Rais Samia songa mbele, wengine watakushukuru na kuacha kelele za lawama tukifika Kanaani

Rais Samia songa mbele, wengine watakushukuru na kuacha kelele za lawama tukifika Kanaani

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Mh. Rais, najua unatambua kuwa safari ya kuyafikia maendeleo siyo nyepesi, siyo tambalale wala mteremko. Mh Rais sisi watanzania huwa tunalalamika sana linapoanza jambo fulani na kuinua sauti za kelele kila mahali ili mradi tu kila mtu kaongea.

Mh. Rais wetu, umekuwa muwazi sana katika serikali yako, wananchi tunaona miradi mbalimbali ikijengwa kutokanaa na makusanyo ya kodi na tozo zilizopitishwa na kupitia michakato ya kisheria. Tunaona dhamira yako ya dhati katika kuijenga nchi hii, tunaona kuwa unachohitaji ni kuona mwananchi anapata huduma bora zilizo karibu kabisa na watu walipo.

Mh. Rais, tunaona dhamira yako ya kuona hakuna mtanzania anayeachwa nyuma kimaendeleo wala kutengwa, tunaona ikijengwa nchi na uchumi unaomgusa kila mtu na kumnufaisha kila mmoja wetu.

Mh. Rais, najua kelele zitapigwa kwa sasa lakini matunda yake yataliwa na kutufaidisha watanzania wote kwa pamoja. Ni lazima tuwajibike kuijenga nchi yetu, lazima tuanze kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe kwa kuchangia maendeleo yetu wenyewe. Hata hao wa Ulaya walipitia huku, hakuna njia nyingine ya kutufikisha waliko fika kama tusipopitia huku.

Mh. Rais, endelea tu kusimamia kila kinachopatikana ili kisiguswe na mtu yoyote kwa manufaa yake binafsi, na ikitokea akibainika kagusa basi awajibishwe bila huruma wala kumpa nafasi ya pili. Maana atakuwa anachezea jasho la watanzania wanyonge walio amua kuijenga nchi yao kwa mikono yao wenyewe, kwa kuchangia na kujibana kutoka katika vipato vyao ili kujenga kesho iliyo bora zaidi, bila kuwa na mzigo wa madeni kwa nchi yetu.

Mh. Rais, jambo kubwa ninalotaka kukuhakikishia ni kuwa, huku niliko mtaani unakubalika sana na kuungwa mkono sana uongozi wako. Wakulima kwa sasa ni shangwe kwako, hasa katika kipindi hiki ambacho zoezi la kujiandikisha kwa ajili ya kupokea mbolea za ruzuku ukiendelea. Wananchi wanakupongeza kwa kuwa wanaona huduma zikisogezwa karibu yao na kuondolewa adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma.

Songa mbele Mh. Rais wetu, maana kazi ufanyazo zimegusa maisha ya watu hasa wanyonge, ipo siku watu watapiga magoti chini kukuomba msamaha kwa kelele zao za sasa. Maana kwa macho yao hawaoni kwa sasa kule tutakako kuwa kesho kwenye nchi ya asali na maziwa na yenye kutiririsha fursa mbalimbali.
 
Yeye mwenyewe anategemea ajira halafu ndio utegemee akupeleke kwenye nchi ya maziwa na asali?
 
😃😃😃Eti kanani!
Kumbuka kabla ya kufika kanani wengi walifia jangwani.
Sisi hatutaki kufia jangwani. Tunataka kufika kanani tukiwa na nguvu!
Kodi na tozo zaidi ya mara moja kwa kipato hicho hicho kimoja, ni wizi!
 
😃😃😃Eti kanani!
Kumbuka kabla ya kufika kanani wengi walifia jangwani.
Sisi hatutaki kufia jangwani. Tunataka kufika kanani tukiwa na nguvu!
Kodi na tozo zaidi ya mara moja kwa kipato hicho hicho kimoja, ni wizi!
Usijari mkuu tunafika kanani tukiwa wazima na wenye nguvu, tuache tu kunung'unika na kulalamika kwa kutamani kurejea, China wenyewe saiz wanaendesha mgao wa umeme kwa Sasa kufuatia mabwawa ya maji kukauka
 
Mh Rais wetu Amedhamilia kutuinua kiuchumi ndio maana unaona akifanya kazi usiku na mchana

Anafanya kazi usiku na mchana au anasema anafanya kazi usiku na mchana? Ni mafanikio gani alikuwa nayo kabla ya ajira ili tujue ana uwezo huo unaompamba nao hapa?
 
Mh Rais najuwa unatambua kuwa safari ya kuyafikia maendeleo siyo nyepesi na Wala siyo Tambalale Wala mteremko, mh Rais sisi watanzania huwa tunalalamika Sana linapoanza Jambo fulani na kuinua sauti za kelele kila mahali ili mradi tu kila mtu kaongea,

Mh Rais wetu umekuwa muwazi Sana katika serikali yako, wananchi tunaona miradi mbalimbali ikijengwa kutokanaa na makusanyo ya Kodi na Tozo zilizopitishwa na kupitia michakato ya kisheria, Tunaona dhamira yako ya dhati katika kuijenga nchi hii, tunaona namna unachohitaji kuona kuwa mwananchi anapata huduma Bora na karibu kabisa na Alipo mwananchi

Mh Rais tunaona dhamira yako ya kuona hakuna mtanzania anayeachwa nyuma kimaendeleo Wala kutengwa, tunaona ikijengwa nchi na uchumi unaomgusa kila mtu na kumnufaisha kila mmoja wetu,

Mh Rais najua kelele zitapigwa kwa Sasa lakini matunda yake yataliwa na kutufaidisha watanzania wote kwa pamoja, Ni lazima tuwajibike kuijenga nchi yetu, Ni lazima tuanze kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe kwa kuchangia maendeleo yetu wenyewe, hata hao wa ulaya walipitia huku, Hakuna njia nyingine ya kutufikisha waliko fika Kama tusipopitia huku,

Mh Rais Endelea tu kusimamia kila kinachopatikana ili kisiguswe na mtu yoyote kwa manufaa yake binafsi , Na ikitokea akibainika kagusa Basi awajibishwe bila huruma Wala kumpa nafasi ya pili,maana atakuwa anachezea jasho la watanzania wanyonge walio amua kuijenga nchi yao kwa mikono yao wenyewe kwa kuchangia na kujibana kutoka katika vipato vyao ili kujenga kesho iliyo Bora zaid bila kuwa na mzigo wa madeni kwa nchi yetu

Mh Rais Jambo kubwa nalotaka kukuhakikishia Ni kuwa huku niliko mtaani unakubalika Sana na kuungwa mkono Sana uongozi wako, wakulima kwa Sasa Ni shangwe kwako hasa katika kipindi hiki ambacho zoezi la kujiandikisha kwa ajili ya kupokea mbolea za Ruzuku ukiendelea, wananchi wanakupongeza kwa kuwa wanaona huduma zikisogezwa karibu yao na kuondolewa adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma

Songa mbele mh Rais wetu maana kazi ufanyazo zimegusa maisha ya watu hasa wanyonge, ipo siku watu watapiga magoti chini kukuomba msamaha kwa kelele zao za Sasa, maana kwa macho yao hawaoni kwa Sasa kule tutakako kuwa kesho kwenye nchi ya asali na maziwa na yenye kutiririsha fursa mbalimbali
Inabidi wananchi tufanye kitu haraka la sivyo tutaangamia.
 
Back
Top Bottom