Rais Samia: Tanzania tuna madini mengi kiasi ambacho mengine hatujui yanaitwaje

Rais Samia: Tanzania tuna madini mengi kiasi ambacho mengine hatujui yanaitwaje

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu ameibariki neema nyingi sana.

Amesema hayo wakati akitoa hotuba yake kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya WAWATA (Wanawake Wakatoliki Tanzania) iliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 11, 2022.

“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.

Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu ameibariki neema nyingi sana.

Amesema hayo wakati akitoa hotuba yake kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya WAWATA (Wanawake Wakatiliki Tanzania) iliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 11, 2022.

“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.

Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
Wote walisema hivyo, isipokuwa Mwalimu aliyepeleka vijana kutafuta maalifa ya kuyafukua madini hayo na akaanzisha STAMICO.
 
Yawezekana kuna uhusiano hasi kati ya akili na madini. Nchi nyingi zenye madini hazina akili za kunufaika na hayo madini.Mwisho tunaishia kujiita matajiri lakini mfukoni teee!
 
Hizo ni siasa tu za kutafuta kuwashushia watu munkari. Yeye kama kiongozi amefanya nini kuhakikisha nchi inanufaika na hayo madini ambayo mengine hatujafahamu hata majina.

Kuna nchi ambazo hazina hayo madini lakini wako vizuri kutuzidi na tofauti yao na sisi ni kama usiku na mchana.

Hayo madini hata uwe nayo kila kaya lakini kama una chama ambacho lengo lake kuu ni kung'ang'ania madarakani pasipo na mikakati ya kuendeleza taifa ni kazi bure tu.
 
Kuna kitu kinaitwa laana ya rasilimali(resource curse) na ugonjwa wa kidachi(dutch disease). Hayo ni matitizo ambayo huzikumbuka nchi nyingi zenye rasilimali zikikosa watu smart kusimamia hizo rasilimali.
Yawezekana kuna uhusiano hasi kati ya akili na madini. Nchi nyingi zenye madini hazina akili za kunufaika na hayo madini.Mwisho tunaishia kujiita matajiri lakini mfukoni teee!
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu ameibariki neema nyingi sana.

Amesema hayo wakati akitoa hotuba yake kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya WAWATA (Wanawake Wakatiliki Tanzania) iliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 11, 2022.

“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.

Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
Magu alikuwasawa kusema makinikia yasisafilishwe
 
"Tatizo ni namna ya kuyatumia"

Hiyo kauli nayo ni tatizo, kwamba Rais anamaanisha Mungu ametupa "wajinga" madini ambayo hatujui namna ya kuyatumia ili kuliondoa hili taifa kwenye lindi la umaskini?

Nyerere aliwahi kutoa kauli inayofanana na hiyo miaka mingi iliyopita, akiwaasa wenzie huko CCM wayaache hayo madini mengi ardhini mpaka pale watanzania wakiwa na uwezo wa kuyachimba wenyewe, akapuuzwa.

Lakini, kauli kama hiyo inaporudiwa leo, zaidi ya miaka thelathini baadae inaonesha tatizo sio ujinga wa watanzania, bali tatizo ni ujinga wa viongozi wa CCM, hawa ni wabinafsi na walafi, muda wote wanawaza 10%.

Ndio maana wanasababisha taifa lisione faida ya kuwa na madini licha ya kuwa na wasomi wengi kuliko wakati ule Nyerere alipoitoa hiyo kauli kwa mara ya kwanza.

Sasa namshauri Rais wetu afuate ule ushauri wa Nyerere alioutoa miaka ile, kwamba, viongozi wa serikali ya CCM wayaache hayo madini yabaki ardhini mpaka pale ujinga wao utakapoondoka kwenye vichwa vyao, ili wasizidi kulitia hasara taifa.
 
Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
Hapa ndipo anapoonyesha dhahiri udhaifu wake wa kuwa kiongozi.
Haya mambo ndiyo anayopashwa kuwa anayafanyia kazi sasa hivi, badala ya kuimba nyimbo zisizoeleweka.
Anadhani ni nani atakayeleta mabadiliko hayo kama siyo yeye na serikali yake?
 
Back
Top Bottom