Rais Trump Ametimiza Tena Unabii Mwingine!!

Rais Trump Ametimiza Tena Unabii Mwingine!!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Mdogo, mdogo, mambo yaliyotabiriwa na kuandikwa kwenye Biblia yanazidi kutimia. Katika kitabu cha 2 Timotheo 3:1-17 BHN imeandikwa hivi:
"Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake."

Kitendo cha Rais Donald Trump kutoa agizo la kusitisha misaada ambayo Marekani ilikuwa ikitoa kwa nchi mbalimbali, kinatimiza unabii huo(watu watakuwa na ubinafsi).

Kitendo cha Rais Trump kutaka kusaini kwanza mikataba ya madini Ukraine na DRC ndio misaada ya ulinzi itolewe kinatimiza unabii huo(wenye tamaa ya fedha).

Kitendo cha Rais Trump kumnenea Rais Zelensky maneno yaliyomfanya anyong'onyee, kinatimiza unabii huo(wenye majivuno, wenye kujiona).

Hakika hizi ni siku za mwisho. Yesu amekaribia kuja. Hatuijui siku wala saa, lakini tukeshe kwa kuishi maisha matakatifu; maana kwa siku na saa tusiyodhani Yesu atakuja kuwanyakua wanaomwamini tu na kuwapeleka mbinguni. Watakaoachwa watabaki kwenye dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Habari za dhiki hiyo kuu zimeandikwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Let all endowed with the faculty of hearing perceive and discern.
 
Mdogo, mdogo, mambo yaliyotabiriwa na kuandikwa kwenye Biblia yanazidi kutimia. Katika kitabu cha 2 Timotheo 3:1-17 BHN imeandikwa hivi:
"Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake."

Kitendo cha Rais Donald Trump kutoa agizo la kusitisha misaada ambayo Marekani ilikuwa ikitoa kwa nchi mbalimbali, kinatimiza unabii huo(watu watakuwa na ubinafsi).

Kitendo cha Rais Trump kutaka kusaini kwanza mikataba ya madini Ukraine na DRC ndio misaada ya ulinzi itolewe kinatimiza unabii huo(wenye tamaa ya fedha).

Kitendo cha Rais Trump kumnenea Rais Zelensky maneno yaliyomfanya anyong'onyee kinatimiza unabii huo(wenye majivuno, wenye kujiona).

Hakika hizi ni siku za mwisho. Yesu amekaribia kuja. Hatuijui siku wala saa, lakini tukeshe kwa kuishi maisha matakatifu; maana kwa siku na saa tusiyodhani Yesu atakuja kuwanyakua wanaomwamini tu na kuwapeleka mbinguni. Watakaoachwa watabaki kwenye dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Habari za dhiki hiyo kuu zimeandikwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Let all endowed with the faculty of hearing perceive and discern.
Ni lini Mambo hayo na Chanzo chake nini mkuu?;!!
 
yani mtu aamue kuacha kukusaidia ili ijitegemee wee useme ndio mwisho ama khyiama wee utakua boya sana mleta uzi, kalime hakuna mambo rahisirahisi sikuhizi.
 
yani mtu aamue kuacha kukusaidia ili ijitegemee wee useme ndio mwisho ama khyiama wee utakua boya sana mleta uzi, kalime hakuna mambo rahisirahisi sikuhizi.
Sawa, mwanangu, fanya haraka ujitegemee, utengeneze ARVs kwa wingi maana Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na Ukimwi (UNAIDS), ameonya kuwa idadi ya maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI (HIV) huenda ikaongezeka mara sita zaidi kwa sababu ya usitishwaji huo wa misaada.

Wakati wa Nuhu watu walikuwa wanaambiwa hivi hivi, gharika itatokea, wakapuuza. Mwisho wa siku gharika ikawaramba wabishi wote kama wewe.
 
Wote tunatambua kwamba tabia kama ubinafsi, tamaa ya fedha, na majivuno zimekuwa sehemu ya asili ya binadamu tangu zamani na pia tabia hizi zimeonekana sehemu nyingi katika masimulizi ya biblia.

Je, tunapaswa kuzingatia unabii wa Biblia kuhusiana na ubinafsi kama ni sehemu ya dalili ya 'siku za mwisho' au ni sehemu tu ya tabia zisizobadilika za kibinadamu ambazo zimekuwepo tangu enzi za kale?

