Rais Samia Suluhu Hassan, mteue Zitto Zuberi Kabwe awe Mbunge akaongeze chachu ya hoja Bungeni

Rais Samia Suluhu Hassan, mteue Zitto Zuberi Kabwe awe Mbunge akaongeze chachu ya hoja Bungeni

fundimchundo

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2010
Posts
739
Reaction score
1,032
Bunge letu linahitaji kuongezewa chachu ya aina fulani ili liweze kuichambua kikamilifu Miswada ya Serikali.

Vile vile Bunge letu linahitaji Sauti ya Upinzani yenye kukubalika mbele ya jamii yetu ya Kitanzania.

Kwa kuwa Kada wawili wa CCM wamekuwa Wabunge wa Kuteuliwa, Humphrey Polepole na Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, basi ikimpendeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, itapendeza sana Mhe. Zitto Zuberi Kabwe wa ACT-Wazalendo, akateuliwa kuwa Mbunge, katika zile nafasi za Rais.

Hali hii itaimarisha Muungano wetu kwa kuwa ACT-Wazalendo imekubali kushiriki katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

CCM, kwa upande wa Tanzania Bara, itakuwa imeungana na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika kuonesha dhamira njema ya kushirikiana na makundi yote ndani ya Nchi yetu, katika kuijenga Nchi yetu.
 
Kwa Zito sawa, huyo mpeni huo ubunge wa hisani. Naomba cdm wasiiingie kwenye huu mtego wa vyeo vya hisani, maana wana uwezo wa kupata kura kupitia kwa wananchi kihalali.
Kila nikiliangalia Bunge letu la miaka hii minne iliyobaki, na kauli ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kueleza bayana kuwa Serikali yake iko tayari kukosolewa, Mbunge aina ya Zitto Zuberi Kamwe, mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja, ni faida sana kuwa nawe Bungeni.
 
Kila nikiliangalia Bunge letu la miaka hii minne iliyobaki, na kauli ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kueleza bayana kuwa Serikali yake iko tayari kukosolewa, Mbunge aina ya Zitto Zuberi Kamwe, mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja, ni faida sana kuwa nawe Bungeni.

Kwani ni lazima akosoe akiwa bungeni? Alikuwa huko bungeni miaka 15, kipi kikubwa kilibadalika?
 
Interesting..

Wakati fulani Zitto aliwahi sema atakuwa Rais wa sita Tanzania..
Leo tuna Rais wa Sitta na Zitto anaombewa ubunge wa huruma..

How things can change
Taifa ni kubwa kuliko mtu yeyote mmoja katika kila Nchi.
Zitto Zuberi Kabwe amethibitisha ukweli huo kwa kukubali Chama chake cha ACT-Wazalendo kushiriki katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.
Uwezo wake wa kujenga hoja hauna shaka.
 
Kwani ni lazima akosoe akiwa bungeni? Alikuwa huko bungeni miaka 15, kipi kikubwa kilibadalika?
Kukosoa kwa staha, kwa lugha ya Kibunge, na hoja ikafanyanyiwa kazi na Serikali, kwa mujibu wa Katiba yetu, inabidi awe Bungeni.
Ndiyo, ni vizuri kukosoa ukiwa Bungeni.
 
Kukosoa kwa staha, kwa lugha ya Kibunge, na hoja ikafanyanyiwa kazi na Serikali, kwa mujibu wa Katiba yetu, inabidi awe Bungeni.
Ndiyo, ni vizuri kukosoa ukiwa Bungeni.
Nasema hivi, alikuwa huko bungeni miaka 15, kipi kilibadilika? Kama unamtafutia ulaji sawa, lakini sio kwamba akifika atasikilizwa. Hilo bunge tunalifahamu.
 
Bunge letu linahitaji kuongezewa chachu ya aina fulani ili liweze kuichambua kikamilifu Miswada ya Serikali.
Vile vile Bunge letu linahitaji Sauti ya Upinzani yenye kukubalika mbele ya jamii yetu ya Kitanzania.
Kwa kuwa Kada wawili wa CCM wamekuwa Wabunge wa Kuteuliwa, Humphrey Polepole na Dkt. Bashiru Ally Kakorwa, basi, ikimpendeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, itapendeza sana Mhe. Zitto Zuberi Kabwe wa ACT-Wazalendo, akateuliwa kuwa Mbunge, katika zile nafasi za Rais.
Hali hii itaimarisha Muungano wetu kwa kuwa ACT-Wazalendo imekubali kushiriki katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.
CCM, kwa upande wa Tanzania Bara, itakuwa imeungana na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Alli Mwinyi katika kuonyesha dhamira njema ya kushirikiana na makundi yote ndani ya Nchi yetu, katika kuijenga Nchi yetu.


