Rais Samia, wanakudanganya kuwa wapinzani wanakudharau kwa kuwa ni mwanamke

Rais Samia, wanakudanganya kuwa wapinzani wanakudharau kwa kuwa ni mwanamke

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kwa kuangalia siku 100 za kwanza za Rais Samia Suluhu Hassan zilivyokuwa zimeleta matumaini makubwa kwa watanzania, katika kuijenga demokrasia na kuheshimu haki za binadamu, kwa namna alivyopiga U turn, katika siku chache zilizopita, ndipo hapo wananchi wanajiuliza, kimetokea nini tena kwa Rais Samia Suluhu Hassan?

Ningependa kulitolea jibu lake kama ifuatavyo:-

Nilichogundua ni kuwa Rais Samia amedanganywa na watu wake wa karibu kuwa wapinzani wanakupuuza wewe kutokana na maumbile yako ya kike.

Wanaendelea kumpotosha kwa kumwambia kuwa mbona alipokuwepo Magufuli, hukuona wapinzani wakidai Katiba mpya na badala yake wote waliufyata?

Sasa kutokana na Rais Samia naye kuwa na hiyo dhana ya kudharauliwa kutokana na maumbile yake ya kike, naye ndiyo hivyo ameingia "kingi" kwa kuwaamini hao "wapambe" wake naye kushusha rungu lake na "kum-victimize" huyo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Hata hivyo naamini huyu Rais Samia Suluhu Hassan "ali-underestimate" matokeo yake baada ya dhana hiyo.

Kwa kuwa yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu, basi ni kama "amejiapiza" kuwa watakiona cha mtema kuni kutokana na dhana yao hiyo, kwa kuvitumia vyombo vya dola "kumbambikia" Mbowe makosa hayo ya ugaidi, kwa lengo tu la kumkomoa, kutokana na kile anachoamini yeye kuwa Mwenyekiti huyo, amedharau mamlaka yake!

Hata ukifuatilia hotuba zake zinadhihirisha hiyo "inferior complex" aliyo nayo, kwa kuwa mara kadhaa katika hotuba zake, amenukuliwa akijitapa kuwa yeye ni Rais mwenye maumbile ya kike!

Watanzania tunajiuliza, hivi kuna haja gani, kuyasema hayo wakati Watanzania wote tunajua kuwa wewe ndiye Rais wetu na Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vyote vya ulinzi na usalama hapa nchini?
 
Hao washauri wake ni kama wanamlazimisha kutumia mbinu za Magufuli dhidi ya wapinzani, maana wanajaribu kuficha ule udhalimu wa Magu dhidi ya wananchi. Na yeye ameamua kuwaridhisha kuwa anafanya kama Magu kwa kuwakomoa wapinzani. Inaonekana yeye na washauri wanajidanganya kuwa dhalimu alikuwa anapendwa, hivyo wakitumia style yake watapendwa. Nadhani uliona mapokezi ya ndege kwa style zile zile za dhalimu.
 
KUTOKANA NA MAUMBILE YAKE YA KIKE
Kwani kuna wanawake wengine hawana maumbile ya kike??!!
Kwani hukuwahi kumsikia Rais Samia katika hotuba zake akiliongelea hilo kwa msisitizo mkubwa?

Hivi unadhani ni kwanini analiongelea hilo kwa msisitizo mkubwa?

Ni kutojiamini tu kwa kuwa yeye ni Rais mwanamke, wapinzani watakuwa wanamdharau na kumchezea watakavyo!
 
Ulikuwepo wakati anadanganywa?

Em acheni kumtetea kwa kigezo cha kudanganywa sijui kuchafuliwa. Maamuzi ya mwisho anayo yeye sifa nzuri anapewa yeye mbaya mnasema kachafuliwa/anadanganywa/anapotezwa.

Ni yeye yeye hakuna wa kumdanganya acheni kumtetea tetea kinamna
 
Kaka kuua upinzani ni miradi ya police kupiga pesa. Mama alianza kwa kuinyofoa badae wameona wanakosa pesa ndio maana wamerudisha mradi kwa nguvu.

Hii ni moja ya miradi ya TISS na Police ili wapige pesa za umma kupitia mlango wa kuwasaidia Ccm

Bila kujua ndio wanakiua Ccm kabisa.
 
Ulikuwepo wakati anadanganywa?

Em acheni kumtetea kwa kigezo cha kudanganywa sijui kuchafuliwa. Maamuzi ya mwisho anayo yeye sifa nzuri anapewa yeye mbaya mnasema kachafuliwa/anadanganywa/anapotezwa.

