Rais Samia, Wananchi hatutaki madalali wa kisiasa kuingilia ujenzi wa reli ya SGR, tunataka plan ya Hayati Magufuli iheshimiwe kwenye SGR

Aisee...
Umeyachambua mataputapu kwa vielelezo vyenye timeline
Halafu mpango mzima ulikuwa wa JK, wengine walidandia treni kwa mbele....
 
ULIAMBIWA AU ULISOMA DOCUMENT?HIVI UNDHANI GHARA YA KUJENGA SGR PALE DAR NA DAR TO MOROGORO NI SAWA NA KUTOKA MAKUTOPORA KUJA TABORA. KUMBUKA GHARAMA ZA MWAZO ULIZOAMBIWA BADALA YA KUJISOMEA HAIKUWA YA UMEME..BALI ILIKUWA KAMA YA MKENYA
1. Ulikuwa na sababu ipi ya kutumia capital letter ambayo ni shouting?
2. Gharama za kutoka Dar to Morogoro ni 9 Billion, na kutoka Morogoro to Makutopora ni 10.4 Billion/kilometer!!!

Sasa tueleze kuna kipi kutoka Moro to Makutupora cha kufanya gharama iwe kubwa kiasi hicho, ambacho hakipo kutoka Makutupora kwenda huko kwingine?

Kwamba eti ni reli ya umeme, kwahiyo kwa mifumo ile ya umeme ambayo ipo bado kabisa ndo unataka kutuaminisha imechukua 50% ya gharama iliyotarajiwa hapo kabla?
 
Makadirio ya awali ni kwa reli la viwango vya zamani, reli isiyo ya kisasa.
Huu mkeka uliotandazwa na JPM ni wa viwango vikubwa ndiyo maana gharama zimeongezeka!
Kwanza hujajibu... zile 14.2 billion/kilometer mmezitoa wapi?!

Btw, yaani wakati hata mifumo yenyewe ya umeme haijakamilika, ndo unataka kutuambia inatumia zaidi ya TZS 3 billion/kilometer?!

And FYI, "ukisasa" wa reli hautokani na kuwa electrified au kutokuwa electrified bali unatokana na upana wa reli husika!!

Reli ya kisasa ni SGR, bila kujali kama ni ya umeme au hapana wakati reli ya kizamani ni meter gauge... hata ikiwa ya umeme, bado haitaifanya kuwa ya kisasa!!
 
Aisee...
Umeyachambua mataputapu kwa vielelezo vyenye timeline
Halafu mpango mzima ulikuwa wa JK, wengine walidandia treni kwa mbele....
JK alikuwa na mpango wa reli inayoweza kuaccomodate treni za speed ndogo, JPM akabadili plan, akaja na yenye uwezo wa kuaccomodate speed kubwa zaidi na ya umeme
 
Nadhani ukimsikiliza Kikwwte mwenyewe juu ya aina ya reli aliyokuwa anaiwaza na ile ambayo JPM aliacha inajengwa unaweza kupata picha nzuri zaidi: video hii hapa chini👇

 
Mafisadi watetea wachina na wezi wa kichina naona washaanza ufisadi.. Bahati nzuri sana sanaaa, Mama Samia naamini kwa 100% hawezi kuruhusu huu upuuzi.

Mh. Rais wetu awe makini sana sanaaa na wastaafu wa serikali ya 4 na Spika, sbb Spika amekuwa nae mtetezi wa wachina, hivyo, Mh. Rais wetu naamini yuko macho sana.

Mungu utusaidie, mafisadi wanajipanga na wako tunawaona. Mungu waangamize, Mungu utuokoe watanzania.
 
ULIAMBIWA AU ULISOMA DOCUMENT?HIVI UNDHANI GHARA YA KUJENGA SGR PALE DAR NA DAR TO MOROGORO NI SAWA NA KUTOKA MAKUTOPORA KUJA TABORA. KUMBUKA GHARAMA ZA MWAZO ULIZOAMBIWA BADALA YA KUJISOMEA HAIKUWA YA UMEME..BALI ILIKUWA KAMA YA MKENYA
Makadirio ya awali ni kwa reli la viwango vya zamani, reli isiyo ya kisasa.
Huu mkeka uliotandazwa na JPM ni wa viwango vikubwa ndiyo maana gharama zimeongezeka!
Huyo Chige ni kati ya watu waliokuja ghafla kutetea mradi wa wachina wa bandari ya Bagamoyo muda mfupi baada ya Magufuli kufa. Ana maslahi flani na hao wazalendo waliotajwa. Kwenye thread ile nilimuambia "watanzania hawajasahau ...."