Kikwazo atakuwa Spika kwani yeye hapendi wabunge design ya Zitto, Lissu, Msigwa,Heche nk, wanaoweza kumkosoa hata yeye.
 
Aongeze wabunge tena, sio kupunguza?
Nchi itapigaje hatua kwa kuwa na wabunge wengi vile, na hakuna cha maana. Kama ni sheria za hovyo zinapitishwa kila leo.
Mama atupe Katiba mpya, hatuna shida ya kuongezewa wabunge. Tukipunguza wabunge kufikia idadi ya watu 70, pesa zitazookolewa hapo zitakwenda kwenye miradi maendeleo na kupunguza idadi ya wanaokosa mikopo ya elimu kutoka HESLB.
 
Kila nikiliangalia Bunge letu la miaka hii minne iliyobaki, na kauli ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kueleza bayana kuwa Serikali yake iko tayari kukosolewa, Mbunge aina ya Zitto Zuberi Kamwe, mwenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja, ni faida sana kuwa nawe Bungeni.
Raisi atakua hajawatendea haki wanakigoma waliomgaragaza huyo zito mchana kweupe. Zito anafaida gani bungeni mbali na ubishiiiii???
 
Raisi atakua hajawatendea haki wanakigoma waliomgaragaza huyo zito mchana kweupe. Zito anafaida gani bungeni mbali na ubishiiiii???
Sina hakika kama WanaKigoma wote watakubaliana na wewe.
Jamii zetu Tanzania zina kundi dogo la Wafiachama, ambalo kwalo Nchi inakuja baada ya Chama.
Kundi hilo dogo linafurahia Wabunge wote watoke CCM, Madiwani wote watoke CCM.
Kwa wale wengi wanaoipenda Nchi yao kuliko Vyama vyao, wanaamini kuwa SAUTI MBADALA Bungeni inaimarisha AFYA ya Taifa.
Sauti ya Zitto Bungeni ni Sauti Mbadala.
 
Aongeze wabunge tena, sio kupunguza?
Nchi itapigaje hatua kwa kuwa na wabunge wengi vile, na hakuna cha maana. Kama ni sheria za hovyo zinapitishwa kila leo.
Mama atupe Katiba mpya, hatuna shida ya kuongezewa wabunge. Tukipunguza wabunge kufikia idadi ya watu 70, pesa zitazookolewa hapo zitakwenda kwenye miradi maendeleo na kupunguza idadi ya wanaokosa mikopo ya elimu kutoka HESLB.
Nakubaliana na hoja yako ya Bunge dogo.
Lakini kwa sasa, Bunge ndilo hili tulilo nalo na Rais anazo nafasi zake za uteuzi.
Humphrey Polepole na Dkt. Bashiru Ally ni wanufaika wa nafasi hizo.
Wote hawa wanaimba wimbo mmoja na Spika Ndugai, Naibu Spika Dkt. Tulia na Wabunge wengine wa Chama cha Mapinduzi.
Taifa linahitaji Sauti Mbadala huko Mjengoni.
Rais Mama Samia akimteua Zitto Zuberi Kabwe, Taifa litaweza kupata Sauti Mbadala iliayo Nyikani.
 
kwanini awe zito tu
Siyo lazima awe Zitto tu, maana hata huko nyuma, Rais Kikwete aliwahi kumteua James Mbatia.
Tuangalie uhalisia.
ACT-Wazalendo inafanya kazi na CCM Zanzibar.
Chadema haiutambui Uchaguzi Mkuu uliopita, inasema ulikuwa Uchafuzi Mkuu.
Na Tanzania yetu ipo na maisha yanaendelea.
Mawazo yangu ni kwamba, kwa kuwa hali halisi ndiyo hii iliyopo, angalau Bungeni iwepo Sauti Mbadala.
Ukiangalia ndani ya ACT-Wazalendo, ni nani anafaa kuwepo Bungeni zaidi ya Zitto Zuberi Kabwe?
 
Interesting..

Wakati fulani Zitto aliwahi sema atakuwa Rais wa sita Tanzania..
Leo tuna Rais wa Sitta na Zitto anaombewa ubunge wa huruma..

How things can change
Unavyozungumza ni as if Zitto mwenyewe kasema anataka ubunge.

Zitto kawa mbunge miaka 15 majimbo mawili.

Hata kama angetaka kugombea Urais, angegombea tu mwaka jana.

Inashangaza kuchukua maoni ya mtu mtandaoni na kuyapachika kwa Zitto halafu anahukumiwa nayo.

Mimi siyo mfuasi wa chama chochote, ila ni wazi Zitto angetaka ubunge angegombea tu maana mpaka sasa kuna majimbo mawili Kigoma yako wazi.
 
Back
Top Bottom