na tawala zilizofuata.

Sasa tunapata wasiwasi kuwa umeenda huko kipindi hiki ambacho kuna vuguvugu la kutaka kuwaondoa wamasai kwa visingizio feki vya kutunza mazingira na uhifadhi lakini dalili zote ni. kutaka kuipa hiyo kampuni ya UAE eneo zaidi. Hatujui kama kwenye meza ya majadiliano hilo mmelizungumza, lakini hata kama mmelizungumza, mheshimiwa rais hiyo kitu ni kaa ya moto achana nayo kabisaa maana sisi wsnanchi hatuwezi kuikubali.

Tunajua miezi mitatu iliyopita alikuwepo waziri wako wa fedha huko UAE ndugu Mwigulu Nchemba, na tunajua kuwa kipindi Mwigulu alipokuwa naibu katibu mkuu wa CCM enzi za Kikwete amewahi kuunda kamati ya kuchunguza ishu za migogoro ya Ngorongoro, na hatujui kamati yake ilikuja na findings zipi, kwa hiyo tulipomuona kaenda huko UAE, na kisha aliporejea nchini tukaanza kuona harakati za kuwaondoa Wamasai Ngorongoro zimeshika kasi, tukahisi hapa lazima kuna kitu mwarabu keshafabya behind the scene!

Mwisho nataka nikwambie mheshimiwa Rais, kama mmewekeana saini ya kusafirisha wanyama wetu ili Dubai watengeneze Mbuga yao kwa kutumua wanyama kutoka Africa kama tulivyoona kwenye mitandao nayo achana nayo. Hao watu wana hela, na wanaweza kuathiri utalii wetu sana kama wakiweza kutengeneza mfano wa Safari za Afrika.

Tunajua, Mwarabu ni mzuri sana wa kugawa "Takrima", Tafadhali ndugu Rais hakikisha mwarabu hatii mguu kwenye Mbuga zetu, wanyama wetu na kikubwa zaidi kufukuza wananchi wetu ili yeye apate nafasi ya vitalu zaidi vya uwindaji.
 
Binafsi nilikuwa naegemea upande mmoja ila, nasadiki kusema acheni watu wale na kumbukeni nchi inafunguliwa, acheni kulialia, hii nchi ni kubwa.

Ongeza na hii ya wale ndugu zako, "tuliumizwa sana na sasa anaupiga mwingi"
 
Hivi kipi Bora? Mmasai aharibu mazingira ya wanyama tukose watalii na pato lake ama mwarabu atunze wanyama na kutupatia Kodi?
Anatunza au anaua huyo? Mwarabu kazi ya kusafirisha walio hai na waliopo anaua ndugu!!

Kama.wanawafukuza Wmasaai na waachane na uwindaji pia
 
OBC Bado Wapo Ngorongoro Na Mkataba Wao Ni Mrefu
 
1. Hujawai ona jema kwa Samia

2. Hakuna mkataba uliosainiwa juu ya Wanyama au Ngorongoro. Kabla ya kupost kitu fanya utafiti

3. Ngorongoro lazima ilindwe kwa faida na maslahi makubwa kwa Taifa kiutalii inayoongoza katika kukuza pato la Taifa hivyo lazima uhifadhi ulindwe kwa gharama yeyote

4. Tayari Wamasai wameanza kujiandiskisha kuondoka na soon sheria inatungwa
 
Ngorongoro ishapigwa bei.
Mwinyi aliuza Loliondo Gate
Mkapa akauza mashirika ya serikali, nyumba na viwanda na migodi pia.
Kikwete akauza ardhi ya Bagamoyo kwa Wachina.
Huyu sasa kasaini mikataba 14 ya uwekezaji.
Soon wamasai wataondolewa
Malalamiko fc kazini
 
Mikataba tuliyo saini nao ni pamoja na maswala ya Utalii .

Sasa sijui waarabu tunashirikiana nao katika Utalii kuhusiana na nini kama sio uwindaji maana ndio wanachokipenda.
 
Mikataba tuliyo saini nao ni pamoja na maswala ya Utalii .

Sasa sijui waarabu tunashirikiana nao katika Utalii kuhusiana na nini kama sio uwindaji maana ndio wanachokipenda.
Kwa upande wa utalii Elsewedy company wanajenga kituo cha utalii wa mikutano Zanzibar

Muwe mnafuatilia mambo mnatia aibu
 
Kwa upande wa utalii Elsewedy company wanajenga kituo cha utalii wa mikutano Zanzibar

Muwe mnafuatilia mambo mnatia aibu
Kituo cha utalii??

Hilo ndio jambo tunalohitaji kweli ili kukuza utalii wetu??

Haya ndio madhara ya kuomba omba unapewa hata usivyohitaji.
 
Kituo cha utalii??

Hilo ndio jambo tunalohitaji kweli ili kukuza utalii wetu?

Haya ndio madhara ya kuomba omba unapewa hata usivyohitaji.
Kwanza unaelewaje ukiambiwa kituo cha utalii wa mikutano?

Manaake naona kama una elimu ya hapa na pale? Nikueleweshe kwanza
 
Hizi ni pumba tu. Hata wangechukua nusu ya wanyama na kuwapeleka Sharjah kwenye Zoo hawawezi kuathiri biashara ya Ngorongoro kiutalii. Ngorongoro ni caldera pekee duniani ambayo ina wanyama wanaishi na binadamu.

Pili suala la kupunguza watu Ngorongoro ni la kitaalamu. Wananchi wapatao 110,000 na mifugo ikadriwayo kufika 800,000 ni hatarishi kwa uhai wa Ngorongoro kama kivutio cha watalii.
 
Masai hana ardhi ngorongoro, Tanzania ardhi yote ni ya Wananchi na itatumika kwa maslahi ya Taifa.

Kama arshi ya ngorongoro ya wamasai, kilosa mnatafuta nini? Mvomero mnafanya nini?

Hawa masai wanacheleweshwa wanazidi kuchonga mdomo.

Serikali inipe tenda ya kuwaondoka chapu niwaonyeshe.
 
Back
Top Bottom