Rais si mkweli, Mawaziri si wakweli, Mkuu wa jeshi, mkuu wa polisi na polisi wake SI WAKWELI.

Rais si mkweli, Mawaziri si wakweli, Mkuu wa jeshi, mkuu wa polisi na polisi wake SI WAKWELI.

field marshall1

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2017
Posts
1,171
Reaction score
2,732
Uongo umeshakuwa kitu cha kawaida katika nchi yetu, Serikali yetu haikuwahi kuaminika na itaendelea kutoaminika.

Rais si mkweli, mbabe, ukandamizaji wa haki za raia, matumizi mabaya ya madaraka, matumizi mabaya ya fedha za umma (Bado tunadaiwa mabilioni kama siyo matrillioni ya shillingi kutokana na tabia yake ya kukosa uvumilivu na kuvunja mikataba ovyo ovyo).

Mawaziri hawasemi ukweli kuanzia kwenye ukuaji wa uchumi hadi kwenye elimu ndiyo maana unasikia siku hizi tamko linatolewa halafu linafutwa utadhani linafanywa na watoto wa darasa la kwanza! Tunaambiwa uchumi unakua....kivipi? Bank ya dunia imeshasema haukui kama jinsi ilivyotabiriwa (Projected) serikali inasema unakuwa kwa 7.2% World Bank wanasema unakua chini ya 6.6% na ni sekta moja ya ujenzi ndiyo unakua kwingine kote hakuna ukuaji...hivyo hakuna uwiano wa ukuaji na wakifanya uchunguzi kwenye quarter hii inayokuja uchumi wetu unaweza ukawa umekuwa kwa asilimia chini ya 5.

Kwenye elimu huko nako wanajichanganya....ni propaganda tupu. Huyu waziri haeleweki anafanya nini? Anachofanya kwa ufanisi ni kuvifunga Vyuo vikuu badala ya kuvisaidia ili vikue....yeye anakomesha tu, Wahitimu wa darasa la saba wengi kwa malaki waliofaulu wamekosa nafasi ya kuingia kidato cha kwanza.....wanafunzi hawa watakuwa mitaani wakipigana vikumbo na wanafunzi wa vyuo vikuu binafsi na wa vyuo vya kati, na vya waalimu waliomaliza ambao hawana ajira kwa miaka mitatu sasa, TUMEAMBIWA HAKUNA KUAJIRI SASA HADI KIBALI KITAKAPOTOLEWA NA SASA IMESHAPITA MIAKA MITATU na hakuna mpango wa kuwasaidia, Hawa wahitimu watakaa bila kazi kwa miaka yote hii?

Serikali ikiambiwa hilo ni bomu linalosubiri kupasuka wanaanza kukamata hao wanaowakumbusha wajibu wao! Gavana wa benki kuu yeye kazi yake kufunga Mabenki badala ya kuyasaidia ili yakue yaweze kuwafikia wananchi hadi wa vijijini...... Gavana hana elimu ya fedha, alikuwa mwalimu wangu pale Mlimani.

Waziri wa Fedha anasema hali itakuwa ngumu kwa kuwa wafadhali wamepunguza misaada.....Hivi kweli kupunguza misaada tu kunaweza kufanya hali ikawa mbaya hivi? Hapo bado hawajakata misaada yote! Mbona tuliambiwa tunafanya miradi kwa PESA ZETU WENYEWE! Rais kasema kwa msisitizo kuwa pesa zipo sasa waziri anaongea nini? Mpango anatuambia kuwa masharti tuliyopewa ni kukubaliana na ushoga kitu ambacho si ukweli.......SHAME ON WAZIRI MPANGO!

Mbona kuna mambo kumi na tano (15) hataki kuyasema....anaona hilo moja la ushoga tu? Hata hilo la ushoga kama anavyosema huyo waziri halilazimishi nchi kuwatambua mashoga bali linataka lisivunje haki zao za msingi kama kuwakamata na kuwafunga....Mbona Makonda alitajwa? Hiyo sheria ya kuwakamata washukiwa wa ushoga inavunja haki za msingi za binadamu.
Kila waziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wanaropoka angalau waonekane na Magufuli huku wananchi wakiumia.

Mkuu wa majeshi inaonekana naye ana taaluma ndogo (semi-illiteracy) anaingilia mambo ya polisi na mahakama wakati kazi ya jeshi inafahamika ni kulinda mipaka yetu siyo kusimamia ununuzi wa korosho, anafanywa mjinga na rais wake, jeshi linashushwa hadhi limekuwa la propaganda, Juzi akiongea bila aibu amesema jeshi letu kwa ubora ni la 27 duniani.....NI KWA UBORA UPI?

