Rais Samia toa kauli zenye nguvu na zilizo bayana

Rais Samia toa kauli zenye nguvu na zilizo bayana

Mnataka afoke foke kama yule kichaa aliyekuwa mtaani kwenu.
Sio afoke bali atoe maagizo yanayoeleweka. Kama sisi huku bado hatujamuelewa hao watendaji watatekeleza nini? Anasema "wamachinga wapangwe vyema" jiulize kuwapanga vyema ndio vipi wakati wanamaeneo rasmi tayari, ni ama atoe amri ya kuwaondoa au awaache sio kutoa maagizo yasiyoeleweka.
 
Kwa kauli hizi na hayo maagizo yakishindwa kutekelezeka watu wakimwona Mama yetu kama ni "dhaifu" watakuwa wanakosea au watakuwa sawa?
Mkuu Wamachinga lazima waondoke katikati ya miji yote nchini. Ni suala la muda tu.
 
Jamaa anahisi mbinu ni kusubiria kura za wamachinga😅!!! CCM ina mbinu nyingi mbadala ndio maana still iko madarakani
Na ndio maana ukianza habari za katiba wa warioba ni sawa na kuwashika makalio watakavyokushambulia!!
 
Sio afoke bali atoe maagizo yanayoeleweka. Kama sisi huku bado hatujamuelewa hao watendaji watatekeleza nini? Anasema "wamachinga wapangwe vyema" jiulize kuwapanga vyema ndio vipi wakati wanamaeneo rasmi tayari, ni ama atoe amri ya kuwaondoa au awaache sio kutoa maagizo yasiyoeleweka.
Maeneo rasmi kwenye barabara za gari na njia za waenda kwa miguu? Kama hamjamuelewa endeleeni na shughuli zenu ipo siku mtamuelewa.
 
Maeneo rasmi kwenye barabara za gari na njia za waenda kwa miguu? Kama hamjamuelewa endeleeni na shughuli zenu ipo siku mtamuelewa.
Hujanielewa, point yangu ni kwamba tayari wanamaeneo rasmi kwamba wakitolewa humo barabarani ndio wataenda huko sasa hii kauli ya kuwapanga vyema ina maana gani? Je ina maana kwamba wafunge mitaa kama alivyosema mkuu wa mkoa, wakae barabarani lakini isiwe karibu maduka au wawaelekeze barabara za kufanya biashara. Yeye anatakiwa aseme wamachinga waondolewe au wabaki lakini sio stori za kuwapanga vyema.
 
Sio afoke bali atoe maagizo yanayoeleweka. Kama sisi huku bado hatujamuelewa hao watendaji watatekeleza nini? Anasema "wamachinga wapangwe vyema" jiulize kuwapanga vyema ndio vipi wakati wanamaeneo rasmi tayari, ni ama atoe amri ya kuwaondoa au awaache sio kutoa maagizo yasiyoeleweka.
This is what we are talking about..

Atoe kauli iliyonyooka ili hata hao machinga wajiandae kisaikolojia seriously coz wataona hawana mtu wa kuwatetea kwenye hili kama msimamo wa Rais ni dhabiti kwamba lazima waondoke kwenye sehemu zote zisizokuwa rasmi.
 
Tangu lini ccm wanategemea kura zilizopigwa na wananchi?!!tena wamachinga?!!unatania wewe
Hao wamachinga hata kupiga kura tu huwa hawaendi achilia mbali kuwa kura za Watanzania sio greenlight ya CCM kuingia Ikulu.
 
hapo ndipo tatizo lilipo; Chama gani kitakachopishwa na CCM iwapo vyama vyenwe ndiyo hivi. Hata kama CCM ingeendelea kuwa Madarakani, iwapo vyama vya upinzani vingekuwa na nguvu, haingefanya hayo yanayolalamikiwa. Zamani sana ilikuwa mtu akionekana na nguo za kijani za CCM anazomewa, leo hii hali siyo hivyo.
True..vyama vya upinzani inabidi wajipange watengeneze watu aisee..CDM ya kina Slaa sio hii ya sasa,hii ya sasa imeparanganyika vibaya mno hata tukisema waingie ikulu itakuwa ni utani aisee.
 