Ikiwa Biblia inataja mambo kama ubinafsi, tamaa ya fedha, na majivuno kama sehemu ya tabia ya binadamu ambayo imekuwa ikijirudia kwa muda mrefu toka agano la kale, je, tunaweza kusema kwamba unabii wa Biblia ni tu tathmini ya mambo ya kawaida ambayo lazima yatokee?

Zingatia kwamba Ubinafsi ulikuwepo hata kipindi Yesu anatabiri huo unabii.
 
Kabla ya Trump

Ubinafsi haukuwepo?

Tamaa ya fedha haikuwepo?
Yalikuwepo hayo unayosema, lakini sasa yanaongezeka. Kuongezeka kwa maasi ni dalili pia ya siku za mwisho. Mt 24:12
Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.
Ulikuwa unapenda kumsaidia jirani sasa unasema ajitegemee, hiyo ni nini kama sio upendo kupoa.
 
Wote tunatambua kwamba tabia kama ubinafsi, tamaa ya fedha, na majivuno zimekuwa sehemu ya asili ya binadamu tangu zamani na pia tabia hizi zimeonekana sehemu nyingi katika masimulizi ya biblia.

Je, tunapaswa kuzingatia unabii wa Biblia kuhusiana na ubinafsi kama ni sehemu ya dalili ya 'siku za mwisho' au ni sehemu tu ya tabia zisizobadilika za kibinadamu ambazo zimekuwepo tangu enzi za kale?

Ikiwa Biblia inataja mambo kama ubinafsi, tamaa ya fedha, na majivuno kama sehemu ya tabia ya binadamu ambayo imekuwa ikijirudia kwa muda mrefu toka agano la kale, je, tunaweza kusema kwamba unabii wa Biblia ni tu tathmini ya mambo ya kawaida ambayo lazima yatokee?

Zingatia kwamba Ubinafsi ulikuwepo hata kipindi Yesu anatabiri huo unabii.
Ni kweli kwamba ubinafsi, tamaa ya fedha, na majivuno vimekuwepo tangu zamani, hata katika maandiko ya Biblia. Ukitaka kuelewa vizuri ujumbe wa Biblia, usisome sura moja tu ukaishia hapo. Soma kwa kulinganisha na sura za vitabu vingine. Hilo Andiko la 2 Timotheo 3:1-5 utalielewa vizuri ukisoma na Mt 24:12. Hapo tunaambiwa maasi yataongezeka. Kuongezeka kwa maasi ni nini. Ni kuongezeka kwa mmomonyoko wa maadili. A good example: Ushoga. Ushoga ulikuwepo hata zamani. Lakini sasa angalia jinsi unavyopigiwa kampeni hadharani. Ni nini hiyo kama sio kuongezeka kwa maasi kulikotabiriwa.
 
MAREKANI HAINA WAJIBU WA KUSAIDIA NCHI ZINGINE, NI CHARITY SIO LAZIMA.

Viongozi wetu wa Afrika wanaopiga kelele wananunua mashangingi V8 ya milioni 300, wake za maraisi, mawaziri wakuu, maspika wanalipwa mabilioni, Misaada inadonolewa 😐
 
Ni kweli kwamba ubinafsi, tamaa ya fedha, na majivuno vimekuwepo tangu zamani, hata katika maandiko ya Biblia. Ukitaka kuelewa vizuri ujumbe wa Biblia, usisome sura moja tu ukaishia hapo. Soma kwa kulinganisha na sura za vitabu vingine. Hilo Andiko la 2 Timotheo 3:1-5 utalielewa vizuri ukisoma na Mt 24:12. Hapo tunaambiwa maasi yataongezeka. Kuongezeka kwa maasi ni nini. Ni kuongezeka kwa mmomonyoko wa maadili. A good example: Ushoga. Ushoga ulikuwepo hata zamani. Lakini sasa angalia jinsi unavyopigiwa kampeni hadharani. Ni nini hiyo kama sio kuongezeka kwa maasi kulikotabiriwa.
Je, unaweza ukanitajia mfano wa Ushoga wa nyakati za sasa ambao unazidi ule uovu wa sodoma na Gomola?
 