Jeshi hili lenye obsolete equipments kama ndege za mwaka 1965 za shenyang J-6 na J-7 ambazo hazitumiki tena duniani zipo kwenye museum, au helicopters (Eurocopters, bells)ambazo siyo "gunship" kwa strength tupo namba 98 na 99 kwa ubora, level moja na Sudan kusini, tumeshindwa na majirani zetu isipokuwa Burundi tu.

Mkuu wa majeshi kudanganya hakusaidii sana....uwe mkweli acha habari za kuokoteza au hisia zako.....Tafuta facts la sivyo utajiabisha na kuaibisha nchi yetu.

Mkuu wa polisi na polisi wake hawa ndiyo maarufu kwa kudanganya ila uwongo wao hauna akili hata kidogo....Hilo la MO Dewji limewaondolea heshima, utekaji feki mlioufanya hata kwenye michezo ya katuni ya watoto haupo.....Ahsanteni sana kwa kutupa moyo kuwa watekaji wa MO walimrudisha salama na bunduki zao.....HILO LINAWEZEKANA TANZANIA TU! Mmetuaminisha kuwa watekaji hao ni watu wema sana na wameshaacha uhalifu.....Vipi kuhusu vidole vyao (Fingerprints zao kwenye bunduki na kwenye hilo gari fake?) mmeshazipata? Mmetuacha hoi na hiyo CCTV zenu............Hongereni sana!

Makonda aliwaona wazungu wawili ila walibadilika baadaye wakawa wa- South Africa weusi......Kweli hiyo Bongo movie ni kali.
Tanzania tunarudi nyuma miaka 50. kwa uongozi huu wa Magufuli na wasaidizi wake.
 
Uongo umeshakuwa kitu cha kawaida katika nchi yetu, Serikali yetu haikuwahi kuaminika na itaendelea kutoaminika. Rais si mkweli.
Mkuu FM1, kwanza title ya bandiko kutokuwa mkweli ni tofauti na content ya kuwa muongo!.

Bila kuingilia uhuru wako wa maoni, japo nakiri inconsistency ya rais Magufuli katika baadhi ya mambo, lakini kiukweli kabisa ukimuondoa Mwalimu Nyerere, rais Magufuli ndiye rais wa pili wa Tanzania ambaye ni mkweli hadi kupindukia.

Rais Magufuli ni Mkweli Daima!. Jee Tumuunge Mkono Rais Wetu Katika Kila Ukweli Wake, Hata Kama Uko Kinyume cha Katiba, Sera na Ilani?. - JamiiForums

"Pongezi Rais Magufuli Kuwa Mkweli Daima. Tuanzishe Church of Africa, Tuoe Wake Wengi, Tuzae Watoto Wengi?" - JamiiForums

P.
 
Sina uhakika Paschal kama zina utofauti. Labda.....
kutokuwa mkweli ni neno pana, not being truthful kwa kukosea, wrongly, lakini kuwa muongo ni lier telling lies kudanganya.

Mfano kusema sukari ilikuwa TZS 5,000 au Saadam rais wa Kuwaiti ni kuteleza tuu ulimi by being not correct lakini sio kudanganya.
P.
 
Pale unaposikia mtu akisema Bwana fulani elimu haijamkomboa.. ndio sasa kwa viongozi wetu.
Nilishangazwa pia na hotuba ya Professor Kabudi akiongea na Diaspora....Anadanganya kuwa muuaji wa Kennedy au MLK hakupatikana na anatafutwa hadi leo....Hivi unadanganya hadi kwenye kitu ambacho kipo wazi???? Huyu huyu alishasema tofauti kwenye bunge la katiba lakini alikuja kubadilika kwa nyuzi 360. Polepole naye alisema CCM haiwezi kushinda bila kuiba leo anafanya tofauti....wame-disown maneno yao.....wakiulizwa wanakuja juu...HIVYO KUNA CREDIBILITY KWA VIONGOZI WETU?
Mkuu kila siku anadanganya mara "tunafanya kwa pesa zetu" nk. Hakuna credibility kabisa kwa nchi za wenzetu wangejiuzulu na wasingechaguliwa kama wanagombea kwenye ofisi za umma.
 
Huenda ulikua na hoja nzuri
Ila Lugha ya Tutajuaje kama....... imekuharibia andiko lko
Umevuka mipaka
 
Mkuu FM1, kwanza title ya bandiko kutokuwa mkweli ni tofauti na content ya kuwa muongo!.

