Rais Samia: Tanzania tuna madini mengi kiasi ambacho mengine hatujui yanaitwaje

Rais Samia: Tanzania tuna madini mengi kiasi ambacho mengine hatujui yanaitwaje

hahahahaha kuwa madini ni suala lingine na kuyachimba ni suala nyingine.

Hakuna jambo zuri na muhimu kama taifa kuwa na watu wakutosha wenye maarifa yakutosha.
 
Yawezekana kuna uhusiano hasi kati ya akili na madini. Nchi nyingi zenye madini hazina akili za kunufaika na hayo madini.Mwisho tunaishia kujiita matajiri lakini mfukoni teee!
Yani mfukoni mbongo teee, ni kukamuana tozo tu,
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu ameibariki neema nyingi sana.

Amesema hayo wakati akitoa hotuba yake kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya WAWATA (Wanawake Wakatiliki Tanzania) iliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 11, 2022.

“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.

Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
Hili nalo mkalitizame
 
“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.
"Neema ambayo MUNGU ameumba hapa duniani... Tuyatumie maumbile haya kwa maendeleo yetu.. Asanteni sana kwa kunisikiliza.. Kristuuuuu.. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania... Asanteni sana WAWATA.."

In SSH Voice
 
Si wayaite tozonia!
Au mengine ndio yale yenye majina ya mwigulu nchemba rais 2015?
Mbona majina ni mengi tu.

Waache kutukata tozo!

Tozo ni wizi!
 
Mtangulizi wake alikuwa anayajua yote na mahali yalipo na thamani yake. Ye kama hajui basi hatoshi.
 
"Tatizo ni namna ya kuyatumia"

Hiyo kauli nayo ni tatizo, kwamba Rais anamaanisha Mungu ametupa "wajinga" madini ambayo hatujui namna ya kuyatumia ili kuliondoa hili taifa kwenye lindi la umaskini?

Nyerere aliwahi kutoa kauli inayofanana na hiyo miaka mingi iliyopita, akiwaasa wenzie huko CCM wayaache hayo madini mengi ardhini mpaka pale watanzania wakiwa na uwezo wa kuyachimba wenyewe, akapuuzwa.

Lakini, kauli kama hiyo inaporudiwa leo, zaidi ya miaka thelathini baadae inaonesha tatizo sio ujinga wa watanzania, bali tatizo ni ujinga wa viongozi wa CCM, hawa ni wabinafsi na walafi, muda wote wanawaza 10%.

Ndio maana wanasababisha taifa lisione faida ya kuwa na madini licha ya kuwa na wasomi wengi kuliko wakati ule Nyerere alipoitoa hiyo kauli kwa mara ya kwanza.

Sasa namshauri Rais wetu afuate ule ushauri wa Nyerere alioutoa miaka ile, kwamba, viongozi wa serikali ya CCM wayaache hayo madini yabaki ardhini mpaka pale ujinga wao utakapoondoka kwenye vichwa vyao, ili wasizidi kulitia hasara taifa.
Wenzetu Botswana wana uzoefu kwenye masuala ya madini na wameendelea kwa kutumia rasilimali hiyo.

Pia SADC ipo, hivyo twahitaji ushirikiano tu.

Tatizo la baadhi yetu sisi waafrika kujiona twafahamu kila kitu kumbe tupo nyuma sana kwenye tasnia ya kufikiri kwa undani.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu ameibariki neema nyingi sana.

Amesema hayo wakati akitoa hotuba yake kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya WAWATA (Wanawake Wakatoliki Tanzania) iliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 11, 2022.

“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.

Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
Kwa miaka 60 hatujatumia rasilimali zetu kutuondolea umaskini .
tatizo watawala siku zote hutumia nguvu nyingi kupambana na vyama vya upinzani, na wanaharakati wenye mawazo na sera mbadala.
 
Tatizo letu watanzania ujuaji na uvivu umekithiri sana. Hii kasumba kama hatutaiacha basi kizazi chetu kitabakia nyuma Kwa Karne ijayo. Mh Rais amemaanisha kuwa Sisi tu matajiri na utajiri wetu tunaweza kunufaika nao kupitia masoko yaliyopo nk. Tozo ni lazima tutoe na labda jambo la muhimu hapo ni kutizamwa upya viwango ukizingatia na Hali halisi ya maisha ya watanzania Kwa Sasa. Mama yetu anapambana kuhakikisha nchi inapona majeraha ya mdororo wa uchumi duniani Sisi tumekalia makelele tu.
 
Hapo kimeelewa tu maumbile yetu tuliyojaliwa na mwenyezi Mungu tuyatumie kwa maendeleo yetu
 
Nadhani madini ya tozo ndiyo mengi zaidi,tuendelee kuyachimba tu.
 
Ipo siku atakuja mtawala atasema madini yote yameisha.
Hapo ndipo tutakapoelewa siasa ni kitu gani.
Machimbo mengi ya dhahabu yanavumbuliwa na wachimbaji wadogo. Baada ya muda anapewa mwekezaji feki, anakopea hela anafanyia mambo yake, migodi inasimama haindelezwi na mrabaha hakuna. Mwisho tutaambiwa madini yametoweka
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suhulu Hassan amesema kuwa Tanzania ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu ameibariki neema nyingi sana.

Amesema hayo wakati akitoa hotuba yake kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya WAWATA (Wanawake Wakatoliki Tanzania) iliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, Septemba 11, 2022.

“……Tanzania ni nchi nzuri. Tuna mambo mengi ya kujivunia, tunaweza kufanya biashara popote kupitia bandari ya Dar es salaam, tuna maziwa, mito na ardhi yenye rutuba kubwa. Tuna madini ambayo mengine hata hatujui majina yake. Tatizo ni namna gani ya kutumia” amesema Rais.

Rais amesema kuwa anayo matumaini makubwa kuwa kadri muda unavyokwenda, Tanzania itaweza kujisimamia vizuri pamoja na kuzitumia rasilimali hizi kwa ufanisi na manufaa makubwa kwa nchi.
Tuna madini mengi lakini tunategemea tozo
 
"Tatizo ni namna ya kuyatumia"

Hiyo kauli nayo ni tatizo, kwamba Rais anamaanisha Mungu ametupa "wajinga" madini ambayo hatujui namna ya kuyatumia ili kuliondoa hili taifa kwenye lindi la umaskini?

Nyerere aliwahi kutoa kauli inayofanana na hiyo miaka mingi iliyopita, akiwaasa wenzie huko CCM wayaache hayo madini mengi ardhini mpaka pale watanzania wakiwa na uwezo wa kuyachimba wenyewe, akapuuzwa.

Lakini, kauli kama hiyo inaporudiwa leo, zaidi ya miaka thelathini baadae inaonesha tatizo sio ujinga wa watanzania, bali tatizo ni ujinga wa viongozi wa CCM, hawa ni wabinafsi na walafi, muda wote wanawaza 10%.

Ndio maana wanasababisha taifa lisione faida ya kuwa na madini licha ya kuwa na wasomi wengi kuliko wakati ule Nyerere alipoitoa hiyo kauli kwa mara ya kwanza.

Sasa namshauri Rais wetu afuate ule ushauri wa Nyerere alioutoa miaka ile, kwamba, viongozi wa serikali ya CCM wayaache hayo madini yabaki ardhini mpaka pale ujinga wao utakapoondoka kwenye vichwa vyao, ili wasizidi kulitia hasara taifa.
Nakuunga mkono kwa [emoji817]
 
Back
Top Bottom