Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,843
- 31,057
Nimemsikia Rais Samia Jana, wakati akihutubia wakazi wa Mtibwa -Morogoro, akiwa katika ziara Mkoani humo, akiwatahadharisha wateule wake, hususani walioko Kwenye wizara ya kilimo kuwa chakula ni jambo nyeti sana, ukitokea upungufu wa chakula nchini, unaweza walazomisha vijana wanaotambulika siku hizi kama Gen Z, waingie mitaani na kuandamana.
Ninachomwambia Rais Samia, ni kuwa Kuna mambo mengi sana ya hovyo, yanayofanyika nchini kwetu, ambayo hao vijana wa Gen Z wa nchini kwetu, wanayavumilia, lakini naamini, itakapofika mwisho wa uvumilivu wao, wataingia barabarani na kuandamana.
Matatizo hayo ni pamoja na vijana wengi sana wanaomaliza elimu ya vyuo vikuu kila mwaka, kukosa ajira nchini
Vile vile mifumo ya nchi hii ndilo tatizo Kuu linaloliangamiza Taifa letu.
Hii nchi kiuhalisia Haina mipaka ya utendaji wake wa kazi, Kati ya mihimili mikuu 3 ya Dola, ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama.
Katika nchi yetu, serikali, chini ya Rais wa Jamhuri ndiye mhimili Mkuu, ambao Kwa maneno ya Mwendazake John Magufuli kuwa ndiyo mhimili uliojichimbia zaidi chini!
Katika nchi yetu Rais amepewa madaraka makubwa mno ya ki-mungu- mtu, kunakofanya mihimili Ile mingine ya Bunge na Mahakama, isiweze kufanya kazi Kwa uhuru.
Mimi huwa najiuliza hivi kama kweli mihimili hii 3 ingekuwa inafanya kazi Kwa uhuru bila kuingiliwa na mhimili mwingine, hivi ni kwanini wale wabunge 19 wa viti maalum, wanaendelea kuwemo Bungeni Kwa mwaka wa 4 hivi sasa, wakati inafahamika wazi kuwa wabunge hao hawana chama wanachokiwakilisha Bungeni, baada ya Chama Cha Chadema, wanachodai kuwa wao ni wanachama wa chama hiko, kusema kuwa imeshawafukuza zamani sana, tokea mwaka 2020??
Hivi inakuwaje Spika wa Bunge, achukuwe uamuzi wa kumfukuza Mbunge Luhaga Mpina, ambaye amesema kuwa Waziri Bashe amelidanganya Bunge, ambao ni wajibu namba moja wa wabunge wa kuisimamia serikali, wakati alipotoa taarifa ya uagizaji wa sukari, wakati kulipotokea upungufu mkubwa wa sukari, mwishoni mwa mwaka Jana??
Kwa hiyo nimwambie Rais Samia, kuwa vipo viashiria vingi sana, vinavyoweza kusababisha hii Gen Z ya hapa nchini kuweza kuandamana na Wala siyo tuu kwa kukosa sukari, kama alivyotahadharisha Rais Samia Jana, ambako yupo ziarani Mkoani Morogoro.
Mungu ibariki Tanzania
Ninachomwambia Rais Samia, ni kuwa Kuna mambo mengi sana ya hovyo, yanayofanyika nchini kwetu, ambayo hao vijana wa Gen Z wa nchini kwetu, wanayavumilia, lakini naamini, itakapofika mwisho wa uvumilivu wao, wataingia barabarani na kuandamana.
Matatizo hayo ni pamoja na vijana wengi sana wanaomaliza elimu ya vyuo vikuu kila mwaka, kukosa ajira nchini
Vile vile mifumo ya nchi hii ndilo tatizo Kuu linaloliangamiza Taifa letu.
Hii nchi kiuhalisia Haina mipaka ya utendaji wake wa kazi, Kati ya mihimili mikuu 3 ya Dola, ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama.
Katika nchi yetu, serikali, chini ya Rais wa Jamhuri ndiye mhimili Mkuu, ambao Kwa maneno ya Mwendazake John Magufuli kuwa ndiyo mhimili uliojichimbia zaidi chini!
Katika nchi yetu Rais amepewa madaraka makubwa mno ya ki-mungu- mtu, kunakofanya mihimili Ile mingine ya Bunge na Mahakama, isiweze kufanya kazi Kwa uhuru.
Mimi huwa najiuliza hivi kama kweli mihimili hii 3 ingekuwa inafanya kazi Kwa uhuru bila kuingiliwa na mhimili mwingine, hivi ni kwanini wale wabunge 19 wa viti maalum, wanaendelea kuwemo Bungeni Kwa mwaka wa 4 hivi sasa, wakati inafahamika wazi kuwa wabunge hao hawana chama wanachokiwakilisha Bungeni, baada ya Chama Cha Chadema, wanachodai kuwa wao ni wanachama wa chama hiko, kusema kuwa imeshawafukuza zamani sana, tokea mwaka 2020??
Hivi inakuwaje Spika wa Bunge, achukuwe uamuzi wa kumfukuza Mbunge Luhaga Mpina, ambaye amesema kuwa Waziri Bashe amelidanganya Bunge, ambao ni wajibu namba moja wa wabunge wa kuisimamia serikali, wakati alipotoa taarifa ya uagizaji wa sukari, wakati kulipotokea upungufu mkubwa wa sukari, mwishoni mwa mwaka Jana??
Kwa hiyo nimwambie Rais Samia, kuwa vipo viashiria vingi sana, vinavyoweza kusababisha hii Gen Z ya hapa nchini kuweza kuandamana na Wala siyo tuu kwa kukosa sukari, kama alivyotahadharisha Rais Samia Jana, ambako yupo ziarani Mkoani Morogoro.
Mungu ibariki Tanzania