Bila kuingilia uhuru wako wa maoni, japo nakiri inconsistency ya rais Magufuli katika baadhi ya mambo, lakini kiukweli kabisa ukimuondoa Mwalimu Nyerere, rais Magufuli ndiye rais wa pili wa Tanzania ambaye ni mkweli hadi kupindukia.

Rais Magufuli ni Mkweli Daima!. Jee Tumuunge Mkono Rais Wetu Katika Kila Ukweli Wake, Hata Kama Uko Kinyume cha Katiba, Sera na Ilani?. - JamiiForums

"Pongezi Rais Magufuli Kuwa Mkweli Daima. Tuanzishe Church of Africa, Tuoe Wake Wengi, Tuzae Watoto Wengi?" - JamiiForums

P.
Naomba niseme ukweli huu. Rais Magufuli ni muongo, kwanza anadanganya kuhusu Ukuaji wa uchumi, pili anajua kabisa kuwa wapinzani wanatekwa na wanapelekwa wapi, Tatu anajua Tundu Lissu alipigwa risasi na akina nani na anajua fika ni nani ali-order huo udhalimu, nne anajua anadanganya kuhusu hizo projects anazofanya kuwa tunatumia pesa zetu wakati siyo kweli.
Nikisema siyo mkweli nina maana kwa kiingereza "he is lying" Nitabadilisha heading.
 
Ukitaka kufanikiwa kwasasa wewe jitoe ufahamu na usifie kila jambo la sizonje hata kama yeye mwenyewe anajua amefanya ujinga
, Hakuna kitu anapenda kama sifa.

Ndio maana hadi kabudi kiakili amegeuka kama mtoto wa darasa la 4 kisa Kulinda ugali, kwasababu ukimpatia changamoto basi jiandae kupotea.

kiufupi wananchi tumetwishwa zigo la miba.. hakuna msaada zaidi ya maumivu.
 
Mkuu FM1, kwanza title ya bandiko kutokuwa mkweli ni tofauti na content ya kuwa muongo!.

Bila kuingilia uhuru wako wa maoni, japo nakiri inconsistency ya rais Magufuli katika baadhi ya mambo, lakini kiukweli kabisa ukimuondoa Mwalimu Nyerere, rais Magufuli ndiye rais wa pili wa Tanzania ambaye ni mkweli hadi kupindukia.

Rais Magufuli ni Mkweli Daima!. Jee Tumuunge Mkono Rais Wetu Katika Kila Ukweli Wake, Hata Kama Uko Kinyume cha Katiba, Sera na Ilani?. - JamiiForums

"Pongezi Rais Magufuli Kuwa Mkweli Daima. Tuanzishe Church of Africa, Tuoe Wake Wengi, Tuzae Watoto Wengi?" - JamiiForums

P.
Brother nazidi kukushushia heshima huku tunapoelekea kwa kumtetea huyo mtu. Katekeleza lipi kati ya aliyoongea hapo hadi sasa? Tusimwite muongo kwa hii style? Yeye anashughulika na kumkomoa mbowe tu. Ipo siku yake usiyo na jina yajaView attachment vid_BpV3dCBBNOI.mp4
 
Nilishangazwa pia na hotuba ya Professor Kabudi akiongea na Diaspora....Anadanganya kuwa muuaji wa Kennedy au MLK hakupatikana na anatafutwa hadi leo....Hivi unadanganya hadi kwenye kitu ambacho kipo wazi???? Huyu huyu alishasema tofauti kwenye bunge la katiba lakini alikuja kubadilika kwa nyuzi 360. Polepole naye alisema CCM haiwezi kushinda bila kuiba leo anafanya tofauti....wame-disown maneno yao.....wakiulizwa wanakuja juu...HIVYO KUNA CREDIBILITY KWA VIONGOZI WETU?
Mkuu kila siku anadanganya mara "tunafanya kwa pesa zetu" nk. Hakuna credibility kabisa kwa nchi za wenzetu wangejiuzulu na wasingechaguliwa kama wanagombea kwenye ofisi za umma.
Uongo wa Watanzania huanzia kwenye familia na baadaye unakuwa wa jamii nzima.

Tuliambiwa hapa kwamba wakati serikali ya 5 ikiingia madarakani sukari ilikuwa kilo 5000 na wakashusha hadi 1800/2000.

Jambo hili ni baya sana.

Halafu , hivi mtu msema kweli anajipima yeye kuwa msema kweli? Anajitangaza yeye kuwa msema kweli? Siyo matendo na kauli zako vitakavyokufanya uonekane msema kweli?
 
Back
Top Bottom