Rais Samia Suluhu Hassan ni kiongozi kwa kuzaliwa

Kama kuongea ukweli Ni kuwa chawa Basi acha niwe chawa wa mh Rais wakuyasema mazuri yote ayafanyayo na yanayokonga nyoyo za watanzania kwa sasa
Alafu unapost ukiwa sebuleni kwa shemeji ukisubili ugali was mchana ule na vitoto vya Dada yako.
 
Hata
Wewe mwqmba kila siku unakuja na uzi mpya wa kumpongeza rais...

Sio kitu kuna bure... Either wewe ni yeye kbsa au utakuwa wa buku 7
Kwani wewe huoni hata Kazi anafanya kila siku mh Rais wetu, kila siku anakiu ya kuona Tanzania Ina kuwa mpya
 
Moja ya sifanayompendea ni hakuna kuyumbishwa na makelele ya wapuuzi,kiufupi sio mtu wa mihemko.

Pili ana uwezo wa ku face na kufanya mambo magumu,refer chanjo na sakata la Ngorongoro,tozo na mafuta.

Tatu ni mtu anayevumilia ukosoaji yaani hana huo mda wa kugombezana hovyo huko na wanaokosoa..

Mwisho naona anajitahidi Sana kutembea kwenye bajeti,sijawahi ona akienda kinyume na haya mambo hata akikabiliwa na pressure kwenye mikutano ya hadhara ya wale jamaa wanaosema mama sema neno moja tuu watu wapone,amekuwa akiwajibu kwamba atalichukua ila kwa sasa uelekeo ni moja mbili tatu.

Mwisho naona ana Nia ya kuleta mageuzi kabisa hapa Tanzania tatizo ni kuwa na watu wenye uwezo wachache huko Serikalini..imagine ajenda yake ya kumtua mama ndio kichwani,kuhakikisha Vijijini vyote vinapitika Kwa barabara,mageuzi ya kilimo na kuwa cha umwagiliaji,mageuzi ya sekta ya ajira,ajenda ya Watalii mil.5 by 2025 na ishu ya Katiba mpya..
 
Mh Rais anafanya kazi kubwa Sana Ni vile tu kwa kuwa wengine mnajipa upofu, embu jaribuni kuona kwa majirani zetu Hali Ilivyo, sisi mh Rais wetu anatoa Hadi Ruzuku
 
Mkuu Lucas mwashambwa iko hivi, Mama yetu, Rais Samia ni kiongozi mzuri mno tena mwenye viwango vya kimataifa. Kinachomrudisha nyuma na kumkwamisha hana wasaidizi. Ninaamini angewasikiliza kidogo watu wake wa Vetting naamini watu kama Makamba, Nape, Mwigulu, Ridhiwani etc wasingekuwepo kwenye hizo nafasi na gharama ya maisha ingekuwa chini na watanzania wangempenda mno. Tatizo lilianzia kwenye chanjo ya korona, kila mtu alimuona kituko. Likaja la machinga hawa hawa akina Makala na wengine wakamhujumu akachukiwa. Akaja huyu Mwigulu tozo. Akaja Makamba kuhakikisha bei ya nishati inapanda. Kama utakumbuka walimdanganya Rais wakamwambia eti ni vita Ukraine, baadaye kelele zilivyozidi wakamdanganya tuweke ruzuku. Akaja nape na gharama za vifurushi etc, Ridhiwani hakupaswa kumpatia nafasi kwa sababu ya rekodi mbaya ya baba yake Dkt Kikwete. Mzee wetu JK hapendwi mno na watanzania kwa sababu ya kupenda kukumbatia watu waovu. Sasa Mama yetu uwezo wake wa kiuongozi unamezwa na maovu mengi yanayotokana na ugumu wa maisha. Wewe kama unatumwa kumsifia hapa JF ili kubadili upepo unajichosha, ni yeye mwenyewe achukue ushauri wetu wana JF aufanyie kazi na uzuri sisi ni wana CCM kindakindaki tunajua ni ngumu kujitokeza hadharani kummsema vibaya mwenyekiti wetu ila hapa JF ni dare to talk openly. Mwambie watanzania wanamchukia mno tena wanatamani aondoke kwenye urais hata leo maana hana msaada kwa watanzania.
 
Hapana natof
Natofautiana na wewe kwa hoja zangu zifuatazo kwa kila hoja zako, kwanza nisema kuwa mh Rais hachukiwi na watanzania Bali anapendwaa na watanzania, kwa kuwa suala la Bei ya vitu siyo kwamba mh Rais amepansisha Bei za vitu Bali suala Hilo limesababishwa na Hali Ilivyo kwa Sasa duniani kwote ambayo Inatuathiri Hadi huku tuliko

Katika kukabiliana na Hilo mh Rais ameamua Kutoa Ruzuku ili kukabiliana na mfumuko wa Bei unaoitesa Dunia kwa Sasa, hivi hata hapa nipo kitongojini kwangu kuandikisha jina kwa ajili ya kuja kunufaika na mbolea za Ruzuku

