Rais Samia: Tujenge vijana wasio na jazba bali wenye kujenga hoja

Rais Samia: Tujenge vijana wasio na jazba bali wenye kujenga hoja

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanalea kizazi chenye maadili mema, heshima, na uwezo wa kujenga hoja, ili kuimarisha jamii yenye mshikamano na taifa lenye maendeleo.

Akizungumza mkoani Arusha, Machi 8, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuwa na vijana wanaojiamini badala ya kuwa na kizazi kinachotumia jazba na sauti kubwa bila hoja madhubuti.

Rais Samia pia amewataka vijana kujielewa na kujitambua, akisema kwamba hilo ndilo msingi wa kujenga taifa lenye ustawi, haki na usawa. Ameongeza kuwa Tanzania inapaswa kuendelea kupinga ubaguzi wa aina yoyote katika jamii, huku ikijenga misingi ya maendeleo shirikishi kwa watu wote.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amehimiza ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, akisisitiza kuwa usawa wa kijinsia unapaswa kuanza kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuimarisha demokrasia na maendeleo ya taifa.

Rais Samia amehitimisha kwa kusema kuwa amani, mshikamano na haki za kijamii ndizo nguzo za maendeleo endelevu, hivyo kila mwananchi ana jukumu la kuhakikisha usawa wa kijinsia unadumishwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
 
Hoja ni chaguzi huri na haki ndiyo mziki mpya una trend kwa sasa. No reform no election
 
Mzee mwenzenu kada Godfrey Malisa bila jazba wala nini alitoa hoja nzito, lakini badala ya kuitekeleza mmemfukuza, sasa hoja za vijana mtaweza kuzivumilia


View: https://m.youtube.com/watch?v=Gl_enK_qbVg
Tarehe 9 February 2025
KADA WA CCM MALISA AJILIPUA, "RAIS AJIUZURU" AMVAA RAIS SAMIA NA KIKWETE HADHARANI kwa kuvunja katiba ya chama ili kubakia madarakani bila kufuata utaratibu unaoainishwa katika katiba, ...
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanalea kizazi chenye maadili mema, heshima, na uwezo wa kujenga hoja, ili kuimarisha jamii yenye mshikamano na taifa lenye maendeleo.

Akizungumza mkoani Arusha, Machi 8, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuwa na vijana wanaojiamini badala ya kuwa na kizazi kinachotumia jazba na sauti kubwa bila hoja madhubuti.

Rais Samia pia amewataka vijana kujielewa na kujitambua, akisema kwamba hilo ndilo msingi wa kujenga taifa lenye ustawi, haki na usawa. Ameongeza kuwa Tanzania inapaswa kuendelea kupinga ubaguzi wa aina yoyote katika jamii, huku ikijenga misingi ya maendeleo shirikishi kwa watu wote.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amehimiza ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, akisisitiza kuwa usawa wa kijinsia unapaswa kuanza kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuimarisha demokrasia na maendeleo ya taifa.

Rais Samia amehitimisha kwa kusema kuwa amani, mshikamano na haki za kijamii ndizo nguzo za maendeleo endelevu, hivyo kila mwananchi ana jukumu la kuhakikisha usawa wa kijinsia unadumishwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Wamechelewa ccm imejaza vijana machawa , na mbaya zaidi na watu wazima wameisha yakanyaga
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanalea kizazi chenye maadili mema, heshima, na uwezo wa kujenga hoja, ili kuimarisha jamii yenye mshikamano na taifa lenye maendeleo.

Akizungumza mkoani Arusha, Machi 8, 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuwa na vijana wanaojiamini badala ya kuwa na kizazi kinachotumia jazba na sauti kubwa bila hoja madhubuti.

Rais Samia pia amewataka vijana kujielewa na kujitambua, akisema kwamba hilo ndilo msingi wa kujenga taifa lenye ustawi, haki na usawa. Ameongeza kuwa Tanzania inapaswa kuendelea kupinga ubaguzi wa aina yoyote katika jamii, huku ikijenga misingi ya maendeleo shirikishi kwa watu wote.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amehimiza ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi, akisisitiza kuwa usawa wa kijinsia unapaswa kuanza kwa wananchi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuimarisha demokrasia na maendeleo ya taifa.

Rais Samia amehitimisha kwa kusema kuwa amani, mshikamano na haki za kijamii ndizo nguzo za maendeleo endelevu, hivyo kila mwananchi ana jukumu la kuhakikisha usawa wa kijinsia unadumishwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Aahubiri asichokiishi yeye na chama chake.
 
Sasa mbona hilo tatizo liko kwenye inner circle yake na chama chake CCM.

angeanza kuonyesha mfano Kwa kuukataa uchawa na kuacha kazi yake imhukumu,, Watanzania watoe hukumu.
 
Kwasababu hizo, ni kwann sasa ameteua viongizi vijana wa hovyo kama Makonda kuwa RC?!.
Mbona vijana smart wenye utulivu na weledi wapo kibao, ye anatuletea comedians!.
 
Back
Top Bottom