Ni yeye yeye hakuna wa kumdanganya acheni kumtetea tetea kinamna
Wapi na wapi Amiri jeshi mkuu udanganywe huku una nyenzo zote kujua Polepole ana mipango gani
 
Viongozi mashuhuri wenye jinsi ya kike wameweza kuweka alama katika uongozi wao kutokana na kujitambua pamoja na kujiamini kuwa wao ni ndio viongozi wa juu wenye dhamana kubwa juu ya uongozi wa nchi zao. Nyuma yao kulikuwa na mfumo mzuri wa kitaasisi uliowawezesha kuchuja habari kabla ya kufanya maamuzi.

Pamoja na kuzungukwa na wahafidhina ndani ya vyama vyao, bado waliweza kusimamia kile wanachokiamini kuwa ni kitu chenye tija katika mustakabali mwema wa nchi zao. Waliishi siku zote kwa kusimamia ukweli hata kama uliwakwaza baadhi ya wahafidhina ndani ya vyama vyao.

Ni jambo lisilokuwa na afya hata kidogo kwa kiongozi mkuu wa nchi na amiri jeshi mkuu kujiona kuwa ni duni mbele ya mfumo dume uliomzunguka, licha ya madaraka makubwa aliyokuwanayo kikatiba. Ndiyo! Yeye ni mwanamke, mama, bibi na mke wa mtu kama vile walivyokuwa viongozi wengine maarufu duniani, lakini inampasa naye ajifananishe nao kwa kusimama kama kiongozi imara na thabiti aliyekuwa na msimamo usioyumba katika maamuzi yake kwa kile ambacho anakiamini moyoni mwake kuwa ni cha kweli, haki na chenye tija kwa taifa analoliongoza.

Screenshot_20210801-093554.jpg


Screenshot_20210801-093619.jpg
 
Wahafidhina wa CCM tayari wameshamaliza kazi,Samia hawezi tena kujinasua kwenye huu mtego wa wahafidhina kwani ameingia mzima mzima
 
Kina Merkel na Thatcher hawakuwahi kujiona wanyonge mbele ya wote waliokuwa wakiwaongoza, wazungu walishaondokana na hizi dhana za mwanamke kuwa dhalili hivyo wanapopewa vyeo vya juu kabisa hawana sababu ya kukimbilia kudai wanaonewa.

Rais Samia ni mtanzania, raia wa nchi ambayo bado wasichana wanazuiwa wasiendelee na sekondari ili wakaolewe, hivyo ni vigumu kwake kutokubaliana na dhana za yeye kutazamwa kama mwanamke kwanza.
 
Kina Merkel na Thatcher hawakuwahi kujiona wanyonge mbele ya wote waliokuwa wakiwaongoza, wazungu walishaondokana na hizi dhana za mwanamke kuwa dhalili hivyo wanapopewa vyeo vya juu kabisa hawana sababu ya kukimbilia kudai wanaonewa.

Rais Samia ni mtanzania, raia wa nchi ambayo bado wasichana wanazuiwa wasiendelee na sekondari ili wakaolewe, hivyo ni vigumu kwake kutokubaliana na dhana za yeye kutazamwa kama mwanamke kwanza.
Lakini mkuu Bukililo huoni kama anapokuwa akisukumwa na dhana ya uduni mbele ya mfumo dume uliotamalaki nchini, basi itamuwia vigumu sana kwake kuwa na maamuzi binafsi isipokuwa kila siku ataishia kuunda kamati ama kuwekewa vikwazo na wahafidhina waliopo ndani ya chama chake.
 
Lakini mkuu Bukililo huoni kama anapokuwa akisukumwa na dhana ya uduni mbele ya mfumo dume uliotamalaki nchini, basi itamuwia vigumu sana kwake kuwa na maamuzi binafsi isipokuwa kila siku ataishia kuunda kamati ama kuwekewa vikwazo na wahafidhina waliopo ndani ya chama chake.
Siamini kwamba kwa asilimia mia moja hana uwezo wa kuamua mambo muhimu yeye mwenyewe. Alipokuwa akiapisha mawaziri aliwaambia wakuu wa mikoa kwamba ya kwake ni maamuzi kwa maana ya kusikiliza ushauri na kuamua kipi kifanyike.
 
Wapi na wapi Amiri jeshi mkuu udanganywe huku una nyenzo zote kujua Polepole ana mipango gani
Hata mi huwa nashangaa hili suala aisee. Kwanza huko ni kumdharau yule mama kua hana maamuzi binafsi kama raisi, kwanza inabidi ukubali hilo kua hana maamuzi binafsi ndipo uje na hoja ya kua anadanganywa.
 
Wanaomdharau Ni kina Gwajima wanaomtukana wazi wazi
Huyu mtu naweza kusema wao ndio wanamtuma, kwa sababu isingekuwa hivyo asingerudia tena na tena, hicho ni kipaza sauti cha magogoni
 
Back
Top Bottom