MANYORI Jr
JF-Expert Member
- Mar 25, 2012
- 462
- 343
Tangu utawala wa Mh. Hayati Dr. John Magufuli uingie mwaka 2015 huo ndio ukawa mwisho wa ajira kwa walimu wa Arts.
Kwa heshima kubwa na taadhima ninakuomba Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan uwaajiri. Idadi yao ni kubwa kwa sababu walitengwa kwenye mfumo wa ajira tangu mwaka 2015 hadi sasa. Jitahidi sana Mh. Rais, hali ya watu hawa ni dhoofu kupita maelezo. Umasikini umewapiga vilivyo tangu wahitimu. Shule binafsi wamejaa ndugu na watu wasio na sifa ila ukaribu na wamiliki au wakuu wa shule hizi na pana hadi ubaguzi wa dini na jinsia!
Kwa kweli Mh. Rais ninakosa maneno sahihi ya kuelezea hali za wahitimu wa shahada za ualimu masomo ya Arts. Ni fedheha kubwa.
Wasomi hawa wanaonekana kama walifeli chuo, maisha yamewapiga vilivyo. Inatosha! Kama ni adhabu walipewa inatosha! Wamejifunza inatosha Mh. Rais. Sema neno moja tu na roho za watu hawa zitapona.
Mh.Kikwete aliwaajiri hadi 42,000 kwa mkupuo kila mwaka bila kujali masomo yao! Wewe pia unaweza.Hali ya maisha imekuwa ngumu wakati watu waliwekeza huko, mama ona namna.
Wasitokee wakukudanganya kama kina Jafo na wenzake kuwa walimu wa masomo haya wapo wengi wanatosha kwa hiyo hakuna uhaba. Waongo! Waongo wakubwa! Walimdanganya hata Mh. Hayati Magufuli na bila kujiridhisha akasitisha kuwaajiri hadi mauti yamemkuta.
Maisha yameenda kasi sana kwa muda wote ambao vijana hawa watoto wa masikini hawana ajira. Hadi sasa, hawana hata familia tu imekuwa shida. Wametengwa na ndugu na jamaa na wengine wameamua kujiua kuepuka fedheha katika jamii.
Rais Samia Suluhu waokoe. Kama wengine wanavyoajiriwa, walimu wa masomo ya arts pia waajiriwe!
Ahsante sana Mama Samia. Imani yangu kwako ni kubwa kuliko hofu niliyonayo juu yako.
Kwa heshima kubwa na taadhima ninakuomba Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan uwaajiri. Idadi yao ni kubwa kwa sababu walitengwa kwenye mfumo wa ajira tangu mwaka 2015 hadi sasa. Jitahidi sana Mh. Rais, hali ya watu hawa ni dhoofu kupita maelezo. Umasikini umewapiga vilivyo tangu wahitimu. Shule binafsi wamejaa ndugu na watu wasio na sifa ila ukaribu na wamiliki au wakuu wa shule hizi na pana hadi ubaguzi wa dini na jinsia!
Kwa kweli Mh. Rais ninakosa maneno sahihi ya kuelezea hali za wahitimu wa shahada za ualimu masomo ya Arts. Ni fedheha kubwa.
Wasomi hawa wanaonekana kama walifeli chuo, maisha yamewapiga vilivyo. Inatosha! Kama ni adhabu walipewa inatosha! Wamejifunza inatosha Mh. Rais. Sema neno moja tu na roho za watu hawa zitapona.
Mh.Kikwete aliwaajiri hadi 42,000 kwa mkupuo kila mwaka bila kujali masomo yao! Wewe pia unaweza.Hali ya maisha imekuwa ngumu wakati watu waliwekeza huko, mama ona namna.
Wasitokee wakukudanganya kama kina Jafo na wenzake kuwa walimu wa masomo haya wapo wengi wanatosha kwa hiyo hakuna uhaba. Waongo! Waongo wakubwa! Walimdanganya hata Mh. Hayati Magufuli na bila kujiridhisha akasitisha kuwaajiri hadi mauti yamemkuta.
Maisha yameenda kasi sana kwa muda wote ambao vijana hawa watoto wa masikini hawana ajira. Hadi sasa, hawana hata familia tu imekuwa shida. Wametengwa na ndugu na jamaa na wengine wameamua kujiua kuepuka fedheha katika jamii.
Rais Samia Suluhu waokoe. Kama wengine wanavyoajiriwa, walimu wa masomo ya arts pia waajiriwe!
Ahsante sana Mama Samia. Imani yangu kwako ni kubwa kuliko hofu niliyonayo juu yako.