Rais Samia: Vijana limeni; masoko, mashamba ya uhakika yapo

Rais Samia: Vijana limeni; masoko, mashamba ya uhakika yapo

Jamal Akbar

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
413
Reaction score
471
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Wakulima (Nanenane) yaliyofanyika Jijini Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka vijana kujishughulisha na kilimo kwani Serikali imetenga mashamba na imeshatafuta masoko kwa ajili ya mazao yatakayozalishwa.

"Vijana njooni kwenye sekta ya kilimo, tumejipanga kuwapatia mashamba na mashamba hayo yatakuwa na hati zitakazotoka kwa majina yenu wenyewe aidha kwa makundi au kwa mtu mmoja mmoja. Tumejipanga kuwaunganisha na mabenki ili yawapatie mikopo laini (Mikopo ya riba nafuu), tumekaa na mabenki wako tayari. Niwaombe sana vijana ingieni kwenye kilimo." ameeleza Rais Samia

Rais Saima ameeleza kuwa Serikali imejipanga vyema kutafuta masoko na kwamba kila kitakachozalishwa tayari kina soko lake la uhakika.

Amefafanua kuwa ziara anazozifanya nje ya nchi anakwenda kutafuta masoko ya bidhaa zitakazozalishwa na tayari kuna masoko ambayo yanasubiri bidhaa/mazao kutoka Tanzania.
18.jpg
 
Mwambie apambanie kupunguza gharama ya bei mafuta na bidhaa
 
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Wakulima (Nanenane) yaliyofanyika Jijini Mbeya, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka vijana kujishughulisha na kilimo kwani Serikali imetenga mashamba na imeshatafuta masoko kwa ajili ya mazao yatakayozalishwa.

"Vijana njooni kwenye sekta ya kilimo, tumejipanga kuwapatia mashamba na mashamba hayo yatakuwa na hati zitakazotoka kwa majina yenu wenyewe aidha kwa makundi au kwa mtu mmoja mmoja. Tumejipanga kuwaunganisha na mabenki ili yawapatie mikopo laini (Mikopo ya riba nafuu), tumekaa na mabenki wako tayari. Niwaombe sana vijana ingieni kwenye kilimo." ameeleza Rais Samia

Rais Saima ameeleza kuwa Serikali imejipanga vyema kutafuta masoko na kwamba kila kitakachozalishwa tayari kina soko lake la uhakika.

Amefafanua kuwa ziara anazozifanya nje ya nchi anakwenda kutafuta masoko ya bidhaa zitakazozalishwa na tayari kuna masoko ambayo yanasubiri bidhaa/mazao kutoka Tanzania.View attachment 2318146
Kwani sera ya taifa kuhusu kilimo inasemaje?
 
Kalime ujionee miujiza. Hizi ngonjera za kilimo kwanza, kilimo ndo uti wa taifa, kilimo kina masoko ya uhakika, kilimo blah blah zipo enzi na enzi ila angalia hali za wanatanganyika
Mimi nafanya kilimo, labda wewe ndio uende uone miujiza. Karibu Dakawa tulime
 
Kilimo cha kutegemea mvua kimepitwa na wakati.

Tanzania tumejaaliwa underground water ya kutosha tukiongeza na mabwawa mambo ya chakula food security yanakuwa safi.
 
Wanu na mchengerwa wapo mjengoni hadi 2035 bila jasho majimboni mwao!

Ccm hawaamiki, unaweza kuamua kulima, hatafu wakatupia mbegu za bangi ili wapate uhalali wa kukufunga.
 
Wanu na mchengerwa wapo mjengoni hadi 2035 bila jasho majimboni mwao!

Ccm hawaamiki, unaweza kuamua kulima, hatafu wakatupia mbegu za bangi ili wapate uhalali wa kukufunga.
Sasa hapa Wanu na Mchengerwa wametokea wapi?
 
Back
Top Bottom