Rais Samia Suluhu hakikisha unawapa Watanzania Katiba mpya. Itakupa heshima kubwa sana

Rais Samia Suluhu hakikisha unawapa Watanzania Katiba mpya. Itakupa heshima kubwa sana

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2012
Posts
6,710
Reaction score
9,063
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan(SSH), awali ya yote na kwa moyo wa dhati kabisa nikupongeze kwa kuapishwa kuwa Rais wa 6 wa JMT. Watz wanajua huu ni mpanho wa Mungu.

Wewe ndiye ulikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba,(BMK) mkiwa na marehemu Samwel Sitta. Mchakato ulifanyika, tukapata Rasimu ya Katiba na KATIBA PENDEKEZWA. Kama nakumbuka vizuri zilitumika Fedha za walipa Kodi wa Tanzania takribani Tshs. 270 Billioni.

Hayati JPM alipoingia madarakani yeye akadai swala la KATIBA MPYA halikuwa kipaumbele chake wala halikuwa kwene Ilani ya Uchaguzi!!! Sijui kama halikuwa swala la Ilani ilikuwaje Serikali ya CCM A4 chini ya Mhe. Jakaya Mrisho Kikwerte iliamua kutumia mabilioni yote hayo kuwalaghai Watanzania.

Maadamu wewe sasa ndio uko Ikulu jikoni, ni wakati wa kukamilisha upishi huu au mchakato wa KATIBA MPYA. Napenda niku hakikishie kuwa hiyo itakuwa ni zawadi yako kwa Watanzania itakayo kujengea Heshima kubwa sana! Hakika Itakuwa ni alama utakayo waachia Watanzania na wata kukumbuka daima milele ikizingatiwa kuwa wewe ni Rais Mwanamke wa Kwanza Tanzania tangu tupate Uhuru.

Asalaam Aleikum
 
Shavua Tov Mama Samia Suluhu Hassan, unafanya kazi nzuri, ukirejesha katiba kwa mujibu wa Jaji Warioba utanoga zaidi.

Kwa ufupi mimi nilikuwa mfuasi namba 1 wa Magufuli, lakini alipokengeuka na kuanza kuwaona wapinzani kama maadui, na kila mfanyabiashara ni mwizi nilimchukia sana. Mungu ni fundi alifanya yake, sasa ametupa wewe mama yetu jasiri, kiongozi halisi, mpole, mrembo na una kila sifa ya kuwa Rais hata kwa miaka 10 ijayo, ila bibi wewe kumbuka katiba mpya yenye matakwa ya Wazanzibari na Watanganyika tunaihitaji kuliko kitu chochote kile....

Natumai umenifahamu...
 
Shavua Tov Mama Samia Suluhu Hassan, unafanya kazi nzuri, ukirejesha katiba kwa mujibu wa Jaji Warioba utanoga zaidi.

Kwa ufupi mimi nilikuwa mfuasi namba 1 wa Magufuli, lakini alipokengeuka na kuanza kuwaona wapinzani kama maadui, na kila mfanyabiashara ni mwizi nilimchukia sana. Mungu ni fundi alifanya yake, sasa ametupa wewe mama yetu jasiri, kiongozi halisi, mpole, mrembo na una kila sifa ya kuwa Rais hata kwa miaka 10 ijayo, ila bibi wewe kumbuka katiba mpya yenye matakwa ya Wazanzibari na Watanganyika tunaihitaji kuliko kitu chochote kile....

Natumai umenifahamu...
Maaskofu wameshanza yao atakubali tu hakuna namna
 
Back
Top Bottom