Huu upuuzi ulidhibitiwa vizuri kipindi cha JK hadi wakawa wanajengewa masoko ila yule mwehu wa huko mapolini alivyokuja akaulea mpaka inaonekana as if ni utaratibu rasmi kwa maelezo eti ni wapiga kura wake..
Kipindi cha Jk miji ilikuwa safi sana..

Jiwe kuruhusu huu uholela inaonyesha tu ni kiasi gani alikuwa hafai kuwa kiongozi mkuu wa hii nchi..anyway,aendelee kupumzika vyema.
 
Ni vyema Rais Samia wakati wa kutoa maelekezo yake awe anakuwa wazi nini hasa anataka na atoe kauli zenye nguvu ili ujumbe ufike kwa nguvu pia kwa wahusika wote wa pande mbili.

Leo wakati anatoa hotuba yake mara baada ya kuwaapisha Mawaziri na Mwanasheria mkuu wa Serikali alitoa neno kuhusu hili saga la Wamachinga linaloendelea.

Ameonesha hafurahishwi na biashara hiyo inavyofanyika kiholela na inavyovuruga biashara zinazolipa kodi. Lakini aka sugar-coat maneno yake na sijajua ni intentionally au accidentally..Mhe.Rais amesema wapangwe na nguvu isitumike,watolewe kwa amani.

Kitu ambacho hakiwezekani kirahisi hivyo kwa hawa watu na pia kauli hiyo inawapa watekelezaji wakati mgumu na pia kauli hii haiwaandani Wamachinga kutoka sehemu hizo kwa haraka kwa kuhofia matumizi ya nguvu.

Mimi naona ilibidi aseme yafuatayo;

✓ Biashara holela ni marufuku nchini. Watu watafanya biashara kwenye maeneo rasmi tu.

✓ Walioko maeneo yasiyo rasmi kama vile kwenye road reserves,mbele ya fremu za biashara za watu wengine hawaruhusiwi kuendelea na biashara maeneo hayo.

✓ Maafisa wa mipango Miji na Majiji wataelekeza ni maeneo gani rasmi ya kufanya biashara na atakaye kaidi "NGUVU" zaidi itatumika..deadline iwekwe watu wajiandae kuhama.

======

Kauli yake ya leo bado itawapa watekelezaji wakati mgumu..Wamachinga hawa hawataondoka maeneo hayo bila nguvu kubwa kutumika kwa watakaokaidi.
Sasa si uwaeleweshe na wengine...
Si tulielewa hivyo.
😂😂😂😂
 
Ni ngumu ndio ila hatuna budi kufanya sasa hivi wakiachwa hivi na population inazidi kuongezeka hii nchi itakuwa kama jalala..

Najua kila mtu inabidi apeleke mkono kinywani lakini sio kwa kuvurugavuruga utaratibu hivi aisee..Barabara zinatengenezwa then zinaanza kuzibwa tena.
Miji inanuka kupitia wamachinga. Mikojo inawekwa kwenye chupa za maji, vinyesi kwenye mifuko walio ondoa bidhaa.
 
hapo ndipo tatizo lilipo; Chama gani kitakachopishwa na CCM iwapo vyama vyenwe ndiyo hivi. Hata kama CCM ingeendelea kuwa Madarakani, iwapo vyama vya upinzani vingekuwa na nguvu, haingefanya hayo yanayolalamikiwa. Zamani sana ilikuwa mtu akionekana na nguo za kijani za CCM anazomewa, leo hii hali siyo hivyo.
'vyama vyenyewe ndio hivi... ' , ni kauli potofu. CCM hakuanza kama ilivyo. Vyama vya upinzani vinateswa na serikali ya CCM visikuwe, lakini unaona, vyama vyenyewe ndio hivyo. Viongozi wa upinzani nyumba zao ni mahabusu, sebule zao ni mahakamani, lini watajenga vyama vyao? Viongozi wa CCM wanafanya mikutano na wananchi kila siku, wapinzani hata mikutano ya ndani hawaruhusiwi, wewe unaona vyama vyenyewe ndio hivyo. Ujinga wa watu wa aina yako ndio nguvu ya CCM kuendelea kudumaza maendeleo ya nchi hii.
 