Hivyo nilitegemea atakuja kwa kasi kutetea upigaji huo unaotaka kufanywa kwenye SGR.
Ilikuwa lazima afanye hivyo sababu makala ya gazeti la Jamhuri imeponda uhuni wa mradi wa bandari ya Bagamoyo kwa kuwahusisha wapigaji hao wanaojiita wazalendo.
 
Kwanza unatakiwa ujue tofauti ya plan na utekelezaji. Mwalimu Nyerere aliplan dodoma iwe capital city na ujenzi wa bwawa la umeme kule Rufiji ila si nyerere, mwinyi, mkapa wala kikwete aliyeweza kuanzisha mchakato.

Sifa ya Magufuli ilikuwa kupima jambo na kulitekeleza. Ndio maana alipiga chini bandari ya bagamoyo ambayo muasisi ni jk na akamalizia uwanja wa ndege pamaoja na kujenga fly over ya mfugale ambavyo plan ilitoka serikali ya JK.
 
ULIAMBIWA AU ULISOMA DOCUMENT?HIVI UNDHANI GHARA YA KUJENGA SGR PALE DAR NA DAR TO MOROGORO NI SAWA NA KUTOKA MAKUTOPORA KUJA TABORA. KUMBUKA GHARAMA ZA MWAZO ULIZOAMBIWA BADALA YA KUJISOMEA HAIKUWA YA UMEME..BALI ILIKUWA KAMA YA MKENYA
Na JK alisema plan haikuwa ya umeme. Ila Magufuli kaiboresha zaidi.
 
 
Rais aoneshe "uanamke" wake kwenye mambo kama haya ili kulinda legitimacy yake kwa watanzania.
 
Mimi mtu yeyote anayetetea mradi wa bandari ya bagamoyo huwa namuona mwizi.

Reli walitotaka kujenga serikali iliyopita ilikuwa ya kizamani ila Marehemu aliamua kujenga ya kisasa hilo hata namimi namsifu.

Kwenye suala hili tutaina wezi wenhi wakija na utetezi na kuweka maneno ya kejeli.

Sent from my Redmi Note 9S using JamiiForums mobile app
 
Mbaya zaidi miradi yote hiyo kuanzia SGR mpaka ya UMEME ilikataliwa isikaguliwe na CAG, swala la muda tu tutajua gharama zake.... Tumepigwa balaaaa
 
Hapa hatuzungumzii plan na uasisi wa mradi bali tunazungumzia gharama za mradi!!

Kwamba mkataba na Mchina ulikuwa kujenga 2560m kwa USD 7.6 Billion, ikiwa ni less than TZS 7 billion per kilometer; hapa tunadanganywa Mkataba na Mchina ungegharibu TZS 14.2 Billion per kilometer... yaani twice na taarifa rasmi!

Yaani watu kwa makusudi wanasema uongo ili kulinda legcy!!
 
Nadhani ukimsikiliza Kikwwte mwenyewe juu ya aina ya reli aliyokuwa anaiwaza na ile ambayo JPM aliacha inajengwa unaweza kupata picha nzuri zaidi: video hii hapa chini👇

Wala sina haja ya kusikiliza kwa sababu TAYARI NAFAHAMU, unless kama unataka kuniambia maelezo ya JK yanasema alitaka kujenga Meter Gauge na sio Standard Gauge!!!

Tofauti kati ya reli ya JK na ya JPM ni electrification TU lakini zote ni SGR!!!

Man, tumia common sense!!!

JPM alipoingia tu madarakani akaanza ujenzi wa reli!! Endapo JPM angeleta reli tofauti na plan ya JK, feasilibity study LAZIMA ingeanza upya, na kwahiyo ujenzi usingeanza wakati ulioanza kwa sababu feasilibity study ingechukua muda mrefu!!!

Lakini kwavile tangu zamani ilikuwa ni kujenga SGR, hapakuhitajika new feasilibity study cuz' all you need is either to include what's so-called "third rail" or overhead traction system.

Sisi nadhani tuliamua kwenda na overhead traction system
 
Mbaya zaidi miradi yote hiyo kuanzia SGR mpaka ya UMEME ilikataliwa isikaguliwe na CAG, swala la muda tu tutajua gharama zake.... Tumepigwa balaaaa
Hapo chacha....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…