Rais Samia Suluhu tupunguzie mateso, tumecheleweshwa sana ajira mpya

Rais Samia Suluhu tupunguzie mateso, tumecheleweshwa sana ajira mpya

Samiaagain2025

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2020
Posts
3,626
Reaction score
3,869
"SIKIA SAUTI YA WANYONGE':

Tangu awamu ya mheshimiwa hayati Magufuli ilipoanza,mfumo wa ajira ulipinduliwa.

Tulikuwa tunategemea kila mwaka ajira zipo hasa kwa idara ya afya,walimu, na kilimo na mifugo.

Tangu mwaka 2015,tupo mtaani tunahangaika,Tena sisi wanufaika wa HESLB tunazalishiwa deni kila mwaka
(Retention fee)

Hivi mtu umemaliza chuo mwaka 2015 ukitegemea mwaka 2016 utaajiriwa, halafu bado upo mtaani!
Si utakuwa umeharibiwa mipango mingi sana,ikiwemo ya kijamii(ndoa,
n.k),kiuchumi na hata kisaikolojia.

Bora kama hakuna pesa, mtuajiri sisi ambao tuliokuwa tayari tumechagua kazi za kusomea kabla ya awamu ya tano(2015,2016 na 2017),maana tungejua hakuna ajira tusingesoma au tungesomea kazi zingine!

Ila tunaamini kwa serikali ya mheshimiwa rais Samia Suluhu Hassan,tutaajiriwa. Japo tunaumia kusikia mtanzania mwenzetu anakaa na dola za kimarekani 1.6+ milioni nyumbani kwake(pesa ya umma),huku sisi hatuna ajira.

Tunakuomba mama Samia, tuhurumie na sisi wahitimu wa vyuo, especially 2015,2016,na 2017.

NB; Ni ombi tu lakini.


By Sauti ya wanyonge
Tanzania.
 
Usitegemee kumaliza masomo ndo uajiriwe, find means za kuishi usitegemee serikali kukidhi utoaji wa ajira kwa wahitimu wote nchi hii, elimu uliyopata changanya na za kwako.
 
Kwa kweli ukosefu au upungufu wa ajira ni tatizo kubwa sana. Vijana msife moyo, jaribuni kujishughulisha na shughuli ndogo ndogo za kujiingizia kipato
 
Usitegemee kumaliza masono ndo uajiriwe, find means za kuishi usitegemee serikali kukidhi utoaji wa ajira kwa wahitimu wote nchi hii, elimu uliyopata changanya na za kwako......................
Nyie hamuaminiki.
Kwa vile familia zenu ndo zile za akina KAKOKO au MO Dewji,Basi mnachukulia masuala juujuu tu.Okay.
 
Kwa kweli ukosefu au upungufu wa ajira ni tatizo kubwa sana. Vijana msife moyo, jaribuni kujishughulisha na shughuli ndogo ndogo za kujiingizia kipato
Kipato 300000 kwa mwezi,HESLB-15% income tax,NSSF-10%,
Bado wategemezi,n.k,

Utaweza kuishi ?
 
Watanzania inabidi tusisubiri ajira za serikali. Tufungue miradi zaidi mpaka leo hii kuna upungufu wa ngano, sukari, mafuta lakini unataka upate ualimu ambao pesa yenyewe ni ndogo badala ya kuwekeza.
 
Hili suala la serikali kuajiri wafanyakazi ni suala la kimahitaji zaidi kuliko tunavyojaribu kuliweka liwe la "kisiasa "

Serikali lazima itoe ajira kwasababu ni hitaji la ulazima kwaajili ya kuwezesha na kuongeza ufanisi wa shughuli zake za kila siku.

Tanzania na dunia kwa ujumla mambo yanaenda kasi sana na mabadiliko makubwa yanaendelea kutokea kila siku, hivyo idadi ya watumishi waliopo miaka mitano iliyopita haiwezi kuwa na ufanisi ule ule kwa kulinganisha na mabadiliko yanayotokea kwenye sekta mbalimbali kwa sasa.

Ajira za kupeana vimemo na connection zinatoa suluhisho la muda mfupi, ila ili tuwe na ufanisi mzuri serikalini, sula la kutoa ajira za mkupuo ni muhimu at least hata kwa interval ya miaka miwili angalau...