Mdogo, mdogo, mambo yaliyotabiriwa na kuandikwa kwenye Biblia yanazidi kutimia. Katika kitabu cha 2 Timotheo 3:1-17 BHN imeandikwa hivi:
"Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake."

Kitendo cha Rais Donald Trump kutoa agizo la kusitisha misaada ambayo Marekani ilikuwa ikitoa kwa nchi mbalimbali, kinatimiza unabii huo(watu watakuwa na ubinafsi).

Kitendo cha Rais Trump kutaka kusaini kwanza mikataba ya madini Ukraine na DRC ndio misaada ya ulinzi itolewe kinatimiza unabii huo(wenye tamaa ya fedha).

Kitendo cha Rais Trump kumnenea Rais Zelensky maneno yaliyomfanya anyong'onyee, kinatimiza unabii huo(wenye majivuno, wenye kujiona).

Hakika hizi ni siku za mwisho. Yesu amekaribia kuja. Hatuijui siku wala saa, lakini tukeshe kwa kuishi maisha matakatifu; maana kwa siku na saa tusiyodhani Yesu atakuja kuwanyakua wanaomwamini tu na kuwapeleka mbinguni. Watakaoachwa watabaki kwenye dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Habari za dhiki hiyo kuu zimeandikwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Let all endowed with the faculty of hearing perceive and discern.
Bibilia imesema amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu.
Trump amekata utegemezi, tufanye uzinzi tutegemee condom kutoka ulaya, na madawa ya magonjwa ya ngono

Tuache kuondoa mazalia ya mbu, tuzalishe mbu tupate maleria halafu tusubiri net kutoka kwa Trump.

Mungu ametupa ardhi nzuri yenye rutuba na mvua kila mwaka, lakini tunashinda kucheza bao na kupiga soga vijiweni njaa ikitupiga tusubiri Trump atupe msaada

Huko Kongo tunapigana wenyewe weusi kwa weusi, wale wanaoteseka ni watoto wetu na wake zetu, sasa tupigane sisi, njaa ikituuma tumsubiri Trump aje atupe chakula
 
Mdogo, mdogo, mambo yaliyotabiriwa na kuandikwa kwenye Biblia yanazidi kutimia. Katika kitabu cha 2 Timotheo 3:1-17 BHN imeandikwa hivi:
"Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake."

Kitendo cha Rais Donald Trump kutoa agizo la kusitisha misaada ambayo Marekani ilikuwa ikitoa kwa nchi mbalimbali, kinatimiza unabii huo(watu watakuwa na ubinafsi).

Kitendo cha Rais Trump kutaka kusaini kwanza mikataba ya madini Ukraine na DRC ndio misaada ya ulinzi itolewe kinatimiza unabii huo(wenye tamaa ya fedha).

Kitendo cha Rais Trump kumnenea Rais Zelensky maneno yaliyomfanya anyong'onyee, kinatimiza unabii huo(wenye majivuno, wenye kujiona).

Hakika hizi ni siku za mwisho. Yesu amekaribia kuja. Hatuijui siku wala saa, lakini tukeshe kwa kuishi maisha matakatifu; maana kwa siku na saa tusiyodhani Yesu atakuja kuwanyakua wanaomwamini tu na kuwapeleka mbinguni. Watakaoachwa watabaki kwenye dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Habari za dhiki hiyo kuu zimeandikwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Let all endowed with the faculty of hearing perceive and discern.
Uwongo mwingine kama huu ni bora tu usisemwe hadharani, ni haibu kumsingizia Yesu kwa kila kitu. Haya aliyatabiri Hellen G. White toka walipoanzisha kanisa la uzushi la Seventh Day Adventist. Wameropoka vitu vingi kuhusu ujio wa Yesu toka miaka hiyo mpaka leo karibia miaka 200 bado wanamsubiri tu Yesu. Waafrika tunajichosha na kuamini hizi dini za uzushi kwa kweli, inasikitisha mno.
 
Amin nakwambia hamna siku ya mwisho hapa dunuani, Hilo neno "siku za mwisho" walianza kulitmka tangu miaka ya 1980-198... Mara tu ukimwi ulipoingia afrika. Lakin pia mwaka 2000 watu walijua ndio siku za mwisho (fatilia). Kwa kifupi Hilo neno siku za mwisho sio geni.
 
Back
Top Bottom