The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanalea kizazi chenye maadili mema, heshima, na uwezo wa kujenga hoja, ili kuimarisha jamii yenye mshikamano na taifa lenye maendeleo.
Akizungumza mkoani Arusha, Machi 8, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuwa na vijana wanaojiamini badala ya kuwa na kizazi kinachotumia jazba na sauti kubwa bila hoja madhubuti.
Rais Samia pia amewataka vijana kujielewa na kujitambua, akisema kwamba hilo ndilo msingi wa kujenga taifa lenye ustawi, haki na usawa. Ameongeza kuwa Tanzania inapaswa kuendelea kupinga ubaguzi wa aina yoyote katika jamii, huku ikijenga misingi ya maendeleo shirikishi kwa watu wote.
Katika hatua nyingine, Rais Samia amehimiza ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, akisisitiza kuwa usawa wa kijinsia unapaswa kuanza kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuimarisha demokrasia na maendeleo ya taifa.
Rais Samia amehitimisha kwa kusema kuwa amani, mshikamano na haki za kijamii ndizo nguzo za maendeleo endelevu, hivyo kila mwananchi ana jukumu la kuhakikisha usawa wa kijinsia unadumishwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Akizungumza mkoani Arusha, Machi 8, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuwa na vijana wanaojiamini badala ya kuwa na kizazi kinachotumia jazba na sauti kubwa bila hoja madhubuti.
Rais Samia pia amewataka vijana kujielewa na kujitambua, akisema kwamba hilo ndilo msingi wa kujenga taifa lenye ustawi, haki na usawa. Ameongeza kuwa Tanzania inapaswa kuendelea kupinga ubaguzi wa aina yoyote katika jamii, huku ikijenga misingi ya maendeleo shirikishi kwa watu wote.
Katika hatua nyingine, Rais Samia amehimiza ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, akisisitiza kuwa usawa wa kijinsia unapaswa kuanza kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuimarisha demokrasia na maendeleo ya taifa.
Rais Samia amehitimisha kwa kusema kuwa amani, mshikamano na haki za kijamii ndizo nguzo za maendeleo endelevu, hivyo kila mwananchi ana jukumu la kuhakikisha usawa wa kijinsia unadumishwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.