Rais Samia, suala la Machinga kuwa nalo makini. Usije ukajichanganya

Rais Samia, suala la Machinga kuwa nalo makini. Usije ukajichanganya

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Ndugu Rais,

Hili suala la wamachinga ni very sensitive nakushauri uende nalo kwa busara kubwa sana.

Nadhani uliona maelfu ya waliotoka mabarabarani kumlilia Magufuli, naweza kusema probably kuwa zaidi ya 70% ni Wamachinga.

Hili ni jeshi kubwa sana ambalo ukilizingua litakuzingua kweli.

Pamoja na mapungufu mengi tu ya mtangulizi wako katika masuala ya uongozi lakini katika vitu alivyotumia akili ni namna ya kudeal na wamachinga. Baada ya mtangulizi wako kugundua kuwa hakubaliki katika cadre ya wasomi na wafanyabiashara wakubwa, aliamua kurudi chini kwenye grassroots na kufanya urafiki na wamachinga. Hawa ndo waliomzika!

Pia tambua kuwa nchi hii ina tatizo kubwa la ajira, shukuru Mungu kuwa kuna namna japo haipendezi ambayo mamilioni ya wananchi wanajipatia riziki yao. Tafadhali usianze kuwadisturb hawa wamachinga, utapata tabu sana kutawala kama kundi hili la mamilioni litakukataa. Na utapata wakati mgumu zaidi wakitokea watu wa kuwasongesha mtaani.

Pia fahamu kuwa kitendo cha kundi hili kuweza kujipatia riziki kulipunguza sana wimbi la ujambazi mitaani. Chondechonde nakuomba Ndugu Samia, usidisturb kabisa kundi hili bali litafutie utaratibu mzuri wa biashara zao bila kuwaswaga ghafla.

Ndugu, Rais ukivunja vibanda vya wamachinga leo, sisi wenye kipato tutakushangilia, lakini kabla hujafanya hilo jiulize hawa wanaopata rizki kutokana na hivyo vibanda wakale wapi?

Ndugu Rais, naongea haya nikiwa mtu ninayependa miji iwe safi kweli, lakini sasa Wenzetu hawa wanahitaji nao mkono kwenda kinywani tufanyeje?

Angalia dissatisfaction isije ikawa kubwa sana mtaani utapata tabu sana kutawala nchi hii.

Ni lazima uendelee kujali watu masikini bila kuumiza Matajiri, Ukiigeuza serikali yako kuwa ya Matajiri na wenye kipato tu bila kuwaangalia walalahoi utafeli

Kuwa Makini sana!
 
Umeongea kistaarabu sana mleta mada.

Ila hawa wafanya biashara ndogo ndogo wanatakiwa waangaliwe kwa jicho la tatu.
Mtindo wao wa kufanya biashara umeharibu kabisa mipangilio ya miji pia kuchafua sana mazingira, vile vile usisahau aina hiyo ya ufanyaji biashara inahatarisha mno maisha yao.

Muhimu serikali ichukue hatua mapema iwekanavyo kwa mujibu wa sheria zilizoko.
Utawala wa Magu ulikosea sana kwenye hili.
 
Njia pekee ya kupunguza idadi ya machinga mijini ni kurudisha hali ya mzunguko wa pesa mtaani, kufungua Milango kwa Wawekezaji, kufungua mipaka watu wauze watakapo.

Ongezeko la machinga mijini chanzo ni mwendazake alipouwa uchumi kwa kusomesha watu namba wawe masikini ili aweze kuwatawala.Aliuwa kilimo,alikimbiza Wawekezaji kwa dhania kila aliyefanikiwa ni mwizi hizi ni fikra za kizamani za kijamaa.
 
Watafutiwe sehemu wakae wateja watawafuata wametapakaa sana, Kariakoo hata pakukanyaga hakuna, barabarani wamejaa hadi kwenye vituo vya abiria hakuna pakusimama, mwendazake hakuwa malaika nae alikuwa anakosea pia.
 
Sidhani kama wanavinjiwa tu bila kupatiwa eneo la kwenda. Kikubwa wapangiwe maeneo maalumu ya biashara zao, na serikali ichukue jukumu la kuweka mazingira hayo sawa kibiashara kwa Wamachinga.
Kama wanaambiwa mwisho tarehe 18, sioni kama kuna maandalizi yamefanyika mapema. Well, tusubiri siku ifike tuone zoezi litakavyoendeshwa.

Hofu yangu zikitokea vurugu sioni kama tunao askari wa kutosha kudhibiti hali bila kusababisha madhara makubwa.
 
Mimi naamini kama sekta binafsi itapewa meno huku serikali ikijitahidi kuajiri hasa elimu na Afya basi Machinga automatically watapungua.

Na kuhusu kwamba Machinga ndio waliompenda, kumlilia Magu sikubaliani na wewe.

Msiba wa Magu umekuwa 'hyped' sana na lililokuwa genge lake. Kuanzia media, wasanii, viongozi wa dini, watu maarufu.

Sasa ni watu wangapi wenye uwezo wa fikra huru kuukwepa mtego huo?

Hilo genge mpaka CAG lilianza kumwona adui wakati anawasiliana ripoti yake.

Watu wengine ni wahanga wa propaganda alizokuwa anafanya miaka yote mitano.
 
Uchumi wa nchi haukuzwi kwa umachinga bali kupitia uzalishaji. Machinga ni wachuuzi yaani ni madalali wa viwanda vya china kwa nia ya kukuza uchumi wa china.97% za wauzavyo machinga ni made in China.

Ukiboresha kilimo wote wakiingia kwenye uzalishaji badala ya uchuuzi uchumi utakua.
 
Tatizo kubwa n kwamba ss binadamu tukiambiwa kufuata utaratibu tunaona kama tunaonewa. Maeneo yametengwa lakin watu hawataki wako radhi waende maeneo ambayo yanaleta kero kwa wengine na wkuondolewa wanalilia kuonewa kitu ambacho sio kabsaa.
 
Back
Top Bottom