Rais umewasikiliza wanaotaka katiba mpya! Je, sisi tusiotaka katiba mpya utatusikiliza lini? Tuna hoja!

Rais umewasikiliza wanaotaka katiba mpya! Je, sisi tusiotaka katiba mpya utatusikiliza lini? Tuna hoja!

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Asalaam ndugu zangu..

Nianze kumpongeza Rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya. Wamesikilizwa, na ninasikia mchakato karibia utaanza. Ni jambo jema. Lakini tupo sisi ambao hatukubaliani na mchakato huo. Hatuhitaji katiba mpya na tuna hoja na sababu za msingi. Nchi yetu imekuwa na amani kwa miaka zaidi ya 50 kwa katiba hii. Nchi yetu imekuwa na uchumi unaokuwa vizuri kwa katiba hii.

Kwa sisi tusiotaka katiba, utatusikiliza lini? Na sisi tuna haki ya kusikilizwa kama ulivyowasikiliza hao wanaotaka katiba mpya! Mimi na wenzangu wengi tu tusiotaka katiba mpya, tutasikilizwa lini? Hatutaki kabisa katiba mpya! Tumeona nchi jirani zilizokimbilia katiba mpya kwa minajiri ya ustawi kisiasa na maisha ya watu wetu, lakini imekuwa kinyume chake!

Kenya vurugu tupu! Afrika Kusini vurugu tupu! Nchi zote zilizothubutu kubadilisha katiba ziliingia kwenye migogoro isiyoisha. Please, Rais, hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu.

Asanteni.

Pia soma: Serikali: Mchakato wa Katiba Mpya na maboresho ya Sheria ya vyama vya Siasa na Uchaguzi, sasa kuanza
 
Hivi nyie watu wajinga mnapata faida gani mnapoendekeza chuki?
Asalaam ndugu zangu ..nianze Kumpongeza rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya .. wamesikilizwa na ninasikia mchakato karibia utaanza ni jambo jema ... Lakini tupo sisi yoisha .. please rais hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu ..asanteni
..
 
Asalaam ndugu zangu ..nianze Kumpongeza rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya .. wamesikilizwa na ninasikia mchakato karibia utaanza ni jambo jema ... Lakini tupo sisi ambao hatukubaliani na mchakato huo .. hatuhitaji katiba mpya na tuna hoja na sababu za msingi ..nchi yetu imekuwa na amani kwa miaka zaidi ya 50 kwa katiba hii .. nchi yetu imekuwa na uchumi unaokuwa vizuri kwa katiba hii ... Kwa sisi tusiotaka katiba utatusikiliza lini ? Na sisi tuna haki ya kusikilizwa kama ulivyowasikiliza hao wanaotaka katiba mpya !! Mimi na wenzangu wengi TU tusiotaka katiba mpya tutasikilizwa lini ? Hatutaki kabisa katiba mpya !! Tumeona nchi jirani zilizokimbilia katiba mpya kwa minajiri ya ustawi kisiasa na maisha ya watu wetu lakini imekuwa kinyume chake! Kenya vurugu tupu! Afrika kusini vurugu tupu !! Nchi zote zilizothubutu kubadilisha katiba ziliingia kwenye migogoro isiyoisha .. please rais hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu ..asanteni
..
Duh...!. Mkuu Mganguzi , kwanza nikupongeze kwa bandiko hili na kuheshimu uhuru wa maoni na uhuru wa kijieleza, yaani freedom of expression and freedom of speech.

Dunia ilipoumbwa, hakuna aliyejua dunia ni duara, watu wote kwa kutokujua kwao wakajua umbo la dunia ni umbo bapa.

Galileo Galilee alipogundua telescope na kuliona umbo la dunia kupitia kivuli cha kwenye mwezi, alipotangaza kuwa dunia ni duara, Galileo Galilee aliuwawa kwa kosa la kumkufuru Mungu kwa kitendo chake cha kusema dunia ni duara!.

Ukiwa hujaonja embe dodo ukiambiwa tunda tamu kuliko yote ni pera utaamini mpaka utakapoonja embe dodo ndio utagundua kumbe tunda tamu ni embe dodo.

Ukionja zabibu unagundua ni zabibu, ukionja nanasi unagundua ni nanasi, ukionja tende unagundua ni tende, ukionja asali ndipo utagundua asali ndio funga kazi ya utamu!.

Wewe ni mmoja wa Watanzania wasiojua katiba wala Umuhimu wa katiba mpya, hivyo wameridhika sana na hii katiba pera iliyopo, bila kuonjeshwa katiba embe, katiba nanasi, katiba tende na katiba asali, kamwe hauwezi kujua Umuhimu wa katiba mpya.

Hili la Watanzania kutujua katiba, hata Rais Samia amelisema

Hivyo watu kama akina sisi tuliobahatika kajiuwezo ka kusoma sheria na kuijua katiba, tumejitolea kuwaelimisha wengine Umuhimu wa katiba mpya kwanza kwa kuwaelimisha Watanzania wenzetu elimu ya katiba ili waifahamu katiba.

Angalia bandiko hili elimishi kuhusu kuijua katiba ni la lini na limechangiwa na watu wangapi ili kupata picha ya Watanzania wanavyotaka kuijua katiba Ijue Katiba ya JMT-1: Katiba ni nini, ya nani, ya kazi gani? Msemo "Katiba ndio ila kitu" Una maana gani? Katiba ina umuhimu gani?
Just imagine mtu unajitolea kuelimisha umma kuhusu katiba halafu responses ndio hii!, utaendelea kweli?.

Hivyo watu kama nyinyi mnapojitokeza kusema hamuhitaji katiba mpya, hatuwashangai bali tunawahurumia!.

Laiti ungelijua tungekuwa na katiba bora, Tanzania tungekuwa wapi, ndipo ungeweza kujua tofauti ya utamu wa pera na asali!.

Kama una muda karibu pande hizi
P
 
Asalaam ndugu zangu ..nianze Kumpongeza rais kwa kusikiliza hoja za watu wa kada mbalimbali hasa wa mlengo wa kisiasa wakidai katiba mpya .. wamesikilizwa na ninasikia mchakato karibia utaanza ni jambo jema ... Lakini tupo sisi ambao hatukubaliani na mchakato huo .. hatuhitaji katiba mpya na tuna hoja na sababu za msingi ..nchi yetu imekuwa na amani kwa miaka zaidi ya 50 kwa katiba hii .. nchi yetu imekuwa na uchumi unaokuwa vizuri kwa katiba hii ... Kwa sisi tusiotaka katiba utatusikiliza lini ? Na sisi tuna haki ya kusikilizwa kama ulivyowasikiliza hao wanaotaka katiba mpya !! Mimi na wenzangu wengi TU tusiotaka katiba mpya tutasikilizwa lini ? Hatutaki kabisa katiba mpya !! Tumeona nchi jirani zilizokimbilia katiba mpya kwa minajiri ya ustawi kisiasa na maisha ya watu wetu lakini imekuwa kinyume chake! Kenya vurugu tupu! Afrika kusini vurugu tupu !! Nchi zote zilizothubutu kubadilisha katiba ziliingia kwenye migogoro isiyoisha .. please rais hakuna legacy yoyote utakayoiacha kwa kuleta katiba mpya zaidi ya fujo na vurugu ..asanteni
..
Katiba ni takwa la msingi wa jamii yeyote. Katiba siyo static bali ni dynamic, lazima iendane na mabadiliko ya jamii tuliyopo ili kukidhi masilahi ya makundi tofauti.
 
Back
Top Bottom