Kuhusu suala la chanjo ya Corona naomba nikuulize je tumepoteza watanzania wangapi waliopoteza maisha sababu ya Corona, Ni Nini kosa la mama katika juhudi za kupambana Corona, mbona mh Rais alikuwa wazi kabisa juu ya Jambo hili, kwanza alihakikisha Elimu ya kutosha inatolewa juu ya tahadhari tunazopaswa kuchukua kukabiliana na janga la Corona, lakini pia akaleta chanjo ili makundi yaliyokuwa kwenye hatari ya kupata maambukizi kwa ulahisi yapate chanjo mf wazee na watu wenye baadhi ya magonjwa, pia chanjo hii ilikuwa ni hiari na ndio maana hata wewe huku shikiwa mtutu kupata chanjo Bali mtu alichanjwa kwa hiari

Suala la Mh Ridhiwani nalo natofautiana na wewe, kwanza lazima ifahamike kuwa mtu anapewa uongozi na cheo kutokanaa na sifa za kiuongozi alizonazo mhusika, hatuwezi kumpa mtu uongozi kutokanaa na jina au historia ya baba yake aidha kwa kutenda vyema au vizuri wakati wa uongozi wa mzazi wake, tukifanya hivyo itakuwa Ni Jambo la hatari maana tuliotokea katika familia maskini hatuwezi kuwa viongozi, Naamini mh Ridhiwani kikwete anazo sifa kuwa katika eneo aliloaminiwa na mh Rais wetu Kama Naibu waziri wa Aridhi


Kuhusu suala la machinga hivi wewe ilikuwa huoni namna machinga walivyokuwa wanapanga Hadi barabarani, huoni kuwa ilikuwa hatari kwa machinga wetu ikitokea gari limeferi breki, huoni hata magari yalikuwa hayapati nafasi ya kupita vyema, mh Rais aliliona Hilo na akaagiza halmashauri ziwatengee maeneo mazuri machinga ambayo watafanya biashara vizuri na ambayo yanafikika vizuri na watu, lakini pia changamoto zilizokuwa zinajitokeza zilikuwa zinafanyiwa kazi kwa kushirikiana na viongozi wa machinga wa eneo husika maana walikuwa wanashirikishwa kila hatua
 
Alafu unapost ukiwa sebuleni kwa shemeji ukisubili ugali was mchana ule na vitoto vya Dada yako.
Naposti nikiwa hapa kujiandikisha jina ili nije kupata mbolea ya Ruzuku ambayo mh Rais ametoa billioni Mia moja hamsini
 
Una unyani (epidomia)
Hata ukinitukana Mimi siwezi kunitukana maana Namheshimu kila mtu ikiwepo wewe, Naheshimu utu wa mtu na Kamwe siwezi nikakudhalilisha hata ukinitukana, Giza haliondolewi kwa Giza Bali kwa mwanga, chuki haiondolewi kwa chuki Bali kwa upendo,
 
Kiongozi wa watu vs Mapaka👇😁😁😁
Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
 
Hata ukinitukana Mimi siwezi kunitukana maana Namheshimu kila mtu ikiwepo wewe, Naheshimu utu wa mtu na Kamwe siwezi nikakudhalilisha hata ukinitukana, Giza haliondolewi kwa Giza Bali kwa mwanga, chuki haiondolewi kwa chuki Bali kwa upendo,
Yaani wenzio wanalia kibano kila kona we unaleta huu upuuzi... mnakera mno.
 
Yaani wenzio wanalia kibano kila kona we unaleta huu upuuzi... mnakera mno.
Kwani wewe huoni juhudi za mh Rais, Ni nchi gani kwa Sasa ambako wananchi wake wanaishi Raha mstarehe, uchumi wa Dunia umeyumba kwa Sasa baada ya mapito ya Corona na Vita vya Ukraine yaliyo itikisa uchumi wa Dunia, juhudi za mh Rais ndio unaona akitoa Hadi Ruzuku
 
Utakua uta...pakul bladifaken
 
Umekutana na somo linalopaswa kuigwa na viongozi wengi kutoka kwa mh Rais kuwa wanatakiwa wajuwe kuwa ukiwa kiongozi unapaswa kuwa mnyenyekevu na uombe hekima na busara toka kwa Mwenyezi Mungu katika kuongoza watu
Hekima za kunyonya watu masikini na visenti vyao??
 
Unaota mchana
 
Hekima za kunyonya watu masikini na visenti vyao??
Nchi yetu itajengwa na sisi wenyewe watanzania, hatuna.mjomba tunayeweza tukasema tumsubir aje kutujengea vituo vya Afya,shule,zahanati,Barabara, usambazaji wa maji na umeme, unazani huyo mjomba yeye atatoa hela wapi, au unataka wananchi wake walipe Kodi ndio tuje tupewe sisi, hapana lazima tuanze sisi na atakaye taka kutusaidia atatukuta tunaendelea kuijenga Tanzania yetu
 
Hekima za kunyonya watu masikini na visenti vyao??
Nchi yetu itajengwa na sisi wenyewe watanzania, hatuna.mjomba tunayeweza tukasema tumsubir aje kutujengea vituo vya Afya,shule,zahanati,Barabara, usambazaji wa maji na umeme, unazani huyo mjomba yeye atatoa hela wapi, au unataka wananchi wake walipe Kodi ndio tu tupewe sisi, hapana lazima tuanze sisi na atakaye taka kutusaidia atatukuta tunaendelea kuijenga Tanzania yetu
 
Huyu ndie anafaa kuitwa Kiongozi waliobakia wote ni Ma-Rais......


Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…