Tunalalamika serikalini huduma mbovu ila tatizo ni nguvu kazi na rasilimali watu nao pia ni changamoto.. Huwezi kuwa na miradi lukuki ila wasimamizi huna!! Unategemea nini??
 
Watanzania inabidi tusisubiri ajira za serikali. Tufungue miradi zaidi mpaka leo hii kuna upungufu wa ngano, sukari, mafuta lakini unataka upate ualimu ambao pesa yenyewe ni ndogo badala ya kuwekeza.
Inaelekea wewe upo kwenye ajira ya serikali. Ndiyo maana unajibu bila kufikiria vizuri.
Hizo sukari na ngano unaanzishaje miradi yake? Unahitaji pesa(mtaji),
I doubt about your education level.

Halafu ukute wewe ni mwalimu,au baba na mama zako!
Au hata ni kiongozi wa serikali.
Daaaaaa!!!!!
 
Hili suala la serikali kuajiri wafanyakazi ni suala la kimahitaji zaidi kuliko tunavyojaribu kuliweka liwe la "kisiasa "

Serikali lazima itoe ajira kwasababu ni hitaji la ulazima kwaajili ya kuwezesha na kuongeza ufanisi wa shughuli zake za kila siku....
Salute for your high view.
 
Salute for your high view.
Juzi tu hapo Mheshimiwa Raisi akipokea ripoti ya CAG aligusia suala la uchache wa watumishi katika ofisi ya CAG..

Pia alikiri kabisa anajua kuwa uchache wa watumishi katika ofisi ya CAG unakwamisha ufanisi katika utendaji wake CAG na akamsihi ajitahidi tu hivyohivyo.

Sasa leo hii tunalalamika tuna uchache wa AUDITORS lakini kitaani tuna watu kibao wanahaha kujitolea katika private firm za wahindi kama cheap labour, wakati kiuhalisa tulikuwa na uwezo wa kuwapa ajira serikalini ili wakaongeze ufanisi katika kusimamia miradi yetu na mashirika yetu.
 
Hello JF,

Hongera mama Samia kuwa kiongozi wetu mpya.

Swala la ajira kwanza hamna evidence kuwa lilikua tatizo kubwa kipindi cha Magufuli.

Ila hata hivyo kuna tatizo la documentation kwa mfano data zilizopo hazionyeshi specific kati ya wangapi wahitimu walipata ajira.

So kwa vile malalamiko ni mengi kati ya wahitimu na wengine tumeishi nao,then tatizo lipo hata kama data hazisemi hivyo.

Mimi nakuomba mama hili liwe moja ya matatizo ya awali utakayotatua.

Kama unaweza tenga fungu special kwa ajili ya ku deal na hili tatizo.

Kuwe na incentives paid kwa employers watakaoajiri mhitimu wa miaka mitano nyuma.

Priority iwe kwa wale waliohitimu zamani kwa sababu wamekaa muda mrefu kwenye hali ngumu ya kutokua na ajira.

Kingine unachoweza kufanya kama huna enough funds.

Ni kuweka mfuko maalumu wa dharula watu wachangie.

Wapewe wahitimu wanaotaka kujiajiri/hii iwe ya wazamani na wa sasa wanaotaka kujiajiri

Yeyote atakayeandika proposal nzuri itakayowasadia vijana/watu wengine kupata ajira then wapewe priority.

Mengine wana JF changieni ipi unadhani ni njia ya kutatua hili swala la ajira ambalo linawezekana kufanyika ndani ya muda mfupi ujao, ku-rescue wahitimu ambao hawana ajira?

Mods naomba msiunganishe hii.

Becky...
 
subiri may mosi umpime uelekeo wake ikiwa ni mtu wa kujali maslahi ya vijana na watumishi au ni yule msema kweli mpenzi wa Mungu huku akielekeza fedha kwenye "structures" kama alivyopenda kuiita yeye.
 
Hello JF,

Hongera mama Samia kuwa kiongozi wetu mpya..
Sister hili ni tatizo kubwa lakini inaonyesha serikali imelala na haijishushulishi kulitatua. Siku wapinzani wakiidaka hii na kuifanya moja ya ajenda zao kuu ndiyo utaona inaamka na kuanza kutoa matamko uchwara.

Nimefurahi hapo uliposema wale wenye njia nzuri ya kufanya watu wengi wapate ajira wapewe kipaumbele. Hii inaweza saidia sana.
 
Back
Top Bottom