Rais Samia yuko wapi?

Rais Samia yuko wapi?

Ndugu zangu watanzania wenzangu ni zaidi ya wiki sasa Rais haonekani, yuko wapi. Tunasikia tu ndege yake imeonekana uarabuni, kwani Rais ana likizo? Na kama ni ndio kwanini uarabuni. Huyu mama ameshindwa kuvaa koti la Urais?

Tunaambiwa wafanyabiashara wameficha mafuta kusubiri bei mpya na imeonekana ni kweli. Bei mpya tumeisikia imepanda sana kwa zaidi ya sh. 30.

Wafanyabiashara walijuaje itapanda hivi? Lazima kuna wafanyakazi wa EWURA walishatoa mkeka kabla, rais yuko likizo.

Haya tena Geita jana halmashauri ya mji wodi zimefungwa kisa hakuna dawa, na Waziri wa Afya yuko likizo?
Ulitaka umuone Feri anazulura! Yuko ofisini anachapa kazi.
 
Upungufu wa madawa na mafuta na vitu vinginevyo vilisababishwa na ukosefu wa fedha za kigeni baada ya vita na Iddi Amin wa Uganda !!

Mwalimu alikataa kushusha thamani ya pesa ya Tanzania ili akopeshwe fedha za kigeni na IMF !!
Wanaombeza Mwalimu Nyerere kukataa Fedha za IMF ambazo zilikuwa na masharti magumu, angekubali masharti ya IMF wasingesoma hata kufika Kidato cha Nne.
 
Upungufu wa madawa na mafuta na vitu vinginevyo vilisababishwa na ukosefu wa fedha za kigeni baada ya vita na Iddi Amin wa Uganda !!

Mwalimu alikataa kushusha thamani ya pesa ya Tanzania ili akopeshwe fedha za kigeni na IMF !!
Mpe somo kazaliwa 2000 mambo ya nyerere ayajulie wapi. Jf inawajinga wengi hivi mtu anadiriki kulinganisha kipindi tumetoka vitani na sasa ambapo tunachukua mikopo inayoumiza na ufisadi uliozidi
 
Mpe somo kazaliwa 2000 mambo ya nyerere ayajulie wapi. Jf inawajinga wengi hivi mtu anadiriki kulinganisha kipindi tumetoka vitani na sasa ambapo tunachukua mikopo inayoumiza na ufisadi uliozidi
Kwakweli !
 
Muda wa kupiga pesaa huu ,mlitutesa Sana kipindi.cha baba yenu lazima tufidiee

Sent from my Infinix X624 using JamiiForums mobile app
Tanzania itachukua Miaka mingi sana kumpata Rais kama Magufuli Ambae alikua kama baba kwa watu wake.

Siku Alipo fariki Tanzania tuliondokewa na MTU muhimu sana. Mungu Aturehemu watanzania.
 
Tanzania itachukua Miaka mingi sana kumpata Rais kama Magufuli Ambae alikua kama baba kwa watu wake.

Siku Alipo fariki Tanzania tuliondokewa na MTU muhimu sana. Mungu Aturehemu watanzania.
Tanzania ndiyo Nchi imeibeba Dunia katika Ulimwengu wa Roho,

Ni Nchi ya AGANO.

Kuondoka Kwa Magu kutasababisha Dunia kupitia njia ngumu sana Hadi pale Nuru itapoangaza tena NYIKANI.

Aamen
 
Tanzania ndiyo Nchi imeibeba Dunia katika Ulimwengu wa Roho,

Ni Nchi ya AGANO.

Kuondoka Kwa Magu kutasababisha Dunia kupitia njia ngumu sana Hadi pale Nuru itapoangaza tena NYIKANI.

Aamen
Hebu fafanua unaposema TZ imeibeba dunia unamanisha nini
 
Back
Top Bottom