Pia awe muwazi kuhusu katiba mpya na asisingizie kwamba anashughulikia uchumi kwanza.
Kujenga uchumi ni swala endelevu, atafanya sehemu yake na ataondoka. Katiba inahitajika, japo ni mwiba wa samaki kwa CCM.
 
Kwa kweli ni muhimu sana serikali iwe makini na biashara za machinga maani wakiendelea kuwachekea miminiko la vijana kutoka vijijini kwenda mijini litakua tishio.
 
Ni vyema Rais Samia wakati wa kutoa maelekezo yake awe anakuwa wazi nini hasa anataka na atoe kauli zenye nguvu ili ujumbe ufike kwa nguvu pia kwa wahusika wote wa pande mbili.

Leo wakati anatoa hotuba yake mara baada ya kuwaapisha Mawaziri na Mwanasheria mkuu wa Serikali alitoa neno kuhusu hili saga la Wamachinga linaloendelea.

Ameonesha hafurahishwi na biashara hiyo inavyofanyika kiholela na inavyovuruga biashara zinazolipa kodi. Lakini aka sugar-coat maneno yake na sijajua ni intentionally au accidentally..Mhe.Rais amesema wapangwe na nguvu isitumike,watolewe kwa amani.

Kitu ambacho hakiwezekani kirahisi hivyo kwa hawa watu na pia kauli hiyo inawapa watekelezaji wakati mgumu na pia kauli hii haiwaandani Wamachinga kutoka sehemu hizo kwa haraka kwa kuhofia matumizi ya nguvu.

Mimi naona ilibidi aseme yafuatayo;

✓ Biashara holela ni marufuku nchini. Watu watafanya biashara kwenye maeneo rasmi tu.

✓ Walioko maeneo yasiyo rasmi kama vile kwenye road reserves,mbele ya fremu za biashara za watu wengine hawaruhusiwi kuendelea na biashara maeneo hayo.

✓ Maafisa wa mipango Miji na Majiji wataelekeza ni maeneo gani rasmi ya kufanya biashara na atakaye kaidi "NGUVU" zaidi itatumika..deadline iwekwe watu wajiandae kuhama.

======

Kauli yake ya leo bado itawapa watekelezaji wakati mgumu..Wamachinga hawa hawataondoka maeneo hayo bila nguvu kubwa kutumika kwa watakaokaidi.
Mama anangata na kupuliza kwa kauli hiyo legalege nani atakayekubali kuondoka kwa amani
 
Mbona kaweka wazi. Wapangwe vizuri. Maana yake mbele ya frame za biashara nyingine wataondolewa, kwenye road reserves wataondolewa vibanda ambavyo vimejengwa bila vibali vitaondoka, watafutiwe sehemu mwafaka za kufanyia biashara zao. Kipi ambacho hakipo wazi hapo? Nyie mlitaka waswagwe tu kama mtu anaye swaga mifugo yake? Mbona hata mifugo ikiswagwa inakuwa na ulekeo ima inaenda kuchungwa, kupelekwa kwenye kunyweshwa maji, josho, mnadani, machinjioni au kurudishwa zizini. Yuko mwanadamu ambaye thamani yake ni chini ya mifugo?
www unafikiri wataondoka kirahisi hivyo
 
www unafikiri wataondoka kirahisi hivyo

Hakuna njia ya rahisi ya kumuongoza mwanadamu kama utafanikiwa kumuonesha unathamini utu wake, unamuheshimu, kumjali na kumpenda. Zoezi la kuwahamisha wa machinga liwe la ushirikishwaji. Na hapo kwenye kushirikishana na ijulikane kwamba yako mambo serikali itabidi ikompromise.
 
Back
